Tucopy na kupest Katiba ya Kenya

Zero Hours

JF-Expert Member
Apr 1, 2011
12,948
18,648
Hatuhitaji kutumia pesa nyingi eti kutengeneza tume ya katiba ambayo itatumia miaka hata 20 tusipate iyo katiba.

Tufanye kucopy ile ya wakenya tubadili vitu vichache kama muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Kama Kenya imeleta amani na uhuru kwanini ishindikane kwetu?

Kupata katiba mpya bila mapinduzi Tz ni vigumu sana.
 
Hebu tuwekee hapa vifungu 21 muhimu katika Katiba ya Kenya ambavyo haviko kwenye Katiba ya Tz na ambavyo vinahijitaka sana katika Tz ya sasa.
 
Hebu tuwekee hapa vifungu 21 muhimu katika Katiba ya Kenya ambavyo haviko kwenye Katiba ya Tz na ambavyo vinahitaka sana katika Tz ya sasa.
Cha kwanza ni tume huru ya uchaguzi...na mkuu wa tume kuchaguliwa na rais ambaye ni mwenyekiti wa ccm!!
 
Katiba ya Kenya inaendana na mahitaji yao kwa wakati huo. Haitatufaa.
 
ha ha ha! unaweza ukakopi na kupaste lkn utekelezaji 0! vivyohivyo unaweza kuunda katiba imara lkn utekelezaji holla nafikiri tuanze na misingi ya utekelezwaji wa katiba kwanza here we can work good.
 
Tanzania na Kenya ni vitu viwili tofauti sana.
1. Tanzania ni nchi ya muungano Kenya sio
2. Asili ya Tanzania ni ujamaa kenya ubepari
3. Kenya kuna ukabira Tanzania hakuna.
4. Mahitaji ya kenya na Tanzania ni tofauti.

Katiba ya kenya inaendekeza rushwa kwamba rais hana uwezo wa kuwaondosha wala rushwa kwenye utawala wake.

Ukigundua na kuelewa kuwa ni nchi tofauti zenye Ideologies tofauti. Hautaleta tena hiki humu.
 
ha ha ha! unaweza ukakopi na kupaste lkn utekelezaji 0! vivyohivyo unaweza kuunda katiba imara lkn utekelezaji holla nafikiri tuanze na misingi ya utekelezwaji wa katiba kwanza here we can work good.
Katiba kwanza ndyo utekelezaji unafata.
 
Bado kasumba ya kuona kila cha Kenya ni bora kuliko cha Tz inawaandama waTz. Leo Kenya kuna Amani na uhuru kuliko Tz.!?
 
Tanzania na Kenya ni vitu viwili tofauti sana.
1. Tanzania ni nchi ya muungano Kenya sio
2. Asili ya Tanzania ni ujamaa kenya ubepari
3. Kenya kuna ukabira Tanzania hakuna.
4. Mahitaji ya kenya na Tanzania ni tofauti.

Katiba ya kenya inaendekeza rushwa kwamba rais hana uwezo wa kuwaondosha wala rushwa kwenye utawala wake.

Ukigundua na kuelewa kuwa ni nchi tofauti zenye Ideologies tofauti. Hautaleta tena hiki humu.
Acha porojo
 
Kenya hakuna uhuru wa habari kama TZ kama unavyosema mkuu. Wewe fuatilia mitandao ya kijamii ya kenya ndio utaelewa. Wapo na limitation ya kujieleza.
 
hakuna utekelezaji bila ya uzalendo je tunawazalendo wa kuitekeleza hiyo katiba..?
kumbuka nguvu ya maneno/wazo ipo katika vitendo!
Ubovu wa katiba ndyo sababu ya kuua uzalendo. Katiba ingekuwa inawajibisha viongozi kuanzia ngazi ya juu hadi chini. Wasingekuwa wagumu kuwa wazalendo. Ndyo maana unaona Raisi wa Tz anafanya atakavyo sababu katiba iliyopo haimuwajibishi kwa lolote.
 
Kenya hakuna uhuru wa habari kama TZ kama unavyosema mkuu. Wewe fuatilia mitandao ya kijamii ya kenya ndio utaelewa. Wapo na limitation ya kujieleza.
Ukisema kenya haina uhuru wa habari je sisi uku tz tusemeje?

Kenya bunge live- tz bunge dead.
 
Acha porojo
Sasa wewe unaanzisha thread huku hujui chochote unasikitisha sana. Eti kwa sababu jirani anatumia kila siku Panadol na wewe ufanye hivyo eti kwa sababu unataka uwe na afya. Je unajua kwanini anatumia Panadol?

Toa sababu za maana na zinazoendana na mazingira yetu. Halafu fanya research uilete hapa je katiba hiyo imesaidia nini? Je imejibu mambo ya kisisa tu? Vipi mambo ya kiulinzi, vipi mambo ya kijamii vipi mambo ya muungano vipi mambo ya kiuchumi. Katiba sio siasa pekee.
 
Ukisema kenya haina uhuru wa habari je sisi uku tz tusemeje?

Kenya bunge live- tz bunge dead.
Wewe uhuru umadhani ni bunge pekee. Nimekueleza ulinganishe mitandao ya kijamii ya kenya na tanzania. Hebu nenda kwenye mitandao yao kama utapata uhuru huo. Wakikuyu wameteka mitandao yote na hakuna uhuru wa kujieleza. Fikiria kwa jicho la ndani zaidi.
 
Hatuhitaji kutumia pesa nyingi eti kutengeneza tume ya katiba ambayo itatumia miaka hata 20 tusipate iyo katiba.

Tufanye kucopy ile ya wakenya tubadili vitu vichache kama muungano wa Tanganyika na zanzibar.

Kama kenya imeleta amani na uhuru kwanini ishindikane kwetu?

Kupata katiba mpya bila mapinduzi Tz ni vigumu sana.
Ilisemwa sana lakini JK na timu yake ya CCM wakapuuza. Jk naye hafai, usione watu wanalinganisha na kitu kingine, naye hafai. May be angelifanya wajibu wake kikamilifu tungelikuwa na nafasi nzuri ya utawala bora
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom