Tueleweshane tishio la mchele wa plastic

Mangi flani hivi

JF-Expert Member
Jan 2, 2016
2,026
3,100
Salam,

Waungwana nimeona kuna videos na maandiko mbalimbali yakizunguka katika mitandao mbalimbali ya kijamii kuhusu aina mpya ya mchele iliyoingia sokoni ambayo ni bidhaa inayozalishwa kutokana na plastic. Hapa niwe muwazi zaidi kwamba ninapozungumzia plastic ninamaanisha mifuko almaarufu rambo.

Baadhi ya walaji toka sehemu mbalimbali duniani wameonekana wakifanya majaribio kwa kudundisha kitonge cha wali ambacho kilidunda Kama kitenesi... Badala ya kuchanguka Kama tabia ya wali ilivyo.

Sasa,
Kwa kuangalia mazingira ya kila siku na namna ya utafutaji ya maisha ya mtanzania, Nadhani ninaweza kuwa victim kwenye hili ka mchele wa plastic. Kama sikuwahi kula kwa kutokujua basi nitakula kwa kutokujua siku za usoni.

Msaada,

Je kuna namna ya kitaalamu au ya kienyeji kutambua mchele Kama ni wa plastic au la ukiwa bado upo dukani??? Kwa wajuzi tusaidiane.
 
Sema tu wazi umetoa kwa Mange
Kuna njia kadhaa waweza tumia..
1. Kuloweka kwenye maji.. Mchele wa plastick utaelea juu ya maji
2. Kuunguza.. Mchele wa plastic utanuka plastick wakati wa kuungua
3 kuuacha kwa siku 2- tatu baada ya kupika.. Mchele wa plastic hautashambuliwa na fungus
3. Kuukamua kwa mikono.. Mchele / ubwabwa wa plastic hautang'ang'ania kwenye viganja.
 
Mkuu sitakataa kwamba na Mange amepost, lakini ingia youtube uone... Mimi niliona mwaka Jana hicho kiwanda kwa youtube bt sikujua Kama sisi ni victims.

Kwa kuona kwa mange imenifanya nihoji kwa faida ya Wengi! he kuna njia ya utambuzi???
Ata mimi sikujua kama ushafika huku... Ivi mtu anadanganyikaje na mchele feki? Nchi za wenzetu michele yao haina ladha wala harufu ila kwa michele yetu ya Tanzania utakulaje wali hauna ladha wqla harufu?
Mimi ndo maana sipendi michele ya nje kabisa!!! Mwendo wa mchele wa Mbeya...
 
Ata mimi sikujua kama ushafika huku... Ivi mtu anadanganyikaje na mchele feki? Nchi za wenzetu michele yao haina ladha wala harufu ila kwa michele yetu ya Tanzania utakulaje wali hauna ladha wqla harufu?
Mimi ndo maana sipendi michele ya nje kabisa!!! Mwendo wa mchele wa Mbeya...
kuna watu wananunua hadi vitunguu supermarket mchele ananunua eti umetoka japan unakula mchele wa japan au paktan kwani hapa bongo umeisha? acha waipate
 
Ata mimi sikujua kama ushafika huku... Ivi mtu anadanganyikaje na mchele feki? Nchi za wenzetu michele yao haina ladha wala harufu ila kwa michele yetu ya Tanzania utakulaje wali hauna ladha wqla harufu?
Mimi ndo maana sipendi michele ya nje kabisa!!! Mwendo wa mchele wa Mbeya...
Mkuu kwa hiyo ni harufu tu..... Unajua wachuuzi ni wehu... Watatengeneza perfume ya mchele wa Mbeya ili kukupata.... Hakuna njia ya kitaalamu kukagua Kama huu mchele ni halali??
 
Mkuu kwa hiyo ni harufu tu..... Unajua wachuuzi ni wehu... Watatengeneza perfume ya mchele wa Mbeya ili kukupata.... Hakuna njia ya kitaalamu kukagua Kama huu mchele ni halali??
Jamani, plastiki inatafunika? Michele yetu ukitafuna si hnatafunika?
Mi nashauri hao wanaonunua michele ya nje waache na wanaokula kwa mama ntilie wajaribu kuonja wali kidogo bila mboga...
Kwa mambo kama haya hospitali zitajaa sana aisee
 
Salam,

Waungwana nimeona kuna videos na maandiko mbalimbali yakizunguka katika mitandao mbalimbali ya kijamii kuhusu aina mpya ya mchele iliyoingia sokoni ambayo ni bidhaa inayozalishwa kutokana na plastic. Hapa niwe muwazi zaidi kwamba ninapozungumzia plastic ninamaanisha mifuko almaarufu rambo.

Baadhi ya walaji toka sehemu mbalimbali duniani wameonekana wakifanya majaribio kwa kudundisha kitonge cha wali ambacho kilidunda Kama kitenesi... Badala ya kuchanguka Kama tabia ya wali ilivyo.

Sasa,
Kwa kuangalia mazingira ya kila siku na namna ya utafutaji ya maisha ya mtanzania, Nadhani ninaweza kuwa victim kwenye hili ka mchele wa plastic. Kama sikuwahi kula kwa kutokujua basi nitakula kwa kutokujua siku za usoni.

Msaada,

Je kuna namna ya kitaalamu au ya kienyeji kutambua mchele Kama ni wa plastic au la ukiwa bado upo dukani??? Kwa wajuzi tusaidiane.
 
Ila wacha tule kwa kuwa sisi ni wapumbavu sana.hivi nchi yetu ni yakula vyakul kutoka nje kweli.
 
Ata mimi sikujua kama ushafika huku... Ivi mtu anadanganyikaje na mchele feki? Nchi za wenzetu michele yao haina ladha wala harufu ila kwa michele yetu ya Tanzania utakulaje wali hauna ladha wqla harufu?
Mimi ndo maana sipendi michele ya nje kabisa!!! Mwendo wa mchele wa Mbeya...
ukisema kwenye ladha utachemka coz mapishi yanatofautiana kwa mfano kuna baadhi unachemsha na maji mengi ukiiva unamwaga maji unabaki kawaida/testless na c michele yote ina harufu mingine ni harufu za magunia otherwise uwe mtaalam sana
 
Huku kwetu ndani ndani huo wa Plastiki hautafika. Utaishia mjini kwa wanaopenda vya supermarket na vya nje.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom