Uchaguzi 2020 Tuchague watu wa kuleta sheria zisizokataza dhamana kwa watuhumiwa, zimetumika vibaya sana awamu ya tano

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Matumizi ya sheria inayohusu masuala ya uhujumu uchumi yamekuwa mabaya sana awamu ya Tano. Kati ya watu walioteswa na sheria hizi kandamizi ni viongozi wa kisiasa wenye mtizamo chanya dhidi ya wananchi na wafanyabiashara.

Hizi sheria hazijafutwa, bado zipo na zinazidi kutumika vibaya na baadhi ya watumishi wasio waadilifu.

Kipindi hiki Cha uchaguzi watumishi wa Umma wanapaswa kuwawazia wale waliokuwa CCM kindakindaki 2015 lakini leo wanaozea jela bila kesi zao kusikilizwa kwa wakati.

Wafanyabishara mmeona namna mambo yalivyowaendea for five years, msiwaze kuwa Sheria zimefutwa. Unaweza wafadhili wanasiasa leo lakini wakiapishwa ukaenda kuishi jela.

Wakulima na wafugaji mmejionea namna mambo yalivyokwenda, waliotunga hizo sheria ndio hao hao waliopo mtaani leo kuwaomba kura msisite kuwahoji.

Wanasiasa wa vyama vyote, mmeona mlivyopokonywa uhuru wakisema, mlivyolazimishwa kuamini msichoamini, mnao muda wakuamua hatima yenu.

Lazima wapiga kura tutake kuwa na watu watakaoleta Sheria zakusimamia haki, mtu akituhumiwa apewe dhamana kesi isikilizwe ndipo atiwe hatiani. Kumweka mtu ndani bila hata kuwa na chembe ya ushahidi kisa mmechukuliana mke au mme si sahihi hata kidogo.

Tuchague watu watakaotuletea Sheria zinazojali utu wetu. Ukipoteza haki hii leo kwa sababu za ushabiki wa siasa utajuta miaka mitano mbele. Chagua kwa kuingalia familia yako, jamii na Taifa.
 
Kwa mataifa ya Kiafrika iyo sheria haitomfunga mtu yeyote wauaji wenyewe wengi homesles hawana cha kupoteza alafu ukishamruhusu muharifu awe nje lazima ataharibu ushaidi kwa njia ya uchawi tunaona kesi nyingi mashahidi wanakufa. vifo vya ghafla na nakueleza kuwa akitaka hivyo adhabu lazima zipungue La mwisho inawezekana hujawai kufanyiwa uharifu ndio maana unashadadia vitu ambavyo vinaumiza.
 
Chama cha Mbowe, hakina uwezo wa kuwasaidia watanzania. Acheni ulaghai wenu, hatudanganyikiii. Mnataka kulibagaza taifa kwa tamaa zenu, kwa beberu kajiuzeni wenyewe kwa mabeberu wenu. Kura za kishindo kwa JPM.
 
1601280631936.png
 
Hapa ndo pa kugusa kabisa hizi sheria kandamizi za hovyo ndizo zimetumika na mahakimu na waendesha mashtaka kuvuna mabilioni ya watz masikini kwa kuchelewesha kesi zao eti ushahidi haujakamilika kumbe wanataka rushwa Sasa Kama ushahidi haujakamilika mnawakamatia nini watu Kama sio kutengeneza mazingira ya kuwapora pesa zao.

Jiulize why jela masikini ndio wamejaa jibu ni kwamba hawana pesa za kununua Uhuru wao. Thus tunataka Lisu akazibomoe hizi sheria kandamizi zilizowekwa na watawala wasiojiamini wenye uwezo wa kukariri na sio kureasoning. Unamuweka vipi ndani mtu 5 yrs eti ushahidi haujakamilika. Huu Ni uuaji kabisa
 
Chama cha Mbowe, hakina uwezo wa kuwasaidia watanzania. Acheni ulaghai wenu, hatudanganyikiii. Mnataka kulibagaza taifa kwa tamaa zenu, kwa beberu kajiuzeni wenyewe. Watanzania wote wanakwenda na JPM.
Nani arudie kosa Tena, yaani uchague kubomolewa nyumba yako akili matope
 
Back
Top Bottom