BabaDesi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2007
- 6,032
- 3,944
Haya mkuu, we kajitoe mhanga wenzio waje watumbue pilao kwenye msiba wako, halafu maisha yao yanaendelea kama kawa, wewe wa kwako wanabakia yatima ama wanaishia kwa baba wa kambo! Ni hivi ndugu yangu, unapopanga vita yoyote, mtazame adui unayepigana naye, msome vizuri ndipo uandae vifaa na mbinu zitakazokuwezesha kushinda vita, siyo kwenda kufa vitani. Watu hupigana vita washinde, sio wafe, lile suala la kufa vitani huwa ni ajali, lakini mpiganishaji mzuri wa vita akipima akaona vita hii jeshi langu litaangamia, huwa anarudi nyuma, anajipanga vema katika mazingira ya kushinda, siyo kujitoa mhanga, uko hapo? Sasa hawa jamaa wa sijui TUICO na nani vile huko NMB hawajajiandaa hivyo, wamewapelekesha wenzao mzobemzobe, ile inaitwa kwenda "kichwakichwa", sasa subiria kitakachofuata utakumbuka maneno yangu.
Ndio huo woga ninaosema! kila mtu anajifikiria yeye na watoto wake and to hell with wajukuu wa miaka ishirini na tano ijayo!
Mkuu, hata huko vitani naamini kuna wakati majemadari wanaweza kuamua kukitoa muhanga kikosi cha askari 100 iwapo wanaamini kuwa katika kufanya hivyo wataokoa maisha ya askari wengine 1,000?
Tukumbuke pia kuwa kiapo cha askari ni kuapa kuwa tayari kuifia nchi yake na sio kupona kwa ajili ya nchi yake.
Mimi naamini kuwa mgomo utafanyika na wafanyakazi hawa ambao ni ndugu zetu watafanikiwa katika kudai haki yao. lakini pia hata kama hawatafanikiwa kwa asilimia mia moja, watakuwa wamefikisha salamu kwa hawa tunaowaita wawekezaji waanze kusoma maandishi ukutani!!