Tufanye nini ili vijana wengi waingie kwenye Ujasiriamali wa Kijamii?

ukhuty

JF-Expert Member
Oct 9, 2016
16,851
41,924
Social Entrepreurship.jpg

Wakuu kuna utafiti nafanya wenye lengo la kufahamu mtizamo wa vijana na nini kifanyike kuhakikisha vijana wengi wanaingia kwenye social entrepreneurship. Nahitaji msaada wa mawazo yenu.
Mjasiriamali wa kijamii ni nani? Huyu ni mtu anayeanzisha biashara kwa kusudi la kutatua matatizo ya kijamii au athari chanya katika mabadiliko ya kijamii.

Zaidi ya vijana milioni 75 duniani wanaelezwa kuwa hawana ajira, vijana milioni 279+ kwenye nchi za kusini mwa jangwa la Sahara wanaelezwa nao kuwa hawana ajira na hakuna mikakati madhubuti iliyowekwa kwaajili ya kuwatengenezea vijana hawa mazingira ya kujiajiri na kuajiriwa kwenye sekta za umma na sekta binafsi.

Je, tufanye nini ili vijana wengi waingie kwenye Ujasiriamali wa Kijamii?
 
Kwa kiasi kikubwa mazinigira yanachangia, tukitengeneza mazingira mazuri ya ujasiriamali vijana wengi watavutika. Hili linajumuisha kuwapa grace period Wajasi kabla ya kutakiwa kutozwa kodi.
 
Kumbe ustadhati ukhuty unakuwaga na sredi makini hivi?


Mara nyingi huwa ninakuona ukijibu sred kwa maneno ya mshangao kama mmmh" au "poa".

Anyway, mada nzuri kuliko zote, ila ninasikitika itapata wachangiaji wachache kuliko zote, au itapata wachangiaji wasiozidi kumi.

Afrika ni bara la giza nene!
 
Takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya vijana katika nchi zinazoendelea kama Tanzania inaendelea kukua kwa kasi sana na hivyo kuongezeka kwa vijana wengi wasio na ajira na wenye hali duni ya maisha, ukosefu wa mitaji, ukosefu wa mbinu jumuishi na kukosa fursa za kiuchumi.
 
View attachment 692004
Wakuu kuna utafiti nafanya wenye lengo la kufahamu mtizamo wa vijana na nini kifanyike kuhakikisha vijana wengi wanaingia kwenye social entrepreneurship. Nahitaji msaada wa mawazo yenu.
Mjasiriamali wa kijamii ni nani? Huyu ni mtu anayeanzisha biashara kwa kusudi la kutatua matatizo ya kijamii au athari chanya katika mabadiliko ya kijamii.

Zaidi ya vijana milioni 75 duniani wanaelezwa kuwa hawana ajira, vijana milioni 279+ kwenye nchi za kusini mwa jangwa la Sahara wanaelezwa nao kuwa hawana ajira na hakuna mikakati madhubuti iliyowekwa kwaajili ya kuwatengenezea vijana hawa mazingira ya kujiajiri na kuajiriwa kwenye sekta za umma na sekta binafsi.

Je, tufanye nini ili vijana wengi waingie kwenye Ujasiriamali wa Kijamii?
Mitaji na uwezeshaji kwa mazingira bora ni muhimu ili kuwavutia vijana ambao wanaweza kuwekeza katika fursa hizi;

* Biashara ya Kilimo na kilimo usindikaji ikiwa ni pamoja na viwanda

* Biashara inayohusu vyombo vya habari, masoko, mawasiliano, michezo, vifaa, sanaa na utamaduni, utalii na burudani.

* Biashara inayogusa mazingira na utunzaji wa mazingira ikiwa ni pamoja na biashara ya kijamii.

* Biashara inayohusu habari na mawasiliano, teknolojia ikiwa ni pamoja na usindikaji biashara
 
Kumbe ustadhati ukhuty unakuwaga na sredi makini hivi?


Mara nyingi huwa ninakuona ukijibu sred kwa maneno ya mshangao kama mmmh" au "poa".

Anyway, mada nzuri kuliko zote, ila ninasikitika itapata wachangiaji wachache kuliko zote, au itapata wachangiaji wasiozidi kumi.

Afrika ni bara la giza nene!

Hahaha mkuu chit chat na mmu tunapunguza stresi.

Naomba madini yako kuhusu hili, tufanye nini ili vijana waingie kwenye Ujasiriamali wa Kijamii?
 
- Mjasiriamali wa kijamii, unamaanisha kuanzisha CBOs, NGO'S, FBOs etc ??
Sifahamu CBO na FBO ni nini.

Mtu yeyote anayeanzisha biashara au mradi kwa lengo la kutatua changamoto za kijamii huitwa Mjasiriamali wa Kijamii "Social Entrepreneur" Mfano, nikianzisha mradi wa kukusanya taka ili kuondokana na takataka maeneo yetu na kuepusha jamii na magonjwa kama Kipindupindu.
 
Sifahamu CBO na FBO ni nini.

Mtu yeyote anayeanzisha biashara au mradi kwa lengo la kutatua changamoto za kijamii huitwa Mjasiriamali wa Kijamii "Social Entrepreneur" Mfano, nikianzisha mradi wa kukusanya taka ili kuondokana na takataka maeneo yetu na kuepusha jamii na magonjwa kama Kipindupindu.
Unataka kumaanisha kuwa kuna wajasiriamali wa aina nyingine pia ukiachana na hao unaowaita " Wajasiriamali wa Kijamii " ?
 
  1. Wazo zuri sana;Kuna mambo mawili ya kufanya kwanza serikali itoe kitu kinaitwa TAX credits kwa watu watakaofanya shughuli ambazo ni positive kwa jamii.Hizi Tax credit mtu anaweza kutumia kuombea Tax waiver pale anapokuwa na profitable venture.
  2. Pili serikali ifanye utambuzi maeneo muhimu yanayohitaji entrepreneurs na kuyapa kipaumbele katika legislation na Taxation ila watu wengi wavutike huko.Nafikiri hili linawezekana kwani sehemu inayoleta shida ni jinsi ammbavyo serikali inakataa kutoa kipaumbelee kwa community centred intiatives na hivyo tunajikuta tunakwama kila tunapojaribu.
 
Unataka kumaanisha kuwa kuna wajasiriamali wa aina nyingine pia ukiachana na hao unaowaita " Wajasiriamali wa Kijamii " ?
Muuza Spea, Muuza Juice, Mama Ntilie wote ni Wajasiamali kuna world changers, strategists nk lakini categorically kuna Trading Entrepreneurs, Manufacturing Entrepreneurs, Agricultural Entrepreneurs na Social Entrepreneurs ambao ninawazungumzia hapa.
 
  1. Wazo zuri sana;Kuna mambo mawili ya kufanya kwanza serikali itoe kitu kinaitwa TAX credits kwa watu watakaofanya shughuli ambazo ni positive kwa jamii.Hizi Tax credit mtu anaweza kutumia kuombea Tax waiver pale anapokuwa na profitable venture.
  2. Pili serikali ifanye utambuzi maeneo muhimu yanayohitaji entrepreneurs na kuyapa kipaumbele katika legislation na Taxation ila watu wengi wavutike huko.Nafikiri hili linawezekana kwani sehemu inayoleta shida ni jinsi ammbavyo serikali inakataa kutoa kipaumbelee kwa community centred intiatives na hivyo tunajikuta tunakwama kila tunapojaribu.

Waooh, asante sana ubongokid
 
[QUOTE="ukh

Tatizo linaanzia katika mfumo wa elimu.

Elimu ni jambo la kwanza kwa umuhimu katika taifa lolote; lakini, inasikitisha kwamba, mitaala ya elimu haikidhi mahitaji ya mazingira, na vile vile elimu inachangia uoga na ajinga kwa kiasi kikubwa.

Vijana wengi sana wanaamini katika kusoma ili waajiriwe, na hawana wazo la kuanzisha biashara zao wenyewe.

Mfano, utakuta mtu ana masters ila kaajiriwa na mtu asiye soma au aliyesoma kidogo. Hapa maana yake ni kwamba, huyu mwajiri hana elimu ila ni jasiri kuliko mwenye elimu ya masters.

Kwa hiyo elimu na mtaala wake kwa ujumla, unaua ubunifu kwa vijana.

Siasa nazo si rafiki kwa vijana.

Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 70+ ya Watanzania wanategemea kilimo.

Lakini cha ajabu ni kwamba, bajeti katika kilimo ni ndogo sana ukilinganisha na sekta nyingine.

Vile vile, mitaala ya elimu haijakipa kilimo kipaumbele cha kutosha.

Masoko ya mazao si rafiki na sera za kupiga marufuku usafirishaji wa mazao nje ya nchi unawaumiza sana wakulima, na inafifisha kilimo biashara.


Mimi binafsi ni mhitimu wa shahada, lakini nimejikita katika ujasiriamali wa kilimo biashara

Ni hayo tu ukhuty
 
Mimi nadhani Serikali inahitaji kubadili/kufanya marekebisho kwenye mfumo wake wa ELIMU ili kupata wajasiriamali(vijana)wazuri zaidi,na pia vijana wenyewe lazima tukubali kubadilika kuendana na mazingira pamoja na kujifunza uelekeo wa technologia na hali ya ukuaji wa uchumi..mambo ni mengi ya kufanya ili kijana/vijana wawe wajasiriamali.
 
[QUOTE="ukh

Tatizo linaanzia katika mfumo wa elimu.

Elimu ni jambo la kwanza kwa umuhimu katika taifa lolote; lakini, inasikitisha kwamba, mitaala ya elimu haikidhi mahitaji ya mazingira, na vile vile elimu inachangia uoga na ajinga kwa kiasi kikubwa.

Vijana wengi sana wanaamini katika kusoma ili waajiriwe, na hawana wazo la kuanzisha biashara zao wenyewe.

Mfano, utakuta mtu ana masters ila kaajiriwa na mtu asiye soma au aliyesoma kidogo. Hapa maana yake ni kwamba, huyu mwajiri hana elimu ila ni jasiri kuliko mwenye elimu ya masters.

Kwa hiyo elimu na mtaala wake kwa ujumla, unaua ubunifu kwa vijana.

Siasa nazo si rafiki kwa vijana.

Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 70+ ya Watanzania wanategemea kilimo.

Lakini cha ajabu ni kwamba, bajeti katika kilimo ni ndogo sana ukilinganisha na sekta nyingine.

Vile vile, mitaala ya elimu haijakipa kilimo kipaumbele cha kutosha.

Masoko ya mazao si rafiki na sera za kupiga marufuku usafirishaji wa mazao nje ya nchi unawaumiza sana wakulima, na inafifisha kilimo biashara.


Mimi binafsi ni mhitimu wa shahada, lakini nimejikita katika ujasiriamali wa kilimo biashara

Ni hayo tu ukhuty
asante sana kaka
 
Mimi nadhani Serikali inahitaji kubadili/kufanya marekebisho kwenye mfumo wake wa ELIMU ili kupata wajasiriamali(vijana)wazuri zaidi,na pia vijana wenyewe lazima tukubali kubadilika kuendana na mazingira pamoja na kujifunza uelekeo wa technologia na hali ya ukuaji wa uchumi..mambo ni mengi ya kufanya ili kijana/vijana wawe wajasiriamali.
shukrani dia kwa mchango wako.
 
Kwa kiasi kikubwa mazinigira yanachangia, tukitengeneza mazingira mazuri ya ujasiriamali vijana wengi watavutika. Hili linajumuisha kuwapa grace period Wajasi kabla ya kutakiwa kutozwa kodi.
Hapo hajazungumzia profit oriented entrepreneurs, amezungumzia Social entrepreneurs.....

Nadhani unatakiwa kujieleimisha juu ya utofauti wa kada hizi mbili my brother!
 
Back
Top Bottom