Kijakazi
JF-Expert Member
- Jun 26, 2007
- 6,398
- 8,883
Ukiangalia mambo simple sana mfano tu mdogo kwamba sisi tunajipendekeza zaidi, Dar kuna Barabara ya Kenyata, inaitwa Kenyata drive ni kwa wadosi huko ni moja kati ya barabara bora muhimu kabisa Dar wakati Nairobi mtaa wa Nyerere haufiki hata km 2 na ukimuuliza Mnairobi wa kawaida wapi Mtaa wa Nyerere ulipo haujui, wakati Dar karibia kila mwana Dar anajua Kenyata drive.
Haya akaja Kikwete akafuta barabara ya kihistoria inayotoka Ikulu kupita Baharini akaita Barack Obama kumbuka Kenya kwenyewe sijui kama kuna Mtaa maarufu wa Barack Obama ile barabara mpya ya Kawe ambayo ni posh area inakwenda kilometa kibao Kikwete kaita Mwai Kibaki ukiuliza Mwai Kibaki kaifanyia Tanzania kustahili heshima kama hiyo sioni wakati sijaona Mtaa wa Kikwete au Kikwete road Nairobi, tena Kikwete hata alienda kuwasuluhisha walivyopigana vita lkn mbona hakuna kumbukumbu yake popote Kenya? Kibaki kaifanyia Tanzania unaweza kuniambia?
Hayo ni mambo machache tu ambayo yanaonekana kwamba hatuna uhusiano bali tuna kujipendekeza, hakuna Mwanasiasa wa Kenya ambaye atakuwa na matatizo na Serikali ya Kenya akakimbilia Tanzania lkn kinyume chake ni kawaida, Samia alienda Kenya no body cared, Uhuru Kenyata kuja Dar utafikiri yeye ndiyo Raisi wa Tanzania yupo kila mahali media zote, hata hapa JF ni yeye tu.
Raisi wetu kutwa kuomba msamaha kwa Kenya lkn sijawahi kusikia Raisi wa Kenya akiomba msamaha popote kwa Tanzania pamoja na kwamba wametufanyia ushenzi mwingi tu, Watanzania walifurumushwa na kufukuzwa kutoka Nairobi mbona Uhuru hajaomba msamaha kwetu?
Haya akaja Kikwete akafuta barabara ya kihistoria inayotoka Ikulu kupita Baharini akaita Barack Obama kumbuka Kenya kwenyewe sijui kama kuna Mtaa maarufu wa Barack Obama ile barabara mpya ya Kawe ambayo ni posh area inakwenda kilometa kibao Kikwete kaita Mwai Kibaki ukiuliza Mwai Kibaki kaifanyia Tanzania kustahili heshima kama hiyo sioni wakati sijaona Mtaa wa Kikwete au Kikwete road Nairobi, tena Kikwete hata alienda kuwasuluhisha walivyopigana vita lkn mbona hakuna kumbukumbu yake popote Kenya? Kibaki kaifanyia Tanzania unaweza kuniambia?
Hayo ni mambo machache tu ambayo yanaonekana kwamba hatuna uhusiano bali tuna kujipendekeza, hakuna Mwanasiasa wa Kenya ambaye atakuwa na matatizo na Serikali ya Kenya akakimbilia Tanzania lkn kinyume chake ni kawaida, Samia alienda Kenya no body cared, Uhuru Kenyata kuja Dar utafikiri yeye ndiyo Raisi wa Tanzania yupo kila mahali media zote, hata hapa JF ni yeye tu.
Raisi wetu kutwa kuomba msamaha kwa Kenya lkn sijawahi kusikia Raisi wa Kenya akiomba msamaha popote kwa Tanzania pamoja na kwamba wametufanyia ushenzi mwingi tu, Watanzania walifurumushwa na kufukuzwa kutoka Nairobi mbona Uhuru hajaomba msamaha kwetu?