Tuanzishe tuzo kuenzi Utamaduni na Sanaa yetu - Iwe na donge nono 280 Mil. kwa msanii

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
Hivi, kati ya mambo yote Rais wetu hufanya na kutoa tuzo hatuna tuzo fulani ambazo tunaweza kuwapa wasanii wetu na kuwatambua kwa mchango wao katika kuendeleza na kudumisha utamaduni wetu? Watu kama Bi. Kidude, Remmy Ongala, au hata kuwakumbuka waliotangulia mbele ya haki kama kina Mbaraka Mwishehe na Marijani Rajabu? Au ndio imetoka tena?

Nafahamu kuna Nishani ya Shaaban Robert;kwanini hii isiwe jina la Tuzo ya Shaaban Robert ambapo wasanii mbalimbali (wasioazidi labda watano kwa mwaka) ambao wametoa mchango mkubwa katika kazi za fasihi na sanaa katika miaka isiyopungua ishirini ya kazi zao.

Isiwe tuzo tu ya maneno tu bali pia iendane na mkono wa Taifa lenye shukrani na ninapendekeza kitita kisipungue shilingi milioni 50 (kama dola elfu 50). Kiasi hiki ukitoa kwa watu watano kwa mwaka tu ni kama dola 250 elfu; ukiweka kiasi hicho kwa mwanga wa VX 8 za Mawaziri wenu utaona ni gari moja tu la Waziri - kwa hiyo hoja ya sisi ni maskini inavunjika kabla haijatolewa! (hapa tunaweza kufikiria hata kuongeza na kufanya iwe sawa na kiasi hicho cha 280 milioni!

Ni lazima tutunze na kuenzi sanaa yetu na wasanii wetu. Tuwaheshimu wale waliotuburudisha na kutufanya tufurahia utanzania na uafrika wetu. Vinginevyo tutakuwa ni taifa lisilo na utamaduni; taifa lisilo na utambulisho. Nyerere alisema vizuri kabisa kuwa athari kubwa zaidi ya ukoloni ni kujengwa fikra kuwa utamaduni wetu ni duni na kila kilicho chetu hakifai kuenziwa!

Naomba kutoa hoja, hasa kwa ndugu yangu Nchimbi.. tuwaenzi wasanii wetu. Ni kwa kufanya hivyo tutajikuta tunaenzi urithi wetu sisi wenyewe. Maana tusipoangalia Ubalozi wa Uingereza utaanzisha tuzo ya kuenzi wasanii wetu na sisi tutaenda kushughudia na kushangialia kuwa wazungu wametuhusudu!

Natoa hoja!
 
Jambo jema sana.
Zamani RTD kulikuwa na kipindi kinaitwa Tumbuizo Asilia kilikuwa kinaendeshwa na Maremu Michael Katembo.
Leo hakipo wala hakisikiki.
Kijiji cha Makumbusho pana maonyesho ya ngoma za kijadi, cha ajabu wanajaa wazungu watupu.
Sijui nini hitma ya utamaduni wetu
 
Naunga mkono mawazo haya. Unajua kadiri siku zinavyokwenda ndivyo tunavyozidi kumezwa na utamaduni wa wazungu kiasi kwamba vijana wa sasa hawajui kuwa tuna mambo yetu ambayo ni mazuri na nadra kuyapata sehemu zingine duniani.
 
Maana nyumba ya sanaa imeuzwa; na kwenye luninga nimeangalia EATV sijaona kipindi kikionesha ngoma za kiafrika; yaani watoto wetu wanaona aibu kucheza lizombe lakini ukiwawekea Rihanna wataruruka kama kuku maji!
 
Maana nyumba ya sanaa imeuzwa; na kwenye luninga nimeangalia EATV sijaona kipindi kikionesha ngoma za kiafrika; yaani watoto wetu wanaona aibu kucheza lizombe lakini ukiwawekea Rihanna wataruruka kama kuku maji!

Mkuu enzi zile za Asilia Salam, Tumbuizo Asilia, Mkoa kwa Mkoa hazipo tena...Wale wakongwe wa DDC Kibisa Ngoma Troupe, Muungano Cultural Troupe, JKT, JWTZ siku hizi hawana dili tena hakuna mtu anataka kwenda kuwaangalia maonyesho yao. Kila mtu anataka kwenda kuwaona wazee wa Ngwasuma!!
 
Shangingi moja ni 280 milioni. halafu bei yenyewe ya kupigwa maana unicef shangingi hilohilo wananunua kwa 190 milioni. tuna mashangingi 40,000 mama yangu 11,200,000,000,000 = trilioni 11

mwingine anisaidie kuleta data kamili yaani Vx na V8 tofauti zake halafu tujue gharama halisi

amakweli hii ni nchi ya wajinga
 
Mkuu enzi zile za Asilia Salam, Tumbuizo Asilia, Mkoa kwa Mkoa hazipo tena...Wale wakongwe wa DDC Kibisa Ngoma Troupe, Muungano Cultural Troupe, JKT, JWTZ siku hizi hawana dili tena hakuna mtu anataka kwenda kuwaangalia maonyesho yao. Kila mtu anataka kwenda kuwaona wazee wa Ngwasuma!!

huko tunakokwenda viongozi wanapopokelewa itabidi waanze kupokelewa na vikundi vya hip hop, n.k yaani hata wao wanaona aibu ya ngoma zao!
 
huko tunakokwenda viongozi wanapopokelewa itabidi waanze kupokelewa na vikundi vya hip hop, n.k yaani hata wao wanaona aibu ya ngoma zao!

Wameshanza taratibu si umeona kampeni za uchaguzi zilikuwa zinapambwa na kina nani?
 
Hivi, kati ya mambo yote Rais wetu hufanya na kutoa tuzo hatuna tuzo fulani ambazo tunaweza kuwapa wasanii wetu na kuwatambua kwa mchango wao katika kuendeleza na kudumisha utamaduni wetu? Watu kama Bi. Kidude, Remmy Ongala, au hata kuwakumbuka waliotangulia mbele ya haki kama kina Mbaraka Mwishehe na Marijani Rajabu? Au ndio imetoka tena?

Nafahamu kuna Nishani ya Shaaban Robert;kwanini hii isiwe jina la Tuzo ya Shaaban Robert ambapo wasanii mbalimbali (wasioazidi labda watano kwa mwaka) ambao wametoa mchango mkubwa katika kazi za fasihi na sanaa katika miaka isiyopungua ishirini ya kazi zao.

Isiwe tuzo tu ya maneno tu bali pia iendane na mkono wa Taifa lenye shukrani na ninapendekeza kitita kisipungue shilingi milioni 50 (kama dola elfu 50). Kiasi hiki ukitoa kwa watu watano kwa mwaka tu ni kama dola 250 elfu; ukiweka kiasi hicho kwa mwanga wa VX 8 za Mawaziri wenu utaona ni gari moja tu la Waziri - kwa hiyo hoja ya sisi ni maskini inavunjika kabla haijatolewa! (hapa tunaweza kufikiria hata kuongeza na kufanya iwe sawa na kiasi hicho cha 280 milioni!

Ni lazima tutunze na kuenzi sanaa yetu na wasanii wetu. Tuwaheshimu wale waliotuburudisha na kutufanya tufurahia utanzania na uafrika wetu. Vinginevyo tutakuwa ni taifa lisilo na utamaduni; taifa lisilo na utambulisho. Nyerere alisema vizuri kabisa kuwa athari kubwa zaidi ya ukoloni ni kujengwa fikra kuwa utamaduni wetu ni duni na kila kilicho chetu hakifai kuenziwa!

Naomba kutoa hoja, hasa kwa ndugu yangu Nchimbi.. tuwaenzi wasanii wetu. Ni kwa kufanya hivyo tutajikuta tunaenzi urithi wetu sisi wenyewe. Maana tusipoangalia Ubalozi wa Uingereza utaanzisha tuzo ya kuenzi wasanii wetu na sisi tutaenda kushughudia na kushangialia kuwa wazungu wametuhusudu!

Natoa hoja!

................ mzee sasa wengine twashindwa kutofautisha WASANII gani wawe walengwa. Kama common denominator hapa ni USANII na UTAMADUNI wetu, mbona WASANII katika nyanja za siasa nao wanaingia kundini? Kwa haraka haraka zawadi ya millioni 280 tayari weshalamba mawaziri siku nyingi. Mashangingi si unayaona? au wajameni tafadhali nielimisheni. Kina Vasco na wenzake, wale vinara wa lonolongo si WASANII au napotosha mada?
 
Hivi utamaduni wetu ni wa kujivunuia au nao tuuweke jumba la makumbusho?

Kwani kuna utamaduni uliobaki zaidi ya lugha zetu za asili? Hakuna vyakula vya asili( vyooote tunaunga nyanya), hakuna ngoma za asili( zilizopo zimechakachuliwa sana), hakuna jando wala unyago, uharibifu wa mazingira umemaliza kabisa ujenzi wa nyumba za asili, harusi na sherehe zingine na hata mazishi sio yale ya asili( zamani ulikuwa huchangiwi ili uoe!)
Baadhi ya lugha na makabila ya asili vimeanza kutoweka kwa kasi ya ajabu.
 
Kwani kuna utamaduni uliobaki zaidi ya lugha zetu za asili? Hakuna vyakula vya asili( vyooote tunaunga nyanya), hakuna ngoma za asili( zilizopo zimechakachuliwa sana), hakuna jando wala unyago, uharibifu wa mazingira umemaliza kabisa ujenzi wa nyumba za asili, harusi na sherehe zingine na hata mazishi sio yale ya asili( zamani ulikuwa huchangiwi ili uoe!)
Baadhi ya lugha na makabila ya asili vimeanza kutoweka kwa kasi ya ajabu.


Lakini mila zetu za asili zina hadhi sawa na mila za watu wengine?
 
Jamii inatakiwa ifanye kazi kubwa saana kuukomboa utamaduni wetu kwani jamii haina habari kwamba utamaduni wetu umetekwa nyara na ule wa wazungu.mfano wewe mwenyewe unawatu wangapi unaojua kwamba hawa ni wakwetu kijijini.embu waambie kwamba kesho tuvae nguo za asili afu tukacheze ngoma pale k.koo uone kama utapata mtu.
 
Kuhusu tuzo kwa wasanii inawezekana ila wasani kwetu hawathaminiwi. Kuna watu kama salehe jabri na mbunge wa mbeya mr2.hawa kwa mimi ninaamini ndo walio leta bongo fleva hapa nchini lakini je waliwahi kupewa tuzo kubwa ya heshima?
 
Hivi, kati ya mambo yote Rais wetu hufanya na kutoa tuzo hatuna tuzo fulani ambazo tunaweza kuwapa wasanii wetu na kuwatambua kwa mchango wao katika kuendeleza na kudumisha utamaduni wetu? Watu kama Bi. Kidude, Remmy Ongala, au hata kuwakumbuka waliotangulia mbele ya haki kama kina Mbaraka Mwishehe na Marijani Rajabu? Au ndio imetoka tena?

Nafahamu kuna Nishani ya Shaaban Robert;kwanini hii isiwe jina la Tuzo ya Shaaban Robert ambapo wasanii mbalimbali (wasioazidi labda watano kwa mwaka) ambao wametoa mchango mkubwa katika kazi za fasihi na sanaa katika miaka isiyopungua ishirini ya kazi zao.

Isiwe tuzo tu ya maneno tu bali pia iendane na mkono wa Taifa lenye shukrani na ninapendekeza kitita kisipungue shilingi milioni 50 (kama dola elfu 50). Kiasi hiki ukitoa kwa watu watano kwa mwaka tu ni kama dola 250 elfu; ukiweka kiasi hicho kwa mwanga wa VX 8 za Mawaziri wenu utaona ni gari moja tu la Waziri - kwa hiyo hoja ya sisi ni maskini inavunjika kabla haijatolewa! (hapa tunaweza kufikiria hata kuongeza na kufanya iwe sawa na kiasi hicho cha 280 milioni!

Ni lazima tutunze na kuenzi sanaa yetu na wasanii wetu. Tuwaheshimu wale waliotuburudisha na kutufanya tufurahia utanzania na uafrika wetu. Vinginevyo tutakuwa ni taifa lisilo na utamaduni; taifa lisilo na utambulisho. Nyerere alisema vizuri kabisa kuwa athari kubwa zaidi ya ukoloni ni kujengwa fikra kuwa utamaduni wetu ni duni na kila kilicho chetu hakifai kuenziwa!

Naomba kutoa hoja, hasa kwa ndugu yangu Nchimbi.. tuwaenzi wasanii wetu. Ni kwa kufanya hivyo tutajikuta tunaenzi urithi wetu sisi wenyewe. Maana tusipoangalia Ubalozi wa Uingereza utaanzisha tuzo ya kuenzi wasanii wetu na sisi tutaenda kushughudia na kushangialia kuwa wazungu wametuhusudu!

Natoa hoja!

Mkuu Mkjj wazo lako ni poa sana, mm pia nimewahi kuwa na wazo la kutoa awards kwa innovators wa kitanzania kwa ajili ya kupromote innovation. Mfano a simple machine ya kuchambua mchele, au kukuna nazi (auto and large scale), mashine ya kuvuna mahindi etc.

Lakini sasa tunapokuja kwenye nchi iliyofisadiwa kuanzia fikra, mawazo, na hata utendaji usijeshangaa tuzo hizi wanapewa watu ambao hawakustahili na hatimaye maana nzima ya tuzo hizo za sanaa kupotea kabisa. Mwisho wa siku kuonekana just business as usual. Hivyo basi mimi pamoja na kuunga mkono naona kuna haja pia kuchangia modality ya namna gani tuzo hizo ziwe, vigezo, uchaguaji/upigaji kura etc.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom