Tuhuma za kufanyika kwa ‘madudu’ dhidi ya fedha za kujikimu(Meals and accommodation) kutoka HESLB ndani ya Chuo Kikuu St. Augustine Mwanza

Mac Alpho

JF-Expert Member
Aug 5, 2019
13,677
26,997
Nimegundua kuna madudu na ubabaishaji mkubwa sana wa malipo ya fedha za Kijikimu(Meals and Accomodations) kwa wanafunzi wa Chuo kikuu cha ST. AUGUSTINE MWANZA, ambazo kimsingi ni fedha wanazokopeshwa wanafunzi Ili baadae wazilipe.

Serikali inaingiza hela kwenye account ya chuo mapema tu, alafu chuo kinatafuta namna ya kukaa na hizo hela kwa muda mrefu Ili wazizalishe na wapige Faida ndefu kupitia benki ya CRDB ambao ni wabia wao wakuu (Mwanafunzi wa SAUT ni marufuku kufungua account nyingine tofauti na CRDB☹️).

Wanafunzi wanalazimishwa kujisajili kwa mfumo wa kuchukua hela kwa finger print(ambalo ni jambo zuri), lakini unaambiwa kila hela ikiingia mwanafunzi analazimika kukwatwa Sh 15000tsh,hii hela ukizidisha kwa idadi ya wanufaika wa mikopo hapo chuoni ni hela ndefu sana,ambayo nayo hugawanywa Kati ya chuo na benki husika.

Mimi ninasomesha mwanangu wa nne wa kiume hapo SAUT, course ya Electrical engineering mwaka wa kwanza, ila tangu apokee boom lake la kwanza mwezi wa 12,ambalo kimsingi alitakiwa alipokee mwezi wa 11, mpaka sasa unaelekea mwezi wa tatu hajapokea boom la pili ilihali vyuo vingine wanafunzi wamepewa tangu mwezi wa kwanza. Kimsingi sioni Sasa faida ya hio mikopo maana kama mzazi inanilazimu kutoka fedha ndefu tu Ili kumsaidia mwanangu ambae yupo mbali na nyumbani. Kimsingi sishindwi kumhudumia mwanangu, ila leo aliponipigia simu kuomba hela za matumizi, imenifanya nifikirie mengi sana juu ya huu ukiritimba unaofanywa na hiki chuo cha kipumbavu juu ya watoto.

👉🏿Hivi mtoto (tuchukulie wa kike) ambae anatokea familia masikini, anaesoma mbali kabisa na nyumbani kwao, asiekuwa na ndugu huko anaposomea, unapomcheleweshea fedha kwa muda mrefu hivyo(zaidi ya mwezi mmoja na nusu), unamtengenezea mazingira gani, kama sio kuandaa kizazi cha watoto wanaotegemea ngono Ili Kijikimu kimaisha? Na ndiomaana vyuo vingi vimekuwa vitovu vikubwa vya shuguli za ukahaba. Watoto wadogo hawana namna nyingine ya kujisaidia mwisho wanaangukia kwenye tabia za ajabu.

👉🏿Mwanafunzi anapata wapi muda wa kuweka mawazo yake kwenye masomo ikiwa mfukoni hata hela ya kula tu, hana?

Hili tatizo sijawahi kulisikia kabisa kwenye vyuo vingine isipokuwa SAUT,hii inaonyesha kuna ushenzi mkubwa sana hapo.Naanza kupata hata Wasiwasi juu ya kiwango cha elimu kinachopatika kwenye hicho chuo,huenda ni cha chini sana.

NB: Uongozi mzima wa ST. AUGUSTINE UNIVERSITY OF TANZANIA badilikeni haraka iwezekanavyo, hiki mnachokifanya ni swala la kipumbavu sana. Yaani fedha zenyewe wanafunzi wanalewa kama mikopo, Ili baadae waulipe alafu tena upatikanaji wake unakuwa ni mpaka baadhi ya watu fulani wabembelezwe,huu ni upuuzi usiovumilika.
 
Nna ndugu zangu wawili wako hapo, wanatoa maelezo km haya huwa nadhani ni uongo, kumbe ni kweli tupu, sasa naamini hili.
 
Duh,

Kama imekaa hivyo ni habari sana, isije tu ukawa kijana kalitapanya boom kwa warembo halafu akarudisha mpira kwa kipa aanzishe mchezo upya.
Hapana mkuu kabla sijaleta hii taarifa hapa,nimejihakikishia kwa 100%.Wiki mbili zilizopita iliyopita aliponiomba kiasi kikubwa cha fedha kwaajili ya matumi(150,000), nikamkazia hadi nilipopata namba ya Loan officer wa chuo kutoka kwa rafiki angu ambae ni staff hapo chuoni.

Nilipoongea nae akanambia hela za wanafunzi wa mwaka wa kwanza,zitaingizwa kwenye account zao ijumaa ya wiki hii, nililalamika sana, akadai hiyo ni kwasababu eti wamechelewa kusain, niwe mvumilivu. Leo ijumaa imefika mtoto anapiga tena simu kuomba hela, eti hajapata boom. Napiga namba ya Loan officer mpaka Sasa haipatikani, huu si upumbavu huu.

Na Ili ujue ni washenzi, haya yanafanyika kwa first year (ambao kimsingi wanachukuliwa kama washamba), continuous wote washapata hela zao tangu mwezi wa pili mwanzoni.
 
Nna ndugu zangu wawili wako hapo, wanatoa maelezo km haya huwa nadhani ni uongo, kumbe ni kweli tupu, sasa naamini hili.
Huo ni ukweli mtupu. Kibaya zaidi mazingira ya chuo hayaruhusu wanafunzi kuwa na kidomodomo kwakua hatima yao inashikiliwa na chuo chenyewe, ila kwa mazingira hayo ni hakika kuwa wanateseka sana.
 
Nyie mliopitia ukuruti tukiwaambia tuandamane kudai haki zetu na bumu mnagomaga Sana nyie, sijui mnakuwa mmelishwa nini kwenye vichwa vyenu

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna upumbavu mwingi sana kwenye hivi vyuo hasa vya private.Vyuo vinaizungusha kwanza hela kwenye mabenki Ili vipate faida, bila kujali wanafunzi wanaishije mitaani.
 
Hapa naona kama mwanafunzi anapiga pesa kwa mzazi.

Mfumo wa Fingerprint ni mzuri sana na hauna longolongo, hauingiliani na maamuzi ya Chuo, mfumo huu ni kati ya Bodi, crdb na mnufaika, kuhusu makato ya Tshs.15000/- sio kweli, kwa kuthibitisha hili muombe mwanao Bank statement na uilete Hapa.

La kuzungusha fedha! Sasa hivi tofauti na zamani, pesa ikiingia haitakiwi kuchelewa na serikali inafuatilia.

Serikali imeweka watu vyuoni kupata taarifa na viongozi wa serikali ya wanafunzi kupitia TAHLISO Wako active sana kupata taarifa za vyuo.
 
Hapa naona kama mwanafunzi anapiga pesa kwa mzazi...
Aiseeeh....tafuta mwanafunzi yoyote wa mwaka wa kwanza anesoma SAUT uliza kama wote wamepata boom.Kuhusu makato ya fingure prints huyo tsh 15,000 si habari za kubumba.Na baadhi ya data nimezipata kutoka kwa mtu ambae ni staff wa SAUT, na hakuna sababu yoyote ile ya yeye kunidanganya.
 
inamaana bodi ya mikopo wanakicheleweshea chuo hicho tu, mbona hayo mambo hatuyasikii vyuo vingine?
Mkuu kuna watu wanadhani ukiritimba kwenye ofisi za umma unaisha kizembe tu kwa hizi kiki za Rais ambazo mara nyingi zinalenga mtu mmojammoja badala ya kurekebisha mifumo yote kwa ujumla.
 
HUU UONGO
MIMI NIKO HAPO SAUT NA HAKUNA HIKI
PESA INAINGIA MOJA KWA MOJA KUTOKA HESLB NA KINACHOFANYIKA NI VERIFICATION KWA FINGERPRINT MANAKE MWANAFUNZI HATAWEZA KUTOA PESA MPAKA AKATIE KIDOLE

MFUMO HUO UNAITWA DIDIS NA UKO VYUO VYOTE KWA SASA SIO SAUT NA HIYO IMEWEKWA NA CRDB AMBAO NI WABIA WA HESLB NA SIO CHUO CHA SAUT KAMA UNAVYOSEMA WEWE
 
Back
Top Bottom