Filosofia ya Rorya
JF-Expert Member
- Sep 20, 2021
- 3,215
- 3,587
Tujadiliane,
Ufumbuzi wa ugumu wa kufundisha somo la hesabu Tanzania umeshindikana na kufanyika janga la taifa.
Nadhani warasimu waliokasimiwa jukumu la kuleta mfumo rafiki wa ufundishaji hesabu wamejipa dhima hiyo kwa kujihesabia haki ya uelewa wa somo hilo kuliko wengine ambao wangestahili kuwapa ushirikishwaji. Hili peke yake ni tatizo kama lilivyo tatizo la ufundishaji hesabu.
Kadri mtaala wa hesabu unavyobadilishwa tangu 1967 tatizo limeendelea kubaki kama lilivyo kwamba hesabu inawawia wanafunzi wa ngazi zote za elimu ugumu wa kulisoma.
Gharama nyingi zimetumika katika mchakato wa maboresho ya mtaala wa somo la hesabu (yakiwemo masomo mengine) lakini tija ni ndogo sana. Mkwamo wa upatikanaji mfumo rafiki wa kufundisha hesabu hauna utofauti na mkwamo wa Katiba mpya Tanzania.
Ninaamini siyo idadi kubwa ya Watanzania kihivyo hawawezi (wanahofu) somo la hesabu bali ni ufumbuzi wa tatizo umetengeneza tatizo lingine kwenye mchakato wa kutafuta ufumbuzi.
Kwa maoni yangu, nashauri haya yafanyike hata kama ni kwa majaribio (pilot) kwa miaka 5:
1. Wanafunzi wote kwa hatua ya msingi wafundishwe kwa ulazima Mathematical Operations za kuongeza, kutoa, kugawa na kuzidisha, kwa sababu hizi hazikosekani kwenye aina (mada) zote za hesabu kwa ngazi zote za elimu zilizopo duniani.
2. Kwakuwa hesabu ni mtambuka kwenye masomo mengine na ni pana sana, wanafunzi wasibebeshwe zigo lote hilo bali waruhusiwe kubobea kwenye aina fulani ya hesabu ambayo wana uwezo nayo kuanzia ngazi za chini za elimu na kwenye somo la hesabu wasome aina hiyo hiyo pekee hadi hata ngazi ya uzamivu (PhD).
3. Namba 2 hapo juu ikitekelezwa kwa umakini unaoustahili, wanaobobea kwenye hesabu watamaliza mtaala wa hesabu hadi wa chuo kikuu kwa miaka michache ilhali masomo mengine yatakuwa labda yakirefuka muda wake.
4. Wanafunzi waruhusiwe kubobea kwenye mojawapo ya aina (mada) za hesabu zilizopo duniani mfano:-
a) Arithmetics
b) Algebra
c) Geometry
d) Trigonometry
e) Statistics
f) Word Problem nk.
5. Kanuni ya uumbaji inathibitisha kwamba kila binadamu ana kitu anachokiweza. Hivyo kati ya hizo aina (mada) za hesabu lazima tutapata wanaowezea kila mojawapo.
6. Ninaamini kwa hii hypothesis niliyopendekeza, taifa litakuwa na mabingwa wa hesabu kuliko wakati wowote ule katika historia yake, na ari ya kusoma na kufundisha hesabu itaongezeka maana mwanafunzi atasoma anachoweza na anachopenda katika somo la hesabu.
7. Kenya CBC (Competency Based Curriculum au ufundishaji mahiri) yao imedrop baadhi ya mada (topics) za hesabu tangu ngazi za awali za elimu.
8. Hata Isaac Newton hakuwa anajuwa mada zote za hesabu kwenye maisha yake lakini bado anaheshimika duniani kama mtaalam wa hesabu na fizikia. Ni vivyo hivyo kwa Pythagoras (Baba wa Pythagorean Theorem), Muhammad Al-Khwarizmi (Baba wa Algebra), Euclid (Baba wa Geometry), Hipparchus aliyegundua table of chords kwa mara ya kwanza na kuzaa Trigonometry, John Graunt na William Petty waliogundua Statistics, Brahmagupta (Baba wa Arithmetics), na Brahmagupta & Bhaskara waliogundua Fractions.
9. Kwa hypothesis hii taifa litazalisha walimu wabobezi na mabingwa wengi sana wa somo la hesabu.
10. Serikali iondokane na hulka ya kuogopa kujaribu jambo. Woga wako ndiyo mtaji wa adui yako.
Tujadili mada kwa mustakabali wa nchi yetu.
Ufumbuzi wa ugumu wa kufundisha somo la hesabu Tanzania umeshindikana na kufanyika janga la taifa.
Nadhani warasimu waliokasimiwa jukumu la kuleta mfumo rafiki wa ufundishaji hesabu wamejipa dhima hiyo kwa kujihesabia haki ya uelewa wa somo hilo kuliko wengine ambao wangestahili kuwapa ushirikishwaji. Hili peke yake ni tatizo kama lilivyo tatizo la ufundishaji hesabu.
Kadri mtaala wa hesabu unavyobadilishwa tangu 1967 tatizo limeendelea kubaki kama lilivyo kwamba hesabu inawawia wanafunzi wa ngazi zote za elimu ugumu wa kulisoma.
Gharama nyingi zimetumika katika mchakato wa maboresho ya mtaala wa somo la hesabu (yakiwemo masomo mengine) lakini tija ni ndogo sana. Mkwamo wa upatikanaji mfumo rafiki wa kufundisha hesabu hauna utofauti na mkwamo wa Katiba mpya Tanzania.
Ninaamini siyo idadi kubwa ya Watanzania kihivyo hawawezi (wanahofu) somo la hesabu bali ni ufumbuzi wa tatizo umetengeneza tatizo lingine kwenye mchakato wa kutafuta ufumbuzi.
Kwa maoni yangu, nashauri haya yafanyike hata kama ni kwa majaribio (pilot) kwa miaka 5:
1. Wanafunzi wote kwa hatua ya msingi wafundishwe kwa ulazima Mathematical Operations za kuongeza, kutoa, kugawa na kuzidisha, kwa sababu hizi hazikosekani kwenye aina (mada) zote za hesabu kwa ngazi zote za elimu zilizopo duniani.
2. Kwakuwa hesabu ni mtambuka kwenye masomo mengine na ni pana sana, wanafunzi wasibebeshwe zigo lote hilo bali waruhusiwe kubobea kwenye aina fulani ya hesabu ambayo wana uwezo nayo kuanzia ngazi za chini za elimu na kwenye somo la hesabu wasome aina hiyo hiyo pekee hadi hata ngazi ya uzamivu (PhD).
3. Namba 2 hapo juu ikitekelezwa kwa umakini unaoustahili, wanaobobea kwenye hesabu watamaliza mtaala wa hesabu hadi wa chuo kikuu kwa miaka michache ilhali masomo mengine yatakuwa labda yakirefuka muda wake.
4. Wanafunzi waruhusiwe kubobea kwenye mojawapo ya aina (mada) za hesabu zilizopo duniani mfano:-
a) Arithmetics
b) Algebra
c) Geometry
d) Trigonometry
e) Statistics
f) Word Problem nk.
5. Kanuni ya uumbaji inathibitisha kwamba kila binadamu ana kitu anachokiweza. Hivyo kati ya hizo aina (mada) za hesabu lazima tutapata wanaowezea kila mojawapo.
6. Ninaamini kwa hii hypothesis niliyopendekeza, taifa litakuwa na mabingwa wa hesabu kuliko wakati wowote ule katika historia yake, na ari ya kusoma na kufundisha hesabu itaongezeka maana mwanafunzi atasoma anachoweza na anachopenda katika somo la hesabu.
7. Kenya CBC (Competency Based Curriculum au ufundishaji mahiri) yao imedrop baadhi ya mada (topics) za hesabu tangu ngazi za awali za elimu.
8. Hata Isaac Newton hakuwa anajuwa mada zote za hesabu kwenye maisha yake lakini bado anaheshimika duniani kama mtaalam wa hesabu na fizikia. Ni vivyo hivyo kwa Pythagoras (Baba wa Pythagorean Theorem), Muhammad Al-Khwarizmi (Baba wa Algebra), Euclid (Baba wa Geometry), Hipparchus aliyegundua table of chords kwa mara ya kwanza na kuzaa Trigonometry, John Graunt na William Petty waliogundua Statistics, Brahmagupta (Baba wa Arithmetics), na Brahmagupta & Bhaskara waliogundua Fractions.
9. Kwa hypothesis hii taifa litazalisha walimu wabobezi na mabingwa wengi sana wa somo la hesabu.
10. Serikali iondokane na hulka ya kuogopa kujaribu jambo. Woga wako ndiyo mtaji wa adui yako.
Tujadili mada kwa mustakabali wa nchi yetu.