Tuchangiane uzoefu katika malezi: Malezi yako yalikuwaje, unahisi yamekuathiri, ungependa kulea watoto wako kama ulivyolelewa?

Blue G

JF-Expert Member
Jun 20, 2012
5,335
3,652
Habarini Wadau wa MMU, suala la malezi ni changamoto sikuzote,kulea watoto halijawahi kuwa rahisi hata mara moja

tena wanasema mtoto umleavyo ndivyo akuavyo,kwamba utu au tabia za mtoto wako ni matunda ya malezi yako,kama ni ukatili,upendo,huruma,uchapa kazi au uvivu vyote ni matokeo ya malezi yako(japo kuna wengine ambao licha ya jitihada nyingi ambazo mzazi hutumia bado huishia kuwa watu wa ajabu katika jamii)

Mfano kuna mahali nilisoma japo nimesahau chanzo ila nakumbuka nilisoma kuwa watoto ambao hawakuwa wakikumbatiwa mara nyingi wakiwa wachanga wanakabili ugumu wa kuonesha upendo pindi wakikua

lakini pia kuna baadhi ya watu katika stori za hapa na pale ambao wanakiri labda kumkumbatia mtoto wake,au ile mke au mume kutaka taka ukaribu wa mwili inawawia vigumu maana ni vitu ambavyo ni vigeni kwake hakuvizoea

lakini pia kuna dhana kuwa zamani haikuwa rahisi kabisa kuwa Rafiki na baba,yaani akifika kila mmoja anatafuta pa kwenda ili kulinda heshima ya baba,na hivyo kukuta watoto wakibase upendo wao Zaidi kwa mama kuliko baba

Naombeni tushare experience zetu wadau,kuna ukweli kiasi gani kuhusu swala hilii la malezi?kuna mtu anayedhani malezi ambayo mzazi anampa mtoto wake yanaweza kuathirii utu wake hapo baadae?kuna mtu ambaye anahisi malezi aliyoyapata yameamuathiri kwa namna moja au nyingine?kuna mtu ambaye anahisi hatamani kulea watoto wake kama wao walivyolelewa?

Karibuni wana MMU
 
Njia bora kabisa ya kulea mwanao ni kuangalia wewe ulivyolelewa.
Kila ulichokitaka ukakipata na hakikua cha faida, usimfanyie mwanao.
Kila ulichokotaka ukakikosa na sasa unaona au umejifunza ni cha faida, mfanyie mwanao.

Zaidi kuliko, Mlee mwanao amjue MUNGU; Mungu wa kweli.
 
Njia bora kabisa ya kulea mwanao ni kuangalia wewe ulivyolelewa.
Kila ulichokitaka ukakipata na hakikua cha faida, usimfanyie mwanao.
Kila ulichokotaka ukakikosa na sasa unaona au umejifunza ni cha faida, mfanyie mwanao.

Zaidi kuliko, Mlee mwanao amjue MUNGU; Mungu wa kweli.
umenena vyema sana mkuu Tized hadi nakosa swali

ila still naomba nikuulize

unaamini kuwa mtoto kuwa na upendo,kuwa katili au huruma hutokana na malezi anayoyapata? au ni vinasaba ndivyo vinavyoamua mambo yote hayo?
 
Enhe mada kama hizi ndio zenye tija. ... Ngoja nikae standby niambulie mawili ma3 hapa
Mkuu hearly usipite tu

Tupatie uzoefuu wako pia,labda kutokana na malezi ulioyapitia ua hata Rafiki zako wa karibu au hata unavyolea watoto wako(kama unao) unaonaje malezi yako yanwafanya wanakuwa watu wa namna gani?
 
Mkuu Mimi bwana kwanza bado sijabahatika kupata mtoto/watoto bado sijaamua kupitia hiyo hatua bora ambayo huwa inamfanya kila binaadamu ambaye ana akili timamu mwenye kuwa jibika na majukumu yake/family yake ipaswavyo ajione fahari kuitwa mzazi ""

Nitatoa ushauri ...vuta subira kidogo mkuu
Mkuu hearly usipite tu

tupatie uzoefuu wako pia,labda kutokana na malezi ulioyapitia ua hata Rafiki zako wa karibu au hata unavyolea watoto wako(kama unao) unaonaje malezi yako yanwafanya wanakuwa watu wa namna gani?
 
Mkuu Mimi bwana kwanza bado sijabahatika kupata mtoto/watoto bado sijaamua kupitia hiyo hatua bora ambayo huwa inamfanya kila binaadamu ambaye ana akili timamu mwenye kuwa jibika na majukumu yake/family yake ipaswavyo ajione fahari kuitwa mzazi ""

Nitatoa ushauri ...vuta subira kidogo mkuu
ah okay sawa sawa mkuu
nakutakia kila la kheri pindi utakapoamua kuwa mzazi

sawa mkuu nausubiria ushauri wako na maoni yako hapa hapa
 
Ndio...natamani saana kulea kama nilivolelewa mimi na zaidi (nililelewa vema)

Malezi niliolelewa yamenijenga kua mtu mpole,mcheshi...nisiehukumu watu,na mwelewa na ambaye ninaweza kuishi na kila mtu (mtu wa aina yeyote)
 
Binafsi Naona kuwa Malezi ambayo niliyolelewa yalikuwa ni sahihi kwa asilimia 60 na yalikuwa ni malezi bora kutokana na mazingira ya wakati Ule ambao nilikuwa na lelewa ....... Ijapokuwa Ni malezi ambayo kwa namna fulani haya wezi kukosa kasoro ndogo ndogo kwa sababu walio nilea ni binaadamu wa kawaida na kama ambavyo tunavyojua hakuna binaadamu mkamilifu '' that's why Nina ona kuwa kuna upungufu wa asilimia 40 ya malezi niliyo ya Pata kwa sababu walio nilea ni binaadamu wa kawaida

Hivyo basi mimi Nitapenda kuona endapo nitakuja kupata watoto ni waambukize walau 40% ya malezi ambayo nilipitia hiyo asilimia 60% iliyobaki itakuwa ni Aina ya malezi ya mfumo wangu binafsi ambayo nimejifunza toka Katika jamii inayonizunguka jamii ambayo kwa namna 1 ama nyingine nayo ilifanikiwa kuwa kuza watoto katika maadili chanya malezi ambayo yamechangia kwa kiasi kikubwa kuwa fanya watoto hao kuweza kuwa mifano bora ya kuigwa katika jamii yetu ......

Kwanini nimesema kwamba nitawapatia watoto wangu asilimia 40%tu ya malezi niliyo lelewa !!!?

Ni kwa sababu Mazingira ambayo nilikulia mimi na mazingira ambayo wanayo kutana nayo watoto wa sasa ni vitu viwili tofauti '' Mimi nimekulia katika mazingira ambayo TV ili kuwa ni anasa waweza kukuta mtaa mzima ipo katika nyumba 2 tu ...

.so uchache huu wa kasi ya technology ulikuwa una wapa wazazi wetu wepesi wa kuweza kutu monitor ki-malezi pasipo kupata changamoto kubwa kubwa toka kwa watoto kama ilivyo hivi sasa .... wakati wa malezi yetu ilikuwa mzazi akiwa na mimba hauwezi kusikia mtoto akielewa kuwa mama yake ana mimba bali watoto tulikuwa tuna ambiwa kuwa mama ameshiba na hata pale inapotokea akajifungua salama na kurejea nyumbani na mtoto tulikuwa , tunaongopewa kuwa mama alikwenda kununua mtoto ..

kitu ambacho ni tofauti kabisa na sasa kutokana na kasi ya ukuuaji wa Internet na ongezeko kubwa la watu haswaa wageni mbali mbali toka Katika Mataifa yaliyo endelea kuwa wanakuja nchini na kisha kuleta tamaduni zao ambazo zime kuwa zinasambaa kwa kasi mitaani '' watoto Wamekuwa wanajua mambo mengi sana kwa haraka na kasi kubwa mnooo tofauti na wakati wetu ''iwe kwa kusikia au kuona ....

Hivyo basi nitajitahidi Ku -transform mfumo wa malezi ambao utakuwa unaendana na kasi mabadiliko ya Tabia ya nchi iliyopo sasa ...Bila ya kusahau kuingiza asilimia 40 ya mfumo wa malezi nilioupitia toka kwa walezi wangu""
 
Ndio...natamani saana kulea kama nilivolelewa mimi na zaidi (nililelewa vema)

Malezi niliolelewa yamenijenga kua mtu mpole,mcheshi...nisiehukumu watu,na mwelewa na ambaye ninaweza kuishi na kila mtu (mtu wa aina yeyote)
Safi sana mkuu mwakajingatky hongera kwa kupata malezi bora sana kutoka kwa wazazi wako, na kila lakheri katika kulea watoto wako pia kama ulivyolelewa

Kwa hiyo mkuu kulingana na ushuhuda ulioutoa hapa ni wazi kuwa unaunga mkono kuwa utu wa mtoto unathiriwa sana na malezi anayoyapata kutoka kwa wazazi wake,lakini mkuu nini maoni yako kuhusu hili swala la tabia za kurithi? nafasi yake ni ipi? tuseme kama mtoto ana tabia ya kurithi ya ukatili malezi yanaweza kumfanya akawa na upendo na huruma na kumbadilisha kabisa?hii imekaaje hapo?
 
Binafsi Naona kuwa Malezi ambayo niliyolelewa yalikuwa ni sahihi kwa asilimia 85 na yalikuwa ni malezi bora kutokana na mazingira ya wakati Ule ambao nilikuwa na lelewa ....... Ijapokuwa Ni malezi ambayo kwa namna fulani haya wezi kukosa kasoro ndogo ndogo kwa sababu walio nilea ni

kitu ambacho ni tofauti kabisa na sasa kutokana na kasi ya ukuuaji wa Internet na ongezeko kubwa la watu haswaa wageni mbali mbali toka Katika Mataifa yaliyo endelea kuwa wanakuja nchini na kisha kuleta tamaduni zao ambazo zime kuwa zinasambaa kwa kasi mitaani '' watoto Wamekuwa wanajua mambo mengi sana kwa haraka na kasi kubwa mnooo tofauti na wakati wetu ''iwe kwa kusikia au kuona ....

Hivyo basi nitajitahidi Ku -transform mfumo wa malezi ambao utakuwa unaendana na kasi mabadiliko ya Tabia ya nchi iliyopo sasa ...Bila ya kusahau kuingiza asilimia 40 ya mfumo wa malezi nilioupitia toka kwa walezi wangu""
oh safi sana mkuu asante sana kwa maoni yako makini kabisa

labda nikuulize swali la kizushi tena mkuu kuachilia mbali mambo ya sayansi na teknolojia yalivyo sasa na yalivyokuwa zamani

wewe una utu wa aina gani?kaka,dada zako?

unadhani utu ulionao ni kutokana na malezi uliyoyapata kutoka kwa wazazi wako?au unadhani ndivyo ulivyo tu?
 
Oohh Mimi nina Utu wa kutosha tu siwezi kusema kuwa una fika 100% ..ila kwa mazingira ya hizi nchi zetu za dunia ya 3 nchi ambazo Zina watu ambao (baadhi ) hawapendi kuheshimu utu wa mtu na Wanyama naweza kusema nina Utu wa kujitosheleza na takribani siku zinavyo zidi kusonga mbele huwa na jitahidi kuuboresha ili niweze kuwa na utu zaidi

Mkuu Suala la utu sio kwangu tu' hili lipo Katika family yetu kwa Ujumla ijapo kuwa tunazidiana kwa viwango vya utu ...na hii ni desturi ambayo tumeipata baada ya kupokea malezi Yenye Nafuu ya nidhamu toka kwa wazazi wetu ..ila mimi huwa ni mtu ambaye Nina penda kujiongeza zaidi na kusoma machapisho mbali mbali ambayo Yana changia kuweza kuimarisha Imani yangu ya Utu maradufu ili ni siwezi kukengeuka.

Nimefikia hatua ambayo huwa naona kabisa sio sahihi kumchinja ng'ombe na Wanyama wengine wote wanaoliwa kwa sababu na waonea huruma dhidi ya maumivu wanayo pitia wakati wa kuwachinja huwa najiuliza what if binaadamu tungelikuwa tuna fanyiwa hivi but huwa na jitahidi kuji control ili huruma yangu hiyo isiweze sababisha mkanganyiko katika jamii. ..so waweza kujionea binafsi jinsi ambavyo nilivyo katika Suala Zima linalo husu utu
oh safi sana mkuu asante sana kwa maoni yako makini kabisa

labda nikuulize swali la kizushi tena mkuu kuachilia mbali mambo ya sayansi na teknolojia yalivyo sasa na yalivyokuwa zamani

wewe una utu wa aina gani?kaka,dada zako?

unadhani utu ulionao ni kutokana na malezi uliyoyapata kutoka kwa wazazi wako?au unadhani ndivyo ulivyo tu?
 
Oohh Mimi nina Utu wa kutosha tu siwezi kusema kuwa una fika 100% ..ila kwa mazingira ya hizi nchi zetu za dunia ya 3 nchi ambazo Zina watu ambao (baadhi ) hawapendi kuheshimu utu wa mtu na Wanyama naweza kusema nina Utu wa kujitosheleza na takribani siku zinavyo zidi kusonga mbele huwa na jitahidi kuuboresha ili niweze kuwa na utu zaidi

Mkuu Suala la utu sio kwangu tu' hili lipo Katika family yetu kwa Ujumla ijapo kuwa tunazidiana kwa viwango vya utu ...na hii no desturi ambayo tumeipata baada ya kupokea malezi Yenye Nafuu ya nidhamu toka kwa wazazi wetu ..ila mimi huwa ni mtu ambaye Nina penda kujiongeza zaidi na kusoma machapisho mbali mbali ambayo Yana changia kuweza kuimarisha Imani yangu ya Utu maradufu ili ni siwezi kukengeuka.
asante sana mkuu kwa kushare mambo kuhusiana na we mwenyewe binafsi,nimeeelewa sana na sina swali tena juu yako

lakini unaweza ukawa na mifano labda ya majirani zako au mrafiki zako ambao unahisi malezi yao yamewafanya wakawa hivyo walivyo,labda yamewajenga vizuri sana au yamewaharibu sana

maanake lengo la uzi hasa mkuu ni kujua ikiwa kwa kweli malezi yanajenga au kuubomoa utu wa mtoto au kuna la ziada Zaidi ya malezi
 
Mi yangu matatu tu.
Mtoto asikilizi maneno anaangalia matendo.

Mtoto aambiwi maneno ya kumfunga gerezani km we mpole,kiburi,muoga,mnene,mwembamba,una hasira,mjinga.

Mtoto Ana maamuzi yake yaheshimiwe km sio mabaya.

Mtoto wa kiume alelewe km mwanaume na wa kike kama mwanamke.Mlee mtoto wa kiume km mwanamke akibalehe atakuja kutukana mama ake, pamoja na mapenzi yote ya mama ila kumlea mtoto wa kiume km mtoto wa kike ndo source ya watoto kutukana mama zao siki hizi...why because unampa kinyongo umemfanya lege lege akienda kukutana na wenzake waliobalehe km yeye anakuta wamekaza, wanajiamini,wana ukorofi wa kiume,akirudi kwako unambembeleza bembeleza hata kula wakati haliumwi wala nini ...Akifikia umri fln atataka na yeye awe kiumeume,vita ya kwanza Ni na mama yake sababu kubwa ni wenzake wanamdharau ..kuitwa mtoto wa mama hilo Ni tusi kubwa sana kwa mtoto anaebalehe na hasira zake anaenda kuzimaliza kwa mama ake.

Enzi hizo Mama angu nikisema sina njaa,ananiuliza unaumwa?siumwi basi utakula ukisikia no kumbelezena.Ukipigwa ukija kusema ana kuuliza na nani ukimtaja jina km Ni size yako na yeye anakupiga, umefanya ujinga anakukata jicho hilo mwenyewe unakuwa mpole.Watoto wa kiume wa saivi darasa la 1 mtoto analia kwa kitu cha kijinga halafu hachezei kofi moja takatifu..mtoto analilia remote tena wakiume, mama anambeleza.Enzi zetu unaitwa, unakuja unaulizwa unalia nini?huku umeshikwa mkono kwa nguvu zote,thubutu useme remote ilo kofi utakalopigwa.Mtoto anajua kbs sipaswi kulia kwa vitu vya kijinga, swala la kupiga mswaki na kuoga sitakiwi kubembelezwa.Ukiumwa hadi raha mama ako anavyokupenda.
 
Mi yangu matatu tu.
Mtoto asikilizi maneno anaangalia matendo.
asante sana mkuu ni ngumu

nimependa maelezo yako yaani mpaka raha

ulichokisema ni ukweli mtupu tena usiopingika,kila mtoto alelelewe kulingana na jinsi yake,maana kama usemavyo kumlea mtoto wa kiume kilege lege ni hatari sana mkuu coz unatengeneza kichwa cha familia ambacho kitakuja kukosa maamuzi huko mbeleni na kutawaliwa juu

kwa hiyo ni wazi kuwa unaungo mkono kwamba malezi ya wazazi ndiyo yanayojenga utu au tabia za mtoto

lakini vipi kuhusu nafasi ya tabia za kurithi hapa mkuu?
 
Mi yangu matatu tu.
Mtoto asikilizi maneno anaangalia matendo.

Mtoto aambiwi maneno ya kumfunga gerezani km we mpole,kiburi,muoga,mnene,mwembamba,una hasira,mjinga.

Mtoto Ana maamuzi yake yaheshimiwe km sio mabaya.

Mtoto wa kiume alelewe km mwanaume na wa kike kama mwanamke.Mlee mtoto wa kiume km mwanamke akibalehe atakuja kutukana mama ake, pamoja na mapenzi yote ya mama ila kumlea mtoto wa kiume km mtoto wa kike ndo source ya watoto kutukana mama zao siki hizi...why because unampa kinyongo umemfanya lege lege akienda kukutana na wenzake waliobalehe km yeye anakuta wamekaza, wanajiamini,wana ukorofi wa kiume,akirudi kwako unambembeleza bembeleza hata kula wakati haliumwi wala nini ...Akifikia umri fln atataka na yeye awe kiumeume,vita ya kwanza Ni na mama yake sababu kubwa ni wenzake wanamdharau ..kuitwa mtoto wa mama hilo Ni tusi kubwa sana kwa mtoto anaebalehe na hasira zake anaenda kuzimaliza kwa mama ake.

Enzi hizo Mama angu nikisema sina njaa,ananiuliza unaumwa?siumwi basi utakula ukisikia no kumbelezena.Ukipigwa ukija kusema ana kuuliza na nani ukimtaja jina km Ni size yako na yeye anakupiga, umefanya ujinga anakukata jicho hilo mwenyewe unakuwa mpole.Watoto wa kiume wa saivi darasa la 1 mtoto analia kwa kitu cha kijinga halafu hachezei kofi moja takatifu..mtoto analilia remote tena wakiume, mama anambeleza.Enzi zetu unaitwa, unakuja unaulizwa unalia nini?huku umeshikwa mkono kwa nguvu zote,thubutu useme remote ilo kofi utakalopigwa.Mtoto anajua kbs sipaswi kulia kwa vitu vya kijinga, swala la kupiga mswaki na kuoga sitakiwi kubembelezwa.Ukiumwa hadi raha mama ako anavyokupenda.
na hapo kwenye mateno hapo umenikosaha sana mkuu

kweli kabisa mtoto hufuata nyendo hasa za wazai wake vile wanavyoishi na kutendeana

na ndio maana ni nadra sana kukuta kijana ametoka kwenye familia ya baba mpigaji akawa salama na swala la kupiga mke

au binti katoka kwenye familia mama anamtawala mume akawa salama kutokana na swala hilo

au kukuta mtoto anayetoka kwenye familia mabyo matusi kwao ni kama chai afu atokea akiwa salama akawa ni matusi free ni nadra sana mkuu

umenena vyema sana mkuu

kumbe wazazi hasa wanchopaswa kuhakikisha kwenye malezi yao ni vile wanavyoishi na matendo yao kiujumla
 
Malezi bora yaliyo sheheni ustaarabu na ambayo Yana Zingatia namna ya kuweza kumfanya mtoto aweze kutambua mipaka yake dhidi ya makuzi na Tabia alizonazo Yana saidia mnoo kwa kiasi kikubwa ........

Mimi wakati naingia dar nilikuwa na umri wa miaka 12 ....kwa mara ya kwanza nilikutana na jamii ya watu wenye Tabia ambazo sikuwahi kuziona kabla ...nilikutana na jamii ya watu ambao mtoto mdogo wa miaka 10s anaweza kwenda kucheza/kuzurula mpaka saa 6 usiku kisha ana rudi nyumbani pasipo hata kuulizwa alipo kuwa wala mzazi au Mlezi hash tuki mahali Ambapo mtoto wake alipo kuwa Waweza kuona kuwa aina hiyo ya malezi ya wazazi inavyo weza kuzalisha kizazi Chenye Tabia mbovu na Hasi katika jamii tuliyopo

Ni rahisi mnoo kwa mtoto anayeishi katika mazingira hayo kukutana na wahuni wakamlaghai kwa vitu vidogo na kumlawiti /kumnajisi kisha kwakuwa mzazi hana muda wa kumfuatilia mtoto

mtoto anaweza kurudi nyumbani na kukaa kimya Bila kusema kitu kisha akafurahia ile zawadi iliyompumbaza na kumfanya Aingiliwe kimwili na kesho yake Hujikuta anatamani kwenda kufanyiwa Unyama kama huo ili tu aweze kupata zawadi ....m katika mazingira ya malezi kama hayo hayo Pia ni rahisi jamii hiyo kuweza kuzalisha watoto wa vuta bangi/madawa. Wezi /Majambazi. Makahaba. Mimba za watoto wadogo. Watu wenye desturi mbovu ambao vinywa vyao vimejaa maneno makali na matendo maovu(micharuko) etc

Mimi nimelelewa katika mazingira ambayo mtoto ukinunua nguo kwa pesa yako ambayo chanzo chake haijulikani ni kipi lazima utaadhibiwa vikali kisha utatoa maelezo yanayoeleza mahali Ambapo ulipozipata hizo pesa ...Baada ya kutoka shule tuition. .ruksa kwenda kushiriki michezo lakini kurudi nyumbani mwisho saa 12 kinyume na hapo uwe na sababu maalum/nyeti iliyokupelekea uchelewe kurudi nyumbani '' Hiyo ni baadhi ya mifano michache niliyonayo
asante sana mkuu kwa kushare mambo kuhusiana na we mwenyewe binafsi,nimeeelewa sana na sina swali tena juu yako

lakini unaweza ukawa na mifano labda ya majirani zako au mrafiki zako ambao unahisi malezi yao yamewafanya wakawa hivyo walivyo,labda yamewajenga vizuri sana au yamewaharibu sana

maanake lengo la uzi hasa mkuu ni kujua ikiwa kwa kweli malezi yanajenga au kuubomoa utu wa mtoto au kuna la ziada Zaidi ya malezi
 
Malezi bora yaliyo sheheni ustaarabu na ambayo Yana Zingatia namna ya kuweza kumfanya mtoto aweze kutambua mipaka yake dhidi ya makuzi na Tabia alizonazo Yana saidia mnoo kwa kiasi kikubwa ........

Mimi wakati naingia dar nilikuwa na umri wa miaka 12 ....kwa mara ya kwanza nilikutana na jamii ya watu wenye Tabia ambazo sikuwahi kuziona kabla ...nilikutana na jamii ya watu ambao mtoto mdogo wa miaka 10s anaweza kwenda kucheza/kuzurula mpaka saa 6 usiku kisha ana rudi nyumbani pasipo hata kuulizwa alipo kuwa wala mzazi au Mlezi hash tuki mahali Ambapo mtoto wake alipo kuwa Waweza kuona kuwa aina hiyo ya malezi ya wazazi inavyo weza kuzalisha kizazi Chenye Tabia mbovu na Hasi katika jamii tuliyopo

Ni rahisi mnoo kwa mtoto anayeishi katika mazingira hayo kukutana na wahuni wakamlaghai kwa vitu vidogo na kumlawiti /kumnajisi kisha kwakuwa mzazi hana muda wa kumfuatilia mtoto

mtoto anaweza kurudi nyumbani na kukaa kimya Bila kusema kitu kisha akafurahia ile zawadi iliyompumbaza na kumfanya Aingiliwe kimwili na kesho yake Hujikuta anatamani kwenda kufanyiwa Unyama kama huo ili tu aweze kupata zawadi ....m katika mazingira ya malezi kama hayo hayo Pia ni rahisi jamii hiyo kuweza kuzalisha watoto wa vuta bangi/madawa. Wezi /Majambazi. Makahaba. Mimba za watoto wadogo. Watu wenye desturi mbovu ambao vinywa vyao vimejaa maneno makali na matendo maovu(micharuko) etc

Mimi nimelelewa katika mazingira ambayo mtoto ukinunua nguo kwa pesa yako ambayo chanzo chake haijulikani ni kipi lazima utaadhibiwa vikali kisha utatoa maelezo yanayoeleza mahali Ambapo ulipozipata hizo pesa ...Baada ya kutoka shule tuition. .ruksa kwenda kushiriki michezo lakini kurudi nyumbani mwisho saa 12 kinyume na hapo uwe na sababu maalum/nyeti iliyokupelekea uchelewe kurudi nyumbani '' Hiyo ni baadhi ya mifano michache niliyonayo
too sad mkuu kwa mifano uliyoitoa inasikitisha sana mtoto kutoka kwenye innocent state to uchakaramu state just kwa kuwa tu wazazi wanapuuza kuhusu malezi mazima kwa ujumla kumwekea mtoto wao

Duh Mungu atusimamie katika hili jamani

kweli malezi bora kutoka kwa wazazi ni jambo la msingi sana wapendwa

asante sana pia kwa maelezo yako yakinifu na yenye kufikirsha pamoja na kushare experience ya malezi yako binafsi
 
Asante kwa shukrani mkuu --Tuko pamoja katika ujenzi wa taifa
too sad mkuu kwa mifano uliyoitoa inasikitisha sana mtoto kutoka kwenye innocent state to uchakaramu state just kwa kuwa tu wazazi wanapuuza kuhusu malezi mazima kwa ujumla kumwekea mtoto wao

Duh Mungu atusimamie katika hili jamani

kweli malezi bora kutoka kwa wazazi ni jambo la msingi sana wapendwa

asante sana pia kwa maelezo yako yakinifu na yenye kufikirsha pamoja na kushare experience ya malezi yako binafsi
 
Back
Top Bottom