Tuangazie rushwa adui wa maendeleo

Mema Tanzania

Member
Feb 23, 2020
66
65
Tuangazie #Rushwa

Mema Corruption.png

Rushwa ni aina ya ukosefu wa uaminifu au kosa la jinai linalofanywa na mtu, taasisi, au shirika lililopewa madaraka, kujipatia faida haramu au kutumia nguvu vibaya kwa faida binafsi.

Mema Corruption 1.png

Rushwa inamaliza imani, inadhoofisha demokrasia, inakwamisha, maendeleo ya uchumi na inazidisha umaskini, mgawanyiko wa kijamii, kutokuwepo usawa na shida ya mazingira.

Mema Corruption 2.png

Kufichua rushwa na kuwawajibisha watoa na wala rushwa kunaweza kutokea tu ikiwa tunaelewa jinsi rushwa na ufisadi unavyofanya kazi na mifumo inayowezesha.

Mema Corruption 3.png

Misingi ya rushwa

- Rushwa inaweza kuwa ya aina nyingi, na inaweza kujumuisha tabia zifuatazo.

  1. Watumishi wa umma wanaodai au kuchukua pesa au upendeleo badala ya huduma.
  2. Wanasiasaa kutumia vibaya pesa za umma au kutoa kazi za umma au mikataba kwa wafadhili wao, marafiki na familia.
  3. Wanasiasa kuwahonga maofisa kupata mikataba yenye faida kubwa.

Mema Corruption 4.png

Rushwa inaweza kutokea mahali popote katika biashara, serikali, mahakama, vyombo vya habari, asasi za kiraia na sekta zote kuanzia afya, elimu hadi miundombinu na michezo.

Mema Corruption 5.png

Rushwa inaweza kuhusisha mtu yeyote: wanasiasa, maafisa wa serikali, wafanyakazi wa umma, wafanyabiashara au wananchi.

Mema Corruption 6.png

Rushwa na ufisadi hufanyika katika vivuli, mara nyingi kwa msaada wa wataalamu wa uwezeshaji kama mabenki, wanasheria, wahasibu, mifumo ya kifedha na kampuni zisizojulikana zinazoruhusu kushamiri kwa mafisadi na kuficha utajiri wao.

Mema Corruption 7.png

Rushwa huendana na mazingira yanayobadilika. Inaweza kubadilika kwa kujibu mabadiliko ya kanuni, sheria na hata teknolojia.

Mema Corruption 8.png

Athari za rushwa

Kisiasa | Uhuru wa muhusika na utawala wa sheria.​
Kijamii | Ushiriki wako na hata imani yako kwa serikali.​
Kimazingira | Nafasi yako ya mazingira mazuri na mustakbali endelevu.​
Kiuchumi | Nafasi yako ya kujenga na kukuza utajiri.​

Mema Corruption 9.png

#MemaAgainstCorruption

Tufuate kupitia Facebook, Twitter, Instagram na Medium - Mema Tanzania www.linkr.ee/mematanzania
 
Back
Top Bottom