Tuanze kwa dr.harrison mwakyembe, na twende mbele zaidi!

Mbelwa Germano

JF-Expert Member
May 7, 2011
789
289
Mwanzoni mwa mwaka 2011 Mh.Mwakyembe alikaririwa na vyombo vya habari akisema kuna watu wanataka kumuua. Lakini hakuishia alimtaja na Dr. Slaa kama miongoni mwa watu wachache ambao walikuwa kwenye kundi hilo. Vilevile itakumbukwa kwamba Dr. Slaa alipokuwa Mbunge alikuta vinasa sauti ndani ya chumba chake alichofikia kwenye hoteli ya 56. Mpaka leo hatujui malengo ya kumwekea vipaza sauti yalikuwa ni nini na nani amehusika?

Wapo watu wanaodhani kwamba Dr.Slaa anatafuta umaarufu bila kuhusisha vichwa vyao kufikiri. Kwa hoja ya umarufu je wanaamini kwamba Dr. Mwakyembe alikuwa anamtafutia umaarufu Dr.Slaa? Uhai wa mtu unathamani kuliko CCM, CDM, CUF n.k. na ni haki ya kimsingi kwa kila raia wa nchi yetu ya Tanzania. Lazima tutambue Lema, Mnyika n.k. ni political figures ambao wanapata coverage kubwa, hivyo tatizo lisiwe kwasababu ni viongozi wa CDM bali tatizo ni hatarisho la UHAI wao.

Kama ni ushahidi basi Dr. Mwakyembe ameukalia, na tuanze hapa. Kupotosha wajibu wetu ya kufikiri ni kulundika upumbavu ndani ya fikra zetu na kupotosha wajibu wa kibinadamu wa kufikiri kwa bidii. Kama ni UZUSHI tupinge kwa HOJA pevu na si HOJA nyepesinyepesi.
 
Mwanzoni mwa mwaka 2011 Mh.Mwakyembe alikaririwa na vyombo vya habari akisema kuna watu wanataka kumuua. Lakini hakuishia alimtaja na Dr. Slaa kama miongoni mwa watu wachache ambao walikuwa kwenye kundi hilo. Vilevile itakumbukwa kwamba Dr. Slaa alipokuwa Mbunge alikuta vinasa sauti ndani ya chumba chake alichofikia kwenye hoteli ya 56. Mpaka leo hatujui malengo ya kumwekea vipaza sauti yalikuwa ni nini na nani amehusika?

Wapo watu wanaodhani kwamba Dr.Slaa anatafuta umaarufu bila kuhusisha vichwa vyao kufikiri. Kwa hoja ya umarufu je wanaamini kwamba Dr. Mwakyembe alikuwa anamtafutia umaarufu Dr.Slaa? Uhai wa mtu unathamani kuliko CCM, CDM, CUF n.k. na ni haki ya kimsingi kwa kila raia wa nchi yetu ya Tanzania. Lazima tutambue Lema, Mnyika n.k. ni political figures ambao wanapata coverage kubwa, hivyo tatizo lisiwe kwasababu ni viongozi wa CDM bali tatizo ni hatarisho la UHAI wao.

Kama ni ushahidi basi Dr. Mwakyembe ameukalia, na tuanze hapa. Kupotosha wajibu wetu ya kufikiri ni kulundika upumbavu ndani ya fikra zetu na kupotosha wajibu wa kibinadamu wa kufikiri kwa bidii. Kama ni UZUSHI tupinge kwa HOJA pevu na si HOJA nyepesinyepesi.
Mkuu hawa wabishi wasiotaka kuona ukweli kina Dr Nchimbi sehemu yao ni The Hague inawasubiria sijui hawaoni wenzao wanapelekwa wapi????

 
Back
Top Bottom