Tufikiri Upya hulka ya Kukariri Takwimu

Baija Bolobi

JF-Expert Member
Feb 25, 2009
1,093
1,726
Tabia ya Mkuu wetu kupenda watu wakariri takwimu ina pande mbili. Kwa upande wa mambo ya fedha , Mkurugrnzi (DED) kukariri takwimu yaweza kuwa dalili ya yeye kufuatilia mafungu. Wakurugenzi wa namna hii wanajulikana kwa ulaji wa fedha. Huidhinisha fedha na kuzifuata nyuma ili wazitafune. Na katika kukariri huwa wanahakikisha wanakula bila kumaliza na kwa hiyo wanatunza kumbukumbu. Ukiwa mwongo usiwe msahaulifu.

Upande wa pili kutokariri takwimu za fedha ukiwa mkuu wa taasisi, yaweza kuwa dalili ya udhaifu (si uzembe). Kwamba, unategemea mtu mwingine ajue fedha kuliko wewe. Hili si kosa la kumwondoa mtu katika nafasi yake.

Kwa hiyo kutumbuliwa kwa mama yule na baba yule, yawezekana tatizo si kushindwa kukariri. Yawezekana na masuala mengind ukitilia maanani kuwa Mkuu alitamka kuwa amewasamehe.

Nilipoiangalia ile clip kabla ya kutokea barua ya kuwatumbua, nilicomment kuwa "ningelikuwa mimi, ningempandisha cheo yule mama". Nilimwona ana msimamo mzuri na kusimamia anachokijua kuliko kukimbilia kumdanganya Mkuu. Je kuna tofauti gani kati ya Askari aliyemkatalia mke wa waziri fulani barabarani alipotaka kutumia nafasi ya mmewe kutolip faini ya trafic?

Yule mama alim-adress Mkuu wa heshima sana tofauti na kauli ya " huwezi kunijibu hivyo mimi".
 
Yule mama naye ni ujinga wake mwenyewe tu. Kwani yeye hajui serikali iliyopo inahitaji nini? Yeye angetaja fugure yeyote ile kubwa kubwa hata kama ni ya uongo.
Kwani aliyesema Gadaf alikua rais wa kuwait alifanywa nini? Si alishangiliwa tu yakaisha?
 
Yule mama naye ni ujinga wake mwenyewe tu. Kwani yeye hajui serikali iliyopo inahitaji nini? Yeye angetaja fugure yeyote ile kubwa kubwa hata kama ni ya uongo.
Kwani aliyesema Gadaf alikua rais wa kuwait alifanywa nini? Si alishangiliwa tu yakaisha?
Mmmh
 
Sitarajii yule mama angeweza kukumbuka exactly ni shilingi ngapi za barabara alizopokea. Lakini hana ubunifu, na inaelekea IQ yake sio kubwa sana. Hata kama alikuwa hakumbuki kama jumla alizopokea ni bilioni 12 na zilizobaki ni bilioni 2 angesema tu 'tulipokea bilioni 12 kwa ajili ya idara zote. Sina hakika za barabara zilikuwa ni ngapi exactly lakini nafikiri ni bilioni tatu. Na fedha zilizobaki ni bilioni 2. Asingeweza kutumbuliwa angejibu hivyo maana angeonekana wazi anafuatilia mipango yote ya maendeleo wilayani mwake japo hakumbuki kiasi cha kila idara.
 
Kazi ya Mkurugenzi ni pamoja na kujua idadi ya miradi ya maendeleo katika eneo lake. Kujua kiasi cha pesa zilizotolewa kwa ajili ya mradi mmoja katika halmashauri kama ya Bukoba ni jambo ambalo anapaswa kulijua kama sala ya bwana, hata kama anasimamia miradi 10. Naamini kuna figisu na msigano fulani katika halmashauri ya Bukoka.

Rais kuwasimamisha wahusika kwenye mkutano wa hadhara na kuwauliza kiasi kilichotolewa kwenye miradi ya barabara ni kiashiria tosha kuwa kuna kitu hakiendi sawa huko Bukoba mjini, atakuwa aliishapata taarifa fulani kuhusu Bukoba.
 
Ule ni unyanyasaji wa kijinsia baba jesca hana utu kwa akina mama japo anawapenda wajane.....kuna mjane anatafutiwa tobo mahali.
 
Back
Top Bottom