TUCTA; Kutetea maslahi ya watumishi kwa lugha za leja leja kiasi hiki hakutaleta tija.

Bila bila

JF-Expert Member
Dec 20, 2016
21,278
37,402
Leo Mei 1, 2021 ni siku maalum kwa wafanyakazi duniani kote. Ni siku ya kumbukizi la wafanyakazi kudai maslahi na mazingira bora ya kazi. Ni siku ambayo waasisi wake walikiwasha kweli kweli kuhakikisha wanawasukuma waajiri kuboresha maslahi ya wafanyakazi wa mashambani na viwandani, na kuhakikisha mazingira ya kufanyia kazi yanaboreshwa kwa ajili ya usalama wa wafanyakazi na ufanisi wa kazi. Kama waanzilishi wa vuguvugu hili la kudai haki za wafanyakazi wasingeweka msukumo thabiti kwa waajiri, mpaka Leo wafanyakazi wangekuwa wanachapwa viboko mara tu wanapoinua pua zao kudai haki.
Lakini tofauti na viongozi wa wafanyakazi wa kipindi hicho, Leo tuna viongozi nyoronyoro, viongozi mchelemchele ambao hawajui hata wanasimamia nini. Viongozi wanagombea uongozi wa vyama vya wafanyakazi si kwa lengo la kutetea maslahi ya wafanyakazi, bali kutetea matumbo yao kwa kulipana mishahara/posho zilizonona bila kujali wanaowaongoza wako dhofli khali. Kiongozi mkuu wa wafanyakazi unasimama mbele ya mwajiri mkuu na kusema:-
1.Mheshimiwa ikikupendeza waweza kutuongezea mshahara.
2.Mheshimiwa ukiona inafaa utupandishe madaraja
3.Mheshimiwa kwa vile Jana umechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama tawala kwa kishindo nasi njoo uonyeshe moto kama utaona tunastahili.
4.Mheshimiwa kama hali ya uchumi ni nzuri basi utulipe madeni tunayoidai serikali.
Kwa sitahili hii nakubaliana na wanaosema viongozi wa vyama vya wafanyakazi ni watumwa wa chama tawala cha siasa waliowekwa pale kwa lengo la kuhakikisha maslahi ya chama hicho kimachoongoza serikali hayachahafuliwi.
MODS TAFADHALI, NAOMBA UZI UJITEGEMEE.
 
Taifa linaongozwa na wanafiki secta zote

Tabia ndani ya vinasaba vya watanzania asilimia kubwa. Unafiki imegeuka sifa kuu kwa watanzania karibu wote.

Huu unafiki kuanzia ngazi ya vijiji kupitia bungeni mpaka juu ndio unaliangamiza taifa katika nyanja zote.

Sifa za kijingajinga
Utendaji wa kijingajinga.... unafiki zaidi
Takwim za kijingajinga.......unafiki zaidi
Habari na taarifa za kijingajinga...unafiki zaid
Ahadi za kijingajinga. .... unafiki zaidi

Taifa lipo taabani kwa huu ugonjwa wa unafiki kujipendekeza na uupuzaji katiba, sheria, kanuni na Taratibu.
 
Leo Mei 1, 2021 ni siku maalum kwa wafanyakazi duniani kote. Ni siku ya kumbukizi la wafanyakazi kudai maslahi na mazingira bora ya kazi. Ni siku ambayo waasisi wake walikiwasha kweli kweli kuhakikisha wanawasukuma waajiri kuboresha maslahi ya wafanyakazi wa mashambani na viwandani, na kuhakikisha mazingira ya kufanyia kazi yanaboreshwa kwa ajili ya usalama wa wafanyakazi na ufanisi wa kazi. Kama waanzilishi wa vuguvugu hili la kudai haki za wafanyakazi wasingeweka msukumo thabiti kwa waajiri, mpaka Leo wafanyakazi wangekuwa wanachapwa viboko mara tu wanapoinua pua zao kudai haki.
Lakini tofauti na viongozi wa wafanyakazi wa kipindi hicho, Leo tuna viongozi nyoronyoro, viongozi mchelemchele ambao hawajui hata wanasimamia nini. Viongozi wanagombea uongozi wa vyama vya wafanyakazi si kwa lengo la kutetea maslahi ya wafanyakazi, bali kutetea matumbo yao kwa kulipana mishahara/posho zilizonona bila kujali wanaowaongoza wako dhofli khali. Kiongozi mkuu wa wafanyakazi unasimama mbele ya mwajiri mkuu na kusema:-
1.Mheshimiwa ikikupendeza waweza kutuongezea mshahara.
2.Mheshimiwa ukiona inafaa utupandishe madaraja
3.Mheshimiwa kwa vile Jana umechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama tawala kwa kishindo nasi njoo uonyeshe moto kama utaona tunastahili.
4.Mheshimiwa kama hali ya uchumi ni nzuri basi utulipe madeni tunayoidai serikali.
Kwa sitahili hii nakubaliana na wanaosema viongozi wa vyama vya wafanyakazi ni watumwa wa chama tawala cha siasa waliowekwa pale kwa lengo la kuhakikisha maslahi ya chama hicho kimachoongoza serikali hayachahafuliwi.
MODS TAFADHALI, NAOMBA UZI UJITEGEMEE.
Nakuunga mkono asilimia 100
 
Leo Mei 1, 2021 ni siku maalum kwa wafanyakazi duniani kote. Ni siku ya kumbukizi la wafanyakazi kudai maslahi na mazingira bora ya kazi. Ni siku ambayo waasisi wake walikiwasha kweli kweli kuhakikisha wanawasukuma waajiri kuboresha maslahi ya wafanyakazi wa mashambani na viwandani, na kuhakikisha mazingira ya kufanyia kazi yanaboreshwa kwa ajili ya usalama wa wafanyakazi na ufanisi wa kazi. Kama waanzilishi wa vuguvugu hili la kudai haki za wafanyakazi wasingeweka msukumo thabiti kwa waajiri, mpaka Leo wafanyakazi wangekuwa wanachapwa viboko mara tu wanapoinua pua zao kudai haki.
Lakini tofauti na viongozi wa wafanyakazi wa kipindi hicho, Leo tuna viongozi nyoronyoro, viongozi mchelemchele ambao hawajui hata wanasimamia nini. Viongozi wanagombea uongozi wa vyama vya wafanyakazi si kwa lengo la kutetea maslahi ya wafanyakazi, bali kutetea matumbo yao kwa kulipana mishahara/posho zilizonona bila kujali wanaowaongoza wako dhofli khali. Kiongozi mkuu wa wafanyakazi unasimama mbele ya mwajiri mkuu na kusema:-
1.Mheshimiwa ikikupendeza waweza kutuongezea mshahara.
2.Mheshimiwa ukiona inafaa utupandishe madaraja
3.Mheshimiwa kwa vile Jana umechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama tawala kwa kishindo nasi njoo uonyeshe moto kama utaona tunastahili.
4.Mheshimiwa kama hali ya uchumi ni nzuri basi utulipe madeni tunayoidai serikali.
Kwa sitahili hii nakubaliana na wanaosema viongozi wa vyama vya wafanyakazi ni watumwa wa chama tawala cha siasa waliowekwa pale kwa lengo la kuhakikisha maslahi ya chama hicho kimachoongoza serikali hayachahafuliwi.
MODS TAFADHALI, NAOMBA UZI UJITEGEMEE.
Natamani TUCTA na washirika wake wasome uzi huu.
 
Leo Mei 1, 2021 ni siku maalum kwa wafanyakazi duniani kote. Ni siku ya kumbukizi la wafanyakazi kudai maslahi na mazingira bora ya kazi. Ni siku ambayo waasisi wake walikiwasha kweli kweli kuhakikisha wanawasukuma waajiri kuboresha maslahi ya wafanyakazi wa mashambani na viwandani, na kuhakikisha mazingira ya kufanyia kazi yanaboreshwa kwa ajili ya usalama wa wafanyakazi na ufanisi wa kazi. Kama waanzilishi wa vuguvugu hili la kudai haki za wafanyakazi wasingeweka msukumo thabiti kwa waajiri, mpaka Leo wafanyakazi wangekuwa wanachapwa viboko mara tu wanapoinua pua zao kudai haki.
Lakini tofauti na viongozi wa wafanyakazi wa kipindi hicho, Leo tuna viongozi nyoronyoro, viongozi mchelemchele ambao hawajui hata wanasimamia nini. Viongozi wanagombea uongozi wa vyama vya wafanyakazi si kwa lengo la kutetea maslahi ya wafanyakazi, bali kutetea matumbo yao kwa kulipana mishahara/posho zilizonona bila kujali wanaowaongoza wako dhofli khali. Kiongozi mkuu wa wafanyakazi unasimama mbele ya mwajiri mkuu na kusema:-
1.Mheshimiwa ikikupendeza waweza kutuongezea mshahara.
2.Mheshimiwa ukiona inafaa utupandishe madaraja
3.Mheshimiwa kwa vile Jana umechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama tawala kwa kishindo nasi njoo uonyeshe moto kama utaona tunastahili.
4.Mheshimiwa kama hali ya uchumi ni nzuri basi utulipe madeni tunayoidai serikali.
Kwa sitahili hii nakubaliana na wanaosema viongozi wa vyama vya wafanyakazi ni watumwa wa chama tawala cha siasa waliowekwa pale kwa lengo la kuhakikisha maslahi ya chama hicho kimachoongoza serikali hayachahafuliwi.
MODS TAFADHALI, NAOMBA UZI UJITEGEMEE.
Lile liRais la TUCTA ni kilaza sana sijui lilisoma Mzumbe ya Dar.
 
HV kiongozi wa tuckta Ni Nani Bado Nicolas mgaya


Na mimi nahiitaji kujua hilo aisee!

Na sijawahi kusikia kwenye vyombo vya Habari hao jamaa jinsi wanavyochaguliwa na jinsi uchaguzi unavyofanyika.

Tunahitaji kujua.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom