barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,726
- 32,818
Leo ndio uzinduzi wa Msimu wa kipindi cha Maisha Plus East Africa 2016
Kwa wale wadau na wapenzi wa kipindi hiki,tunaweza kukutana hapa kwa muda wa hizo wiki 8 ambazo washiriki watakuwa ndani ya Kijiji cha Maisha Plus.
Mwaka huu washiriki wanatoka katika nchi za Afrika Mashariki kama Tanzania,Kenya,Uganda,Rwanda na Burundi.Washiriki kutoka Tanzania ni 14,wakati washiriki kutoka nje ya Tanzania ni 16.Haijulikani haswa kijiji kipo maeno gani hapa Tanzania,lkn kwa udodoso wa mambo wakati akitangaza Masoud Kipanya alijisahau ni kusema ili ufike inabidi uvuke daraja la Mto Wami.Hivyo haieleweki haswa uelekeo wa kijiji ulipo.
Washiriki watakaa week mbili za mwanzo bila kuwa na mchunjo.Baada ya week hizo mbili ndipo mtoano utakapoanza.Washiriki watatakiwa kujijengea nyumba za kuishi na watakuwa wanapata mkopo wa shilingi elfu moja kwa siku toka kwenye "bank" ya kijiji na mahitaji toka duka la kijiji.Ujenzi wa nyumba zao na vyoo vya kutumia wataupata kwa kuchimba shimo la udongo la futi sita.Mwisho wa siku mshindi kupata milioni 30.
Kutoka hotel waliyofikia,watakuja kijijini wakiwa wamefungwa vitambaa usoni ili kutojua mahali wanapoenda na mahali walipo.Katika week hizo nane,ni mpambano na mtifuano ndani ya kijiji.
Tanzania inawakilishwa na washiriki kutoka Mbeya,Mwanza,Iringa,Mtwara,Dodoma na Kilimanjaro.
Kupitia JF...Wale "wapenzi" wa Maisha Plus,tujuzane vibweka,vitimbi na matukio ya Kijiji cha Maisha Plus.
Kwa wale wadau na wapenzi wa kipindi hiki,tunaweza kukutana hapa kwa muda wa hizo wiki 8 ambazo washiriki watakuwa ndani ya Kijiji cha Maisha Plus.
Mwaka huu washiriki wanatoka katika nchi za Afrika Mashariki kama Tanzania,Kenya,Uganda,Rwanda na Burundi.Washiriki kutoka Tanzania ni 14,wakati washiriki kutoka nje ya Tanzania ni 16.Haijulikani haswa kijiji kipo maeno gani hapa Tanzania,lkn kwa udodoso wa mambo wakati akitangaza Masoud Kipanya alijisahau ni kusema ili ufike inabidi uvuke daraja la Mto Wami.Hivyo haieleweki haswa uelekeo wa kijiji ulipo.
Washiriki watakaa week mbili za mwanzo bila kuwa na mchunjo.Baada ya week hizo mbili ndipo mtoano utakapoanza.Washiriki watatakiwa kujijengea nyumba za kuishi na watakuwa wanapata mkopo wa shilingi elfu moja kwa siku toka kwenye "bank" ya kijiji na mahitaji toka duka la kijiji.Ujenzi wa nyumba zao na vyoo vya kutumia wataupata kwa kuchimba shimo la udongo la futi sita.Mwisho wa siku mshindi kupata milioni 30.
Kutoka hotel waliyofikia,watakuja kijijini wakiwa wamefungwa vitambaa usoni ili kutojua mahali wanapoenda na mahali walipo.Katika week hizo nane,ni mpambano na mtifuano ndani ya kijiji.
Tanzania inawakilishwa na washiriki kutoka Mbeya,Mwanza,Iringa,Mtwara,Dodoma na Kilimanjaro.
Kupitia JF...Wale "wapenzi" wa Maisha Plus,tujuzane vibweka,vitimbi na matukio ya Kijiji cha Maisha Plus.