Tufundishane Ujasiriamali

Sipo

JF-Expert Member
Jul 25, 2008
2,139
91
Kumekuwa na ongezeko la watu wanaotaka kujua ni jinsi gani ya kujiajiri wenyewe, namaanisha kama mtu mmoja au kama kikundi. Naomba tutumie andiko hili hapa kufundishana ni jinsi gani, mbinu zipi, njia zipi tunaweza kutumia katika kujitegemea wenyewe pasipo kutegemea mishahara na kazi za kuajiriwa ambazo kadri dunia inavyosonga mbele ndio jinsi ambavyo kazi hizi zinakwisha.

Kila mwenye wazo au uzoefu aweke hapa kwa jinsi ajuavyo yeye ilimradi ujumbe ufike kwa jamii kubwa zaidi.


Asanteni kwa ushirikiano mtakaoutoa

Wenu
Sipo
 
Moderator naomba utilie mkazo hili na ikiwezekana tukutanisheni na wataalam na walio nautaalam hapa naomba wajitolee; mfano mimi niko tayari kusaidia ama kushauri kwenye upande wa IT na mambo ya Internet cafe
 
Kumekuwa na ongezeko la watu wanaotaka kujua ni jinsi gani ya kujiajiri wenyewe, namaanisha kama mtu mmoja au kama kikundi. Naomba tutumie andiko hili hapa kufundishana ni jinsi gani, mbinu zipi, njia zipi tunaweza kutumia katika kujitegemea wenyewe pasipo kutegemea mishahara na kazi za kuajiriwa ambazo kadri dunia inavyosonga mbele ndio jinsi ambavyo kazi hizi zinakwisha. Kila mwenye wazo au uzoefu aweke hapa kwa jinsi ajuavyo yeye ilimradi ujumbe ufike kwa jamii kubwa zaidi.

Nina uzoefu!

Nilikuwa kijijini juzi, baba yangu alikuwa na mashine za kusaga kwa miaka mingi, ambazo zimetusomesha sisi.

Baada ya yeye kuugua na kuhamia Dar 2008 alimwachia mradi huo baba mdogo, ambaye ameshindwa kabisa kuendeleza kazi hiyo, na ameishia kukopa fedha na kuzalisha madeni kila mtaa huko nyumbani.

Hawezi kulipa bili za umeme,
Hawezi kufanya maintainance pindi kifaa kikiharibika,
Hawezi kabisa kuwalipa vijana wanaomsaidia.

Nadhani hii inasababishwa na ukosefu wa elimu ya ujasiriamali, ambapo angekuwa nayo angejua jinsi ya kupanga bajeti ya mradi, masuala ya uwiano wa mapato na matumizi, na vitu vya namna hiyo.

Tundiko hili litakuwa la msaada sana kwa wengi, hata kama si members wa hapa, lakini kwa wale tunaoishi nao huko mtaani.
 
Moderator naomba utilie mkazo hili na ikiwezekana tukutanisheni na wataalam na walio nautaalam hapa naomba wajitolee; mfano mimi niko tayari kusaidia ama kushauri kwenye upande wa IT na mambo ya Internet cafe

Kitu kizuri wakuu.Hali mtaani si nzuri kwa ujumla hasa kwa ajili za mfumo rasmi. Sector binafsi inakuwa kwa kasi,lakini sehemu kubwa ya sector hiyo inaweza kuja kutawaliwa na wenzetu. Kwa hiyo ni lazima vijana tuanze kuunganisha nguvu ili tujenge misingi na naamini kwa pamoja tunaweza.

Kitu cha kwanza ninachoweza kuchangia ktk suala la ujasiriamali kwa ujumla, la kwanza ni kujitambua wewe mwenyewe na mazingira yako uliyo nayo ( vipaji,rasilimali,ujuzi,fursa nk). Na la pili ni juhudi ktk kujifunza toka kwa waliofanikiwa na kushirikiana nao.
 
Kitu cha kwanza ninachoweza kuchangia ktk suala la ujasiriamali kwa ujumla, la kwanza ni kujitambua wewe mwenyewe na mazingira yako uliyo nayo ( vipaji,rasilimali,ujuzi,fursa nk). Na la pili ni juhudi ktk kujifunza toka kwa waliofanikiwa na kushirikiana nao.

Naam natuanze; kulikuwa na mpango wa wajasiriamali wa JF kukutana umeishia wapi?

Malila ; tunaweza kuanza kuenlist hayo uliyotaja hapo juu? basi fafanua zaidi nini kinahitajika ktk kila nyanja uliyoitaja?
 
Asante Sipo kwa kuileta hoja. Mie ninapenda sana ujasiriamali maana napenda kuanza kujiajiri mapema. Wastaafu wengi wanapata shida sana kwakuanza kujifunza wakiwa tayari hawana kazi, ninauzoefu na hili kwani nimeishaelekeza wawili na ninafuraha wanaendelea vizuri. Mie ninakibiashara changu kwa miaka 3 sasa ambacho kwakweli kinaweza kunipatia mahitaji ya mwezi au tuseme hand to mouth. Ninapenda kutanuka na pia kuinvest tatizo nikifanya hivo ninakula mtaji na inabidi nitoe kwenye salary. Mwenzangu ananiambia kuwa sijui biashara nikasomee enterpreneurship! Ninahitaji account ya biashara, nidhamu ya juu kwenye mtaji etc. Hebu tuelekezane juu ya hili.
 
Mimi ni mtunzi wa kitabu cha mbinu za biashara na maarifa ya kupata pesa na utajiri. Pia ni mshauri wa biashara, ninatoa ushauri wa biashara na kuendesha mafunzo ya ujasiriamali, kuandaa michanganuo kuombea mikopo benki na misaada kutoka kwa wafadhili. Mwaka 2009 niliwezesha wateja wangu kupata mikopo ya Tshs. milioni 300 toka mabenki mbali mbali, niliendesha mafunzo na kutoa ushauri kwa watu mbali mbali, Kati ya mafunzo ambayo niliyafanya na yakafana ni yale ambayo yaliandaliwa na Mwang'amba Communication na kufanyika Millenium tower, ambapo wawezeshaji tulikuwa mimi( Charles Nazi) James Mwangamba, Eric Shigongo, Martin Kaswahili, Mr Msemwa na Chris Mauki.

Utafiti nilioufanya nimegundua kwamba watu wengi wanakwama kuendesha biashara zao au kupata maendeleo ya kiuchumi kwa sababu ya kukosa maarifa ya ujasiriamali.Kwa hiyo nimeamua kuwa lengo langu ni kutoa elimu ya ujasiriamali kwa watanzania wote. Kutokana na wito wa mwenzetu natoa ofa kwa Wana JF ambao wako Dar kuwa niko tayali kutoa mafunzo ya ujasiriamali bila malipo yoyote. Nauomba uongozi wa JF usaidie kutafuta ukumbi. Kwa mawasiliano zaidi kwa wanaohitaji kupata mafunzo hayo na uongozi wa JF wanaweza kunipigia simu namba 0755394701. Pia kama una kikundi cha watu ambao wanahitaji kupata mafunzo mnaweza kuniita niko tayali kutoa mafunzo bila malipo mradi mniandalie mahali pa kukutana na muwe idadi isiyokuwa chini ya watu 10.

CHARLES NAZI
Mshauri wa biashara na Mtunzi wa kitabu cha Mbinu za biashara
 
Bravo Babalao utatufaa sana jamani. Ngoja tuone kama watapatikana watu, ila hata mie hao 10 naweza watafuta. Ninasubiri wengine wenye nia ntakutafuta lol, asante na ubarikiwe.
 
Mshauri wa biashara na Mtunzi wa kitabu cha Mbinu za biashara

Baba Joe since unaoneka upo kwenye mood za kutoa ushauri wa bure leo, wacha na wengine tuombe msaada wa ushauri kutoka kwako.

Hivi mtu anaweza vipi au atumie mbinu gani kuweza attract investors hapo nyumbani, how does he go about raising cash without giving too much shares au what is the maximum loan a bank can offer.
 
Haya tumeshapewa bure basi tuchangamkie basi nafasi hii. Nikirudi Dar nitakutafuta ili ninyonye machache kt ya mengi uliyo nayo. Asante Baba lao.

Nyongeza yangu ni hii, ujasiriamali kwa sasa ni kuthubutu kushusha vitu toka kichwani na kuviweka ktk vitendo ili kupitia vitendo ie practical unajiongezea ujasiri na hivyo unasogea mbele.

Nilipojitambua nilivyo basi nikathubutu kidogo tu na nimeona matokeo.
 
Mimi ni mtunzi wa kitabu cha mbinu za biashara na maarifa ya kupata pesa na utajiri. Pia ni mshauri wa biashara, ninatoa ushauri wa biashara na kuendesha mafunzo ya ujasiriamali, kuandaa michanganuo kuombea mikopo benki na misaada kutoka kwa wafadhili. Mwaka 2009 niliwezesha wateja wangu kupata mikopo ya Tshs. milioni 300 toka mabenki mbali mbali, niliendesha mafunzo na kutoa ushauri kwa watu mbali mbali, Kati ya mafunzo ambayo niliyafanya na yakafana ni yale ambayo yaliandaliwa na Mwang'amba Communication na kufanyika Millenium tower, ambapo wawezeshaji tulikuwa mimi( Charles Nazi) James Mwangamba, Eric Shigongo, Martin Kaswahili, Mr Msemwa na Chris Mauki.

Utafiti nilioufanya nimegundua kwamba watu wengi wanakwama kuendesha biashara zao au kupata maendeleo ya kiuchumi kwa sababu ya kukosa maarifa ya ujasiriamali.Kwa hiyo nimeamua kuwa lengo langu ni kutoa elimu ya ujasiriamali kwa watanzania wote. Kutokana na wito wa mwenzetu natoa ofa kwa Wana JF ambao wako Dar kuwa niko tayali kutoa mafunzo ya ujasiriamali bila malipo yoyote. Nauomba uongozi wa JF usaidie kutafuta ukumbi. Kwa mawasiliano zaidi kwa wanaohitaji kupata mafunzo hayo na uongozi wa JF wanaweza kunipigia simu namba 0755394701. Pia kama una kikundi cha watu ambao wanahitaji kupata mafunzo mnaweza kuniita niko tayali kutoa mafunzo bila malipo mradi mniandalie mahali pa kukutana na muwe idadi isiyokuwa chini ya watu 10.

CHARLES NAZI
Mshauri wa biashara na Mtunzi wa kitabu cha Mbinu za biashara

Bravo Mkuu!

Salute!

Nasi tusiokuwapo Dar tunaweza kuja kushiriki mafunzo hayo; na kama token of apreciation tukajicomit kwa kuchangia gharama za ukumbi! Binafsi sipo Dar; lakini kama mafunzo niya siku kadhaa mfululizo mie naweza kushiriki na pia hapa nakuja na wazo; organization ya JF inaweza ikaandikia BP hii kitu tukapata wafadhili hata kwa hao would be financiers achilia mbali foundations nyingi tu mlizonazo hapo Dar! Ni wazo tu!

mwito wangu JF leadership mtakuwa mmeanzisha kujenga ile iitwayo corner stone mkiweza kuendesha hii kitu!

Mubarikiwe!
 
Jamani hilii wazoo ni zuri sana na nitamani kuliona linasonga mbele kwa maana ya WALK THE TALK

Tuhamasike na kusonga mbelee kwa utekelezaji.
Nashauri kwa hapa dar tukiorganize tutafute sehemu (zipo kumbi mbali mbali za bei nafuu kama kuna yeyote mwenye connection na ukumbi tafadhali kuwa wa kwanza kutuelezaa tuchangishane tayari mtaalamu yupo aweze kutupa somo?

Jamani INAWEZEKANAA TUSONGE MBELEEE
 
Babalao,

Hongera kwa kazi yako nzuri. Nashauri pia uongee na TBC ili kuwe na kipindi cha Ujasiriamali kila wiki kwa angalau saa mbili kwa wiki kupitia Televisheni na Radio. Kipindi hiki kinaweza kuwa chini ya JF ila wewe ukawa ndiyo mzungumzaji na muelimishaji mkuu.
 
Njia nyingine ya kujifunza ni pamoja na kutembelea kazi za wajasiriamali wenzako,hii inaweza kukutia moyo na ari ya kusonga mbele.
 
Babalao,

Hongera kwa kazi yako nzuri. Nashauri pia uongee na TBC ili kuwe na kipindi cha Ujasiriamali kila wiki kwa angalau saa mbili kwa wiki kupitia Televisheni na Radio. Kipindi hiki kinaweza kuwa chini ya JF ila wewe ukawa ndiyo mzungumzaji na muelimishaji mkuu.


Walau tupate tija kwenye hii nyenzo muhimu ya Taifa letu! senksi sana Tanuru
 
wakuu hapa mie nina dokezo la msingi kabsaaa..katika watu 100 wanaoongelea ujasiriamali 99 ni wafanya biashara na 1 ndio mjasiria mali...sasa lazma tujue kuna tofauti ya wafanyabiashara na wajasiriamali.....

Anayenunua nyanya kariakoo tsh. 100 na kuja kupanga gengeni kwake manzese na kuuza tsh. 120..huyu ni mfanya biashara...sawa na wanaokwenda china/dubai/honkong/thailand....MJASIRIAMALI..huyu anatakiwa awe na jicho la ziada la kuona nafasi/fursa zaidi za kutengeneza pesa..na sio kununua na kuuza tuu...say..mjasiriamali atanunua nyanya kariakoo..atazi-preserve zizioze..kisha atazipack vizuri na kuzitia logo yake kisha ataziuza kempinski..na nyingine atasafirisha kwenda nje ya nchi...zilizoanza kuoza pale kariakoo..mjasiriamali atazinunua na kuzitengeneza sauces mbalimbali na kuuza..

ANAKUWA ANA-ADD VALUE before selling..na kwa kuadd value anauza/anapata value for money...ni maoni tuu wadau
 
wakuu hapa mie nina dokezo la msingi kabsaaa..katika watu 100 wanaoongelea ujasiriamali 99 ni wafanya biashara na 1 ndio mjasiria mali...sasa lazma tujue kuna tofauti ya wafanyabiashara na wajasiriamali.....

Anayenunua nyanya kariakoo tsh. 100 na kuja kupanga gengeni kwake manzese na kuuza tsh. 120..huyu ni mfanya biashara...sawa na wanaokwenda china/dubai/honkong/thailand....MJASIRIAMALI..huyu anatakiwa awe na jicho la ziada la kuona nafasi/fursa zaidi za kutengeneza pesa..na sio kununua na kuuza tuu...say..mjasiriamali atanunua nyanya kariakoo..atazi-preserve zizioze..kisha atazipack vizuri na kuzitia logo yake kisha ataziuza kempinski..na nyingine atasafirisha kwenda nje ya nchi...zilizoanza kuoza pale kariakoo..mjasiriamali atazinunua na kuzitengeneza sauces mbalimbali na kuuza..

ANAKUWA ANA-ADD VALUE before selling..na kwa kuadd value anauza/anapata value for money...ni maoni tuu wadau

Well thought,nicely said.
 
..MJASIRIAMALI..huyu anatakiwa awe na jicho la ziada la kuona nafasi/fursa zaidi za kutengeneza pesa..na sio kununua na kuuza tuu...say..mjasiriamali atanunua nyanya kariakoo..atazi-preserve zizioze..kisha atazipack vizuri na kuzitia logo yake kisha ataziuza kempinski..na nyingine atasafirisha kwenda nje ya nchi...zilizoanza kuoza pale kariakoo..mjasiriamali atazinunua na kuzitengeneza sauces mbalimbali na kuuza..

ANAKUWA ANA-ADD VALUE before selling..na kwa kuadd value anauza/anapata value for money...ni maoni tuu wadau

Kwa mapoint ka aya; nashauri ubadili jina kwenda I care tih tih tih tih
 
Kwa mapoint ka aya; nashauri ubadili jina kwenda I care tih tih tih tih


kakaaa...sio kivilee kuwa i dont care...sema mambo kama haya ya ujasiriamali yanahitaji kuujua undani wa mafanikio ya wengine kisha uone tofauti ya wasiofanikiwa...ndio maana wafanyabiashara wengi wanaanguka ila wajasiriamali wanaendelea kuishi...UJASIRIAMALI...unahitaji extra senses...creativity in business....an inborn touch of doing things in a different But EFFECTIVE WAY....

tunayo safari ndefu ya kwenda kuwa wajasiriamali wa kweli..ila tusikate tamaa..tutafika..if at the start somebody can overcome entrepreneu-phobia..she/he stands a great chance of being one of them.....kwa hiyo issue hapa ni ku-overcome uoga wa kuwa mjasiriamali...then unapitia wakati mgumu wa kukomaa kama mjasiriamali kisha unakuwa...soo easier said than...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom