Tufahamishane mambo kadhaa kuhusu neno Kikokotoo

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,570
19,442
Nilipokuwa shule (ya msingi) tulikuwa tunakumbana na maswali yanayondikwa kwa namna tofauti tofauti, mfano unaweza kuulizwa kuwa "Kokotoa mzingo wa mduara iwapo kipenyo chake ni mita mbili". Lakini vile vile unaweza kuulizwa kuwa "Tafuta mzingo wa mduara iwapo kipenyo chake ni mita mbili." Kuanzia huko nilikuwa najua kuwa "Kukokotoa" maana yake kwa kiingereza ni "Calculate" Utakuta maswali yale yaliyokuwa yakihamishwa kutoka vitabu vya hesabu (hisabati) vilivyokuwa vikitolewa na Oxford University Press kama vile Highway Mathematics Book 8 au Entebbe Mathematics Book 1 na kuwekwa katika lugha ya kiswahili yalikuwa yanatumia sana neno kokotoa. Baada ya miaka hiyo sijawahai kuhanganika tena na neno hilo mpaka hivi majuzi kilipotokea kililo cha Kikokotoo!

Sasa wajuzi wa kiswahili naomba tusaidiane maswali matatu tu: (1) Je ni kweli kuwa neno Kokotoa maana yake ni Calculate? (2) Iwapo imani hiyo ni sahihi, je Kikotoo, kwa vile hiyo ni noun, maana yake ni kile kifaa au kimashini kinachoitwa Calculator?, yaani kikokotoo cha kukokotolea mahesabu mbailmbali (3) Iwapo tafasiri hii ya Calculator ni sahihihi je kumekuwa na matumizi mabaya ya neno Kikokotoo kwenye media siku hizi?

Kwa maoni yangu, malumbano yote yaliyokuwa yakiendelea kuhusu kikokotoo cha mafao yanaonyesha kuwa yalihusu formula ya kukuotolea mafao hayo, yaani kanuni za kukokota mafao au fomyula ya kukokota mafao, siyo kile kimashini kinachotumiwa kukokotoa mahesabu.

Je nina maoni sahihi?
 
Nilipokuwa shule (ya msingi) tulikuwa tunakumbana na maswali yanayondikwa kwa namna tofauti tofauti, mfano unaweza kuulizwa kuwa "Kokotoa mzingo wa mduara iwapo kipenyo chake ni mita mbili". Lakini vile vile unaweza kuulizwa kuwa "Tafuta mzingo wa mduara iwapo kipenyo chake ni mita mbili." Kuanzia huko nilikuwa najua kuwa "Kukokotoa" maana yake kwa kiingereza ni "Calculate" Utakuta maswali yale yaliyokuwa yakihamishwa kutoka vitabu vya hesabu (hisabati) vilivyokuwa vikitolewa na Oxford University Press kama vile Highway Mathematics Book 8 au Entebbe Mathematics Book 1 na kuwekwa katika lugha ya kiswahili yalikuwa yanatumia sana neno kokotoa. Baada ya miaka hiyo sijawahai kuhanganika tena na neno hilo mpaka hivi majuzi kilipotokea kililo cha Kikokotoo!

Sasa wajuzi wa kiswahili naomba tusaidiane maswali matatu tu: (1) Je ni kweli kuwa neno Kokotoa maana yake ni Calculate? (2) Iwapo imani hiyo ni sahihi, je Kikotoo, kwa vile hiyo ni noun, maana yake ni kile kifaa au kimashini kinachoitwa Calculator?, yaani kikokotoo cha kukokotolea mahesabu mbailmbali (3) Iwapo tafasiri hii ya Calculator ni sahihihi je kumekuwa na matumizi mabaya ya neno Kikokotoo kwenye media siku hizi?

Kwa maoni yangu, malumbano yote yaliyokuwa yakiendelea kuhusu kikokotoo cha mafao yanaonyesha kuwa yalihusu formula ya kukuotolea mafao hayo, yaani kanuni za kukokota mafao au fomyula ya kukokota mafao, siyo kile kimashini kinachotumiwa kukokotoa mahesabu.

Je nina maoni sahihi?
Uko sahihi kokotoa maana yake ni calculate. Pili kikotoo ni calculator kama ulivyosema... Lakini katika dhana uliyozungumzia neno kikokotoo limetumika kama kanuni au formula iliyotumika kukokotoa huo mfumo wa hayo mafao na wala hakukuwa na matumizi mabaya ya vyombo vya habari katika kuwasilisha maana ya neno hili. Kwani kumbuka kuwa waandishi na vyombo vya habari hupokea taarifa kutoka idara husika na kuiwasilisha.. BAKITA wenyewe wamethibitisha kuanza kutumia hilo neno katika maana hiyo iliyokusudiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lugha huwa zinabadilika pia. Misamiati huongezeka na mingine huongeza/zwa maana zake.

Waweza kuta leo hii neno fulani lina maana moja lakini miaka michache baadaye neno hilo hilo likawa na maana mbili au hata tatu.
 
Uko sahihi kokotoa maana yake ni calculate. Pili kikotoo ni calculator kama ulivyosema... Lakini katika dhana uliyozungumzia neno kikokotoo limetumika kama kanuni au formula iliyotumika kukokotoa huo mfumo wa hayo mafao na wala hakukuwa na matumizi mabaya ya vyombo vya habari katika kuwasilisha maana ya neno hili. Kwani kumbuka kuwa waandishi na vyombo vya habari hupokea taarifa kutoka idara husika na kuiwasilisha.. BAKITA wenyewe wamethibitisha kuanza kutumia hilo neno katika maana hiyo iliyokusudiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante sana; jibu lako linaonyesha kuwa watu wa NSSF walioanza kutumia neo kikotoo ndio waliosababisha upotofu lugha, halafu BAKITA nayo ikaruhusu upotofu huo uendelee. Kuna ubaya gani kuendelea kutumia kanuni za kukokotoa katika mada hiyo na hivyo kuachana na matumizi potofu ya kikokotoo? Unaposema kikotoo siyo kizuri ni kama vile kutaka calculator nyingine itafutwe yaani achana na TI calulator utafute Casio calculator au kitu kama hicho badala ya kulaumu kanuni iliyoweka na mfuko wenyewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom