Tubadilishe Jina la Jiji la Arusha : Liitwe Serengeti au Kilimanjaro

Kasheshe

JF-Expert Member
Jun 29, 2007
4,694
787
Ndugu Watanzania wenzangu,

Kama Mjuavyo majina ya Miji, Mito,barabara n.k yapo yale ya asili na yale ambayo tumebadilisha kwa aidha kumuenzi kiongozi fulani au sababu nyingine yeyote ikiwa pamoja labda na kugawa mikoa na Kadhalika. Mfano... Pugu Road, leo Inaitwa Nyerere Road, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam (DIA) leo Unaitwa Julius Nyerere Inter. Airport (JNIA) Mabadiliko mengi yaliyofanyika ya majina kabla ya leo hii ni kwa sababu za Kisiasa na Kijamii...

Leo hii nakuja na hoja ya Kubadilisha Jina la Jiji la Arusha kwa nia ya Kibiashara au Kiuchumi. Na napendekeza majina haya mawili... aidha jiji lile liitwe Kilimanjaro au liitwe Serengeti.

Nitazungumzia Jina la Kwanza zaidi yaani Kilimanjaro kwa kuwa jina la pili ni kwa ajili ya fall back plan tu!!!

Sababu ya kusababisha kuomba watanzania waridhie mabadiliko hayo ambayo najua yako chini ya TAMISEMI, Mhe. Rais Mwenyewe, Wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro na Arusha, pamoja na Wananchi wote wa Tanzania kwa Ujumla ni hizi zifuatazo:-

A. Kwa kuwa Watani wetu hawapendi kwa makusudi kabisa kusema Mlima Kilimanjaro uko Tanzania!!! (pam9oja na kwamba hawasemi uko Kenya).

B. Kwa kwa Mji wa Arusha ni Makao makuu ya Afrika Mashariki.

C. Kwa kuwa mikutano mingi ya Kikanda na Kimataifa itafanyika kwenye jiji la Arusha

D. Kwa kuwa ujenzi wa Nyumba umefanya sasa Mji wa Moshi na Jiji la Arusha kuunguna kabisa na hata usitambue mipaka kwa urahisi.

E. Kwa kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro pia uko katikati ya Mkoa wa Kilimanjaro na Jiji la Arusha.

F. Kwa kuwa tuna mji wa Moshi mpaka sasa na Hatuna mji unaitwa Kilimanjaro.

G. Kwa kuwa Jina la Arusha halina manufaa yoyote ya Kiuchumi zaidi ya kwamba ni jina la kuridhi tu, kwa maana halitangazi Mbuga ya Manyara, Serengeti, Ngororo au Mlima Kilimanjaro etc.

Napendekeza mipaka ya Mkoa wa Kilimanjaro na Mkoa wa Arusha iangaliwe upya ili, Mji wa Moshi na Halimashauri ya Jiji la Arusha... iwe jiji moja kwa Jina la "Kilamanjaro" Kwa maana pale city centre Arusha na Moshi paitwe Kilimanjaro City. Wilaya za Moshi vijijini, Rombo, Mwanga, Same etc... zawezapewa jina lingine na kuwa mkoa mwingine... Na wilaya za Meru...Serengeti etc.. Zawezapewa Jina lingine.... na kituo cha Mikutano cha Arusha kitaitwa Kilimanjaro International Conference Centre.. KICC... sorry naona inaanza kufanana na Kenyatta inter. conference centre... lakini inaeleweka..

Kwanini Basi napendekeza Hivyo.


Kwa kubadili Jiji la Arusha kuitwa,, Jina Kilimanjaro litatajwa sana duniana, na hivyo kufanya dunia kukumbushwa kwamba Kilimanjaro iko Tanzania. Hivyo kukuza Utalii wetu na Kuleta mapesa kibao.

Wale watakaopinga nawakumbusha jambo moja hivi ukiwa Ulaya/Amerika ukisema naenda Unguja au Pemba utaeleweka... lakini je Ukisema Unaenda Zanzibar?

Hivi ukiwa Ulaya ukisema naenda Moshi, Arusha unaelewaka haraka... Je ukisema Naenda Kilimanjaro... iko tofauti...

Haya wadau jadilini...

Kumbukeni Wenzetu South Afrika wanabadilisha majina ya miji yao... lakini wao ni kwa ajili ya kukumbusha historia... kwa hiyo uwanja wa Johannesbur Inter. Airport sasa ni Oliver Tambo Intertional Airport etc...

NB: Kama mtakataa kuliita Kilimanjaro basi liiteni basi Serengeti kuliko sasa ambapo jina hili(Arusha) halina mvuto wowote wa Kibiasha/Kitalii/Kiuchumi
 
Ndugu Watanzania wenzangu,

Kama Mjuavyo majina ya Miji, Mito,barabara n.k yapo yale ya asili na yale ambayo tumebadilisha kwa aidha kumuenzi kiongozi fulani au sababu nyingine yeyote ikiwa pamoja labda na kugawa mikoa na Kadhalika. Mfano... Pugu Road, leo Inaitwa Nyerere Road, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam (DIA) leo Unaitwa Julius Nyerere Inter. Airport (JNIA) Mabadiliko mengi yaliyofanyika ya majina kabla ya leo hii ni kwa sababu za Kisiasa na Kijamii...

Leo hii nakuja na hoja ya Kubadilisha Jina la Jiji la Arusha kwa nia ya Kibiashara au Kiuchumi. Na napendekeza majina haya mawili... aidha jiji lile liitwe Kilimanjaro au liitwe Serengeti.

Nitazungumzia Jina la Kwanza zaidi yaani Kilimanjaro kwa kuwa jina la pili ni kwa ajili ya fall back plan tu!!!

Sababu ya kusababisha kuomba watanzania waridhie mabadiliko hayo ambayo najua yako chini ya TAMISEMI, Mhe. Rais Mwenyewe, Wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro na Arusha, pamoja na Wananchi wote wa Tanzania kwa Ujumla ni hizi zifuatazo:-

A. Kwa kuwa Watani wetu hawapendi kwa makusudi kabisa kusema Mlima Kilimanjaro uko Tanzania!!! (pamoja na kwamba hawasemi uko Kenya).

B. Kwa kwa Mji wa Arusha ni Makao makuu ya Afrika Mashariki.

C. Kwa kuwa mikutano mingi ya Kikanda na Kimataifa itafanyika kwenye jiji la Arusha

D. Kwa kuwa ujenzi wa Nyumba umefanya sasa Mji wa Moshi na Jiji la Arusha kuunguna kabisa na hata usitambue mipaka kwa urahisi.

E. Kwa kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro pia uko katikati ya Mkoa wa Kilimanjaro na Jiji la Arusha.

F. Kwa kuwa tuna mji wa Moshi mpaka sasa na Hatuna mji unaitwa Kilimanjaro.

G. Kwa kuwa Jina la Arusha halina manufaa yoyote ya Kiuchumi zaidi ya kwamba ni jina la kuridhi tu, kwa maana halitangazi Mbuga ya Manyara, Serengeti, Ngororo au Mlima Kilimanjaro etc.

Napendekeza mipaka ya Mkoa wa Kilimanjaro na Mkoa wa Arusha iangaliwe upya ili, Mji wa Moshi na Halimashauri ya Jiji la Arusha... iwe jiji moja kwa Jina la "Kilamanjaro" Kwa maana pale city centre Arusha na Moshi paitwe Kilimanjaro City. Wilaya za Moshi vijijini, Rombo, Mwanga, Same etc... zawezapewa jina lingine na kuwa mkoa mwingine... Na wilaya za Meru...Serengeti etc.. Zawezapewa Jina lingine.... na kituo cha Mikutano cha Arusha kitaitwa Kilimanjaro International Conference Centre.. KICC... sorry naona inaanza kufanana na Kenyatta inter. conference centre... lakini inaeleweka..

Kwanini Basi napendekeza Hivyo.


Kwa kubadili Jiji la Arusha kuitwa,, Jina Kilimanjaro litatajwa sana duniana, na hivyo kufanya dunia kukumbushwa kwamba Kilimanjaro iko Tanzania. Hivyo kukuza Utalii wetu na Kuleta mapesa kibao.

Wale watakaopinga nawakumbusha jambo moja hivi ukiwa Ulaya/Amerika ukisema naenda Unguja au Pemba utaeleweka... lakini je Ukisema Unaenda Zanzibar?

Hivi ukiwa Ulaya ukisema naenda Moshi, Arusha unaelewaka haraka... Je ukisema Naenda Kilimanjaro... iko tofauti...

Haya wadau jadilini...

Kumbukeni Wenzetu South Afrika wanabadilisha majina ya miji yao... lakini wao ni kwa ajili ya kukumbusha historia... kwa hiyo uwanja wa Johannesbur Inter. Airport sasa ni Oliver Tambo Intertional Airport etc...

Naunga mkono uliyosema ! Nadhani ni jambo zuri na linapaswa kuangaliwa ! Naunga Mkono jina la huo mkoa ubadirishwe, tunaweza kugain mengi tu !
 
Kwa hiyo labda tubadili jina la Tanzania liwe Kilimanjaro, au Serengeti. Badala ya kusema ninakwenda Tanzania, unasema ninakwenda Kilimanjaro au Serengeti.

Lakini mbona sehemu kama 'Acalpulco' zinajulikana vizuri tu huku zikiwa Mexico?

Ni jambo la kunadi na kuuza tu hivyo vivutio ndio kazi inayohitajika bila lazima ya kubadili jina. Arusha, pamoja na kutojua chanzo cha jina hilo, ni jina zuri tu. Libakie hivyo hivyo.
 
kalamu,
akapuko na meksiko achana nako bana kwa sasa, wengi duniani hata hiyo tanzania hawaifahamu, sema kilimanjaro wao wanakwambia kenya, sasa na points zote zilizotajwa na mtoa hoja, nashauri "mkoa" wa arusha na si nchi iitwe either of the proposed names !

manufaa mengi zaidi ya hasara IMO !
 
Cosmetics,

Tell us something that we don't know.Like how to increase tourists, preserve the famous equatorial snowcap, provide housing or deal with crime in Arusha.

Tunapenda sana soap operas lakini kuangalia central issues tunagwaya.
 
Mbona Jina la kilimanjaro tayari lipo? Kwa sababu mlima kilimanjaro uko katika mkoa wa kilimanjaro haitafaa ARUSHA kuitwa kilimanjaro haiwezekani.

Jina la pili, SERENGETI. Serengeti ni Wilaya ambayo iko mkoa wa MARA, sasa iweje arusha iitwe Serengeti?

Kwa jinsi majina yalivyo kaa sioni kama ni Tatizo. Tatizo ni mikakati ya Tanzania katika kukuza biashara ya Utalii.

Kinacho takiwa ni mikakati madhubuti kutangaza utalii na miundombinu imara ya kuwezesha utalii.

Pamoja na jitihada madhubuti za kutangaza utalii, juhudi inabidi iongezwe.

Kukosekana kwa ndege za moja kwa moja (direct flights) mfano kutoka Marekani hadi DAR na sehemu nyingine muhimu ni swala ambalo linakwamisha biashara ya utalii kwa kiwango cha juu. Sasa hivi tuna direct flight kutoka London tu. Watalii watafika vipi.
 
Labda jiji la Arusha tuliite Ngurudoto au Lowassa! (just kidding!)

Pengine ingefaa nchi ikaitwa Kilimanjaro basi kama Kenya inavyoitwa hivyo kwa sababu ya mlima Kenya. Au kama suala ni mlima, basi huo mlima Kilimanjaro uitwe Mlima Tanzania! Hii nadhani ni rahisi kufanya kuliko kubadilisha jina la mkoa au la nchi. Kwa hiyo inakuwa mlima Tanzania uko mkoani Kilimanjaro!

Still confusing though! Nadhani jambo bora sana la kufanya ni kufanya publicity ya kutosha tu, hatuhitaji kubadilisha jina la chochote, litaleta usumbufu sana! Kama hayo majina yaliyokuwepo kwa miaka zaidi ya 100 bado tumeshindwa kuyatangaza vya kutosha, hayo majina mapya bado yatatuchukua muda mrefu kufahamika! Na wakati sisi tunaendelea na longolongo za majina, wenzetu wataendelea kukamua bingo kwa vivutio vyetu kwa kutumia majina yaleyale ambayo sisi tutadai ni "ya zamani!"
 
Hata tukibadilisha majina kiasi gani kama mismanagement inaendelea tusitegemee lolote lile. Arusha ni sehemu iliyobarikiwa na mengi, tukiwa serious na kuiendeleza Arusha kwa miaka mitano tu, inaweza kuwa sehmu nzuri sana na chanzo kizuri sana kwa mapato ya taifa. Lakini sasa tunachoona ni mismanagement. Mabadiliko ya jina itakuwa ni chupa mpya mvinyo uleule.!
 
Ndugu Watanzania wenzangu,

Kama Mjuavyo majina ya Miji, Mito,barabara n.k yapo yale ya asili na yale ambayo tumebadilisha kwa aidha kumuenzi kiongozi fulani au sababu nyingine yeyote ikiwa pamoja labda na kugawa mikoa na Kadhalika. Mfano... Pugu Road, leo Inaitwa Nyerere Road, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam (DIA) leo Unaitwa Julius Nyerere Inter. Airport (JNIA) Mabadiliko mengi yaliyofanyika ya majina kabla ya leo hii ni kwa sababu za Kisiasa na Kijamii...

Leo hii nakuja na hoja ya Kubadilisha Jina la Jiji la Arusha kwa nia ya Kibiashara au Kiuchumi. Na napendekeza majina haya mawili... aidha jiji lile liitwe Kilimanjaro au liitwe Serengeti.

Nitazungumzia Jina la Kwanza zaidi yaani Kilimanjaro kwa kuwa jina la pili ni kwa ajili ya fall back plan tu!!!

Sababu ya kusababisha kuomba watanzania waridhie mabadiliko hayo ambayo najua yako chini ya TAMISEMI, Mhe. Rais Mwenyewe, Wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro na Arusha, pamoja na Wananchi wote wa Tanzania kwa Ujumla ni hizi zifuatazo:-

A. Kwa kuwa Watani wetu hawapendi kwa makusudi kabisa kusema Mlima Kilimanjaro uko Tanzania!!! (pam9oja na kwamba hawasemi uko Kenya).

B. Kwa kwa Mji wa Arusha ni Makao makuu ya Afrika Mashariki.

C. Kwa kuwa mikutano mingi ya Kikanda na Kimataifa itafanyika kwenye jiji la Arusha

D. Kwa kuwa ujenzi wa Nyumba umefanya sasa Mji wa Moshi na Jiji la Arusha kuunguna kabisa na hata usitambue mipaka kwa urahisi.

E. Kwa kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro pia uko katikati ya Mkoa wa Kilimanjaro na Jiji la Arusha.

F. Kwa kuwa tuna mji wa Moshi mpaka sasa na Hatuna mji unaitwa Kilimanjaro.

G. Kwa kuwa Jina la Arusha halina manufaa yoyote ya Kiuchumi zaidi ya kwamba ni jina la kuridhi tu, kwa maana halitangazi Mbuga ya Manyara, Serengeti, Ngororo au Mlima Kilimanjaro etc.

Napendekeza mipaka ya Mkoa wa Kilimanjaro na Mkoa wa Arusha iangaliwe upya ili, Mji wa Moshi na Halimashauri ya Jiji la Arusha... iwe jiji moja kwa Jina la "Kilamanjaro" Kwa maana pale city centre Arusha na Moshi paitwe Kilimanjaro City. Wilaya za Moshi vijijini, Rombo, Mwanga, Same etc... zawezapewa jina lingine na kuwa mkoa mwingine... Na wilaya za Meru...Serengeti etc.. Zawezapewa Jina lingine.... na kituo cha Mikutano cha Arusha kitaitwa Kilimanjaro International Conference Centre.. KICC... sorry naona inaanza kufanana na Kenyatta inter. conference centre... lakini inaeleweka..

Kwanini Basi napendekeza Hivyo.


Kwa kubadili Jiji la Arusha kuitwa,, Jina Kilimanjaro litatajwa sana duniana, na hivyo kufanya dunia kukumbushwa kwamba Kilimanjaro iko Tanzania. Hivyo kukuza Utalii wetu na Kuleta mapesa kibao.

Wale watakaopinga nawakumbusha jambo moja hivi ukiwa Ulaya/Amerika ukisema naenda Unguja au Pemba utaeleweka... lakini je Ukisema Unaenda Zanzibar?

Hivi ukiwa Ulaya ukisema naenda Moshi, Arusha unaelewaka haraka... Je ukisema Naenda Kilimanjaro... iko tofauti...

Haya wadau jadilini...

Kumbukeni Wenzetu South Afrika wanabadilisha majina ya miji yao... lakini wao ni kwa ajili ya kukumbusha historia... kwa hiyo uwanja wa Johannesbur Inter. Airport sasa ni Oliver Tambo Intertional Airport etc...

NB: Kama mtakataa kuliita Kilimanjaro basi liiteni basi Serengeti kuliko sasa ambapo jina hili(Arusha) halina mvuto wowote wa Kibiasha/Kitalii/Kiuchumi

[media]http://www.youtube.com/watch?v=No7jdP2A0N0[/media]
 
Kwa hiyo labda tubadili jina la Tanzania liwe Kilimanjaro, au Serengeti. Badala ya kusema ninakwenda Tanzania, unasema ninakwenda Kilimanjaro au Serengeti.

Lakini mbona sehemu kama 'Acalpulco' zinajulikana vizuri tu huku zikiwa Mexico?

Ni jambo la kunadi na kuuza tu hivyo vivutio ndio kazi inayohitajika bila lazima ya kubadili jina. Arusha, pamoja na kutojua chanzo cha jina hilo, ni jina zuri tu. Libakie hivyo hivyo.

[media]http://www.youtube.com/watch?v=uvi8-e4pEbQ[/media]
 
Du wachangiaji wamekataa kusoma hoja nilizoziandika A mpaka ... G. ama kweli safari ya kulikomboa taifa hili ni ndefu sana.
 
Kasheshe,
Pamoja na maelezo yako marefu mazuri, lakini bado hujatueleza ni namna gani mabadiliko ya jina yataweza kuongeza kuongeza idadi ya watalii. Ninavyoona mimi ni kuwa ukibadilisha jina itatubidi tuingie kwenye mkakati mwingine mkubwa wa kutangaza mabadiliko hayo.

Kwa mtazamo wangu jambo la kufanya sasa hivi kuwa tuelekeze nguvu zote kutangaza vivutio vyetu vya utalii kwa nia ya kuongeza idadi ya watalii watakaokuja hapa nchini kwani sehemu zenye vivutio vya watalii haviko Arusha au Kilimanjaro pekee.

Kama umekuwa mfuatiliaji sana wa masuala ya yanayohusu utalii nchi yetu haikuwa na mikakati iliyokuwa inaishinda nchi ya Kenya katika kutangaza vivutio vya utalii. Katika siku za hivi karibuni tumeanza kuona juhudi mbalimbali zimeanza kuchukuliwa na serikali katika kutangaza masuala ya utalii. Hii ni hatua chanya nzuri kwani mikakati ya kutangaza utalii inaweza kuendelezwa kwa kupitia njia zilezile ambazo hawa jirani zetu walizitumia kutangaza kuwa Mt. Kilimanjaro iko kwao.

Vilevile iko haja ya kufikiria kuweka vivutio zaidi vya kitalii kwa wale wanaokuja kupanda mlima Kilimanjaro, kwa mfano pale carnival Nairobi imekuwa ni mahali mahususi kwa watalii wanaokwenda kupanda mlima kwenda pale a day before hawajaelekea kupanda mlima. Kwa hiyo hata watalii wenyewe wanazo hizon habari kuwa kabla ya kupanda mlima ni muhimu wakatumia muda wao fulani Carnival.

Njia nyingine ya kuvutia watalii kuja kwetu moja kwa moja ni kuweka ada kwa makampuni ya kitalii yasiyo ya Tanzania iliyo kubwa kiasi cha kuwa-discourage kupitisha watalii wao Kenya.
Kutoa nafuu ya ushuru au vinginevyo kwa muda maalumu kwa makampuni yatakayoleta watalii moja kwa moja nchi bila ya kupitia nchi ya jirani.

Kuimarisha mafunzo ya huduma kwa watalii ili kuweza kutoa huduma bora.

Kwa mtazamo wangu, kubadilisha jina la Mkoa wa Arusha sioni kama kunaweza kuwa na tija itakayoweza kufanikisha malengo unayoyafikiria.

Ningependa pia kushauri kuwa watanzania tujaribu kufanya utafiti wa kutosha kabla hatujafikia maamuzi yeyote.
 
Jina la pili, SERENGETI. Serengeti ni Wilaya ambayo iko mkoa wa MARA, sasa iweje arusha iitwe Serengeti?

You do not "THINK BIG" if you do then there is no problem , Wilaya ya Mara can be renamed.

Remember Waingereza mfano walituachia wilaya ya Pare. sasa Mwanga na Same... anything wrong!!!!

Hoja ni kwamba ni Mara ngapi dunia tunaielekeza kwenye wilaya ya Serengeti, na ni Mara Ngapi dunia tunaielekeza kwenye mji wa Arusha?

Again "THINK BIG"


Wakati munajadili hii hoja angalieni impact from outside world, sio kutoka huku ndani!!!
 
Kasheshe,
Pamoja na maelezo yako marefu mazuri, lakini bado hujatueleza ni namna gani mabadiliko ya jina yataweza kuongeza kuongeza idadi ya watalii. Ninavyoona mimi ni kuwa ukibadilisha jina itatubidi tuingie kwenye mkakati mwingine mkubwa wa kutangaza mabadiliko hayo.
Kweli sikuyaeleza yote kwa kuwa ingekuwa hadithi ndefu zaidi.

Ila napenda kukumbusha tu!!! ipi ni gharama kubadilisha wazungu kujua kwamba Kilimanjaro iko Tanzania kwa matangazo unayosema au kuwafanya automatically kila siku wakiambiwa kuna mkutano mfano unafanyika kwenye jiji la Kilimanjaro, Tanzania wao Automatically watajua Kilimanjaro iko Tanzania!

Suala la kubadili Jina halihitaji fedha yoyote ya kutisha kwa kuwa haufanyi overnight... provided Mh. Rais amepitisha tu... mambo mengi yatabadilishwa tena kwa muda mfupi sana. Suala linalohitaji fedha nyingi ni kutangaza vivutio wakati huo ukiwa huna mbinu za kivionyesha viko nchini mwako!!!


Kwa mtazamo wangu jambo la kufanya sasa hivi kuwa tuelekeze nguvu zote kutangaza vivutio vyetu vya utalii kwa nia ya kuongeza idadi ya watalii watakaokuja hapa nchini kwani sehemu zenye vivutio vya watalii haviko Arusha au Kilimanjaro pekee.

Kwanza sikusema baada ya kubadilisha jina ndio tulale hapana. by the way re-branding ni jambo la Kawaida kwenye marketing... sina haja ya kusema hili sana.

Haya unayosema ndio tuliyokarimishwa mashuleni, lakini kuna njia zingine rahisi sana za kufanya Tanzania iwe branded na Zanzibar and Kilimanjaro.... na hili lina uhusiano mkubwa na kuhakikisha sehemu ambayo ina-host mikutano mikubwa ya kimataifa... inaitaja Kilimanjaro kwa Urahisi zaidi bili kutumia mahela mengi.

Asimilia kubwa hamtaelewa sasa lakini baada ya muda mutaelewa kwa nini ni muhimu.


Jiulize kwa nini wenzenu waliokuwa wanafikiri mbali enzi hizo waliuita ule wa Uwanja wa Kimaitaifa Kilimanjaro na walio Sio Kikatiti au Mererani International Airport?
 
Cosmetics,

Tell us something that we don't know.Like how to increase tourists, preserve the famous equatorial snowcap, provide housing or deal with crime in Arusha.

Tunapenda sana soap operas lakini kuangalia central issues tunagwaya.

Mkuu kweli!!!

Lakini jiulize kwa nini makampuni yanafanya re-branding na kuheshimu na kutunza branding zao kwa nguvu zao zote!!!

Tunataka Sura ya Tanzania kwenye utalii imemfanye mtalii yeyote afikirie Zanzibar, Kilimanjaro and Serengeti...

so what ever we can do to promote hivyo vivutio at affordable cost is welcome unayo hiyo alternative ambayo ni affordable karibu mkuu, mimi hii nimeiona ni mojawapo ya strategy za Kuifanya Tanzania ijulikane kwamba ndiyo yenye Mlima Kilimanjaro, Serengeti National Park, na Zanzibar Island....

And one of it is re-branding the clear channels to make sure... "Kilimanjaro, Serengeti, Zanzibar) care Tanzania tourism flag.

Sasa tunataka kuwenga bango la Kilimanjaro pale linapoonekana na Dunia nzima kwa urahisi zaidi, nayo ni Uwanja wa Ndege wa KIA hii ndiyo iliyokuwa nia ya Wenzetu, sasa tunataka Pale wanapofanyia mikutano, pale wanapolala... etc..
 
Kweli sikuyaeleza yote kwa kuwa ingekuwa hadithi ndefu zaidi. ila napenda kukumbusha tu!!! ni gharama kubadilisha wazungu kujua kwamba Kilimanjaro iko Tanzania au kuwafanya automatically kila siku kuambiwa mkutano mfano unafanyika kwenye jiji la Kilimanjaro na Automatically wajue Kilimanjaro iko Arusha!

Suala la kubadili Jina halihitaji fedha yoyote ya kutisha kwa kuwa haufanyi overnight... provided Mh. Rais amepitisha tu... mambo mengi yatabadilishwa tena kwa muda mfupi sana.




Kwanza sikusema baada ya kubadilisha jina ndio tulale hapana. by the way re-branding ni jambo la Kawaida kwenye marketing... sina haja ya kusema hili sana.

Haya unayosema ndio tuliyokarimishwa mashuleni, lakini kuna njia zingine rahisi sana za kufanya Tanzania iwe branded na Zanzibar and Kilimanjaro.... na hili lina uhusiano mkubwa na kuhakikisha sehemu ambayo ina-host mikutano mikubwa ya kimataifa... inaitaja Kilimanjaro kwa Urahisi zaidi bili kutumia mahela mengi.

Asimilia kubwa hamtaelewa sasa lakini baada ya muda mutaelewa kwa nini ni muhimu.


Jiulize kwa nini wenzenu waliokuwa wanafikiri mbali enzi hizo waliuita ule wa Uwanja wa Kimaita Kilimanjaro na walio Sio Kikatiti au Mererani International Airport?


Kwa mtazamo wangu binafsi mimi nilipokuwa ninachangia thread yako niliona kuwa bado haijajitosheleza na ndiyo maana nilikuomba utoe maelezo ya ziada.
Umekiri kuwa hujaandika kila kitu, sasa ni vema ukaendelea kukamilisha fikra zako badala ya kuanza majibizano ilihali kumbe hujamaliza kujieleza.

Maliza kujieleza then nitarudi kuchangia maana hata wewe mwenye umeliona la kuwa hatutaelewa kwa sasa labda baadae.

Naomba ufafanuzi sijaelewa ulikuwa unamaanisha nini kwa sentensi hii "Haya unayosema ndio tuliyokarimishwa mashuleni,"
 
Kwa mtazamo wangu binafsi mimi nilipokuwa ninachangia thread yako niliona kuwa bado haijajitosheleza na ndiyo maana nilikuomba utoe maelezo ya ziada.
Umekiri kuwa hujaandika kila kitu, sasa ni vema ukaendelea kukamilisha fikra zako badala ya kuanza majibizano ilihali kumbe hujamaliza kujieleza.

Maliza kujieleza then nitarudi kuchangia maana hata wewe mwenye umeliona la kuwa hatutaelewa kwa sasa labda baadae.

Naomba ufafanuzi sijaelewa ulikuwa unamaanisha nini kwa sentensi hii "Haya unayosema ndio tuliyokarimishwa mashuleni,"

Hoja kwa kweli sio kwa ajili ya malumbano... nilisema kwamba mashuleni tumekaririshwa kwamba tutangaze utalii kwa namna fulani... sasa strategy hii niliyotoa kama changamoto ni tofauti na haiko kwenye vitabu moja kwa moja.

Ila bado ukisoma hoja yangu kwa makini (A to G) uta-draw point kwamba kwenye ile A-G kulikuwa na mtiririko wa ku-justify mabadiliko ninayoyaomba bila kuelezea maelezo mengi zaidi. Just go through those points again na nipe specific ipi hailewi logic yake then i can start from there!!!

Solution za Kuikomboa hii nchi mara nyingi hazitakuwa zile popular kama kukamata madini Airport yenye thamani ya mil 150, au kurudisha Bil. 133 za EPA etc... then after that what else... we need vitu endelevu !!! sasa katika kuvitoa hivi kwa kweli vitakuja vingi ambavyo sio popular kama hili langu... lakini eventually people will understand.
 
......Kwa wenyeji wa Arusha ..hili jina lina maana kubwa sana....na ya maana...nakumbuka kuongea na wazee zamani na waliniambia..sema nimesahau..kwa kuwa sikuchukulia umuhimu kwa miaka hiyo..........


wapi MORANI 79...yerrro ..taee njoo elesea iko na maana gani hii jina ati!!!
 
Hoja hii inafaa kuipeleka katika Halmashauri ya Manispaa ya Arusha. Madiwani wana uwezo kisheria kubadili majina ya Miji na vitongoji vyao iwapo wataona kuna umuhimu wa kufanya hivyo.

Pamoja na yote sioni mantiki yoyote ya kuita mji wa Arusha.. Kilimanjaro...!
 
Back
Top Bottom