Tuamue lipi Ili tuondokane na siasa za chuki?

Kwisense

JF-Expert Member
Sep 7, 2017
475
1,138
Kuna 'options' kadhaa.. Tutumie "AU" katika kutoa ushauri wetu kwa wanasiasa wa upinzani haswaa CUF na CHADEMA na NCCR-MAGEUZI kwenye mtanziko huu wa kisiasa.


"AU" YA KWANZA..

Wabunge wa upinzani ambao wapo bungeni, aidha wajiondoe katika ubunge wao, waliache bunge likiwa na upande mmoja wa CCM kwa sababu ni wazi hawataki kuona upande wa upinzani ukishamiri ndani ya bunge la Jamhuri ya muungano. mtakuwa tayari kwa hili? Ngumu kidogo.

"AU" YA PILI.

Viongozi wa Taasisi hizo watangaze sasa rasmi kurejesha vuguvugu la UKUTA. hii ni Moja ya 'AU' ngumu, yenye hatari nyingi lakini yenye manufaa makubwa sana. Wataumia watu, watakufa lakini nafikiri baada ya hapo mambo yatakuwa sawa. UKUTA ni muhimu sasa kuliko hata septemba mosi ya 2016. UMOJA WA KUPAMBANA NA UDIKTETA..... Simama, tuhesabiwe.

"AU" YA TATU

Endeleeni na ubunge wenu, lakini ndani ya UKAWA na ikiwezekana na wengine wenye kuwaunga mkono, endelezeni 'harakati' za kuitaka katiba Mpya kwa machozi, jasho na damu. Katiba yenye kutambua muundo Mpya wa tume ya uchaguzi, yenye sheria Mpya ya uchaguzi na kanuni zake. Hii ni kabla ya 2019. Hii pia Kuna kupoteza UHAI na kupata majeraha. Lakini ni bora.

"AU" YA NNE.

Tuendelee kuisho kwa maigizo haya yanayoendelea sasa. Watu wenu na ninyi wenyewe mkiendelea kuteswa na kuumizwa. Mkiendelea kuishi kwa 'hofu' ndani ya nchi yenu wenyewe. Naamini, wale wachache wenye KUKEMEA ndio wapo kwenye hatari, wale wenye kunufaika na siasa hata wakiwa upande huu wa 'upinzani' wataendelea kuwa salama, maana sio 'wakosoaji'.

"AU" YA TANO.

Kuchagua kufanya siasa zenye kuwapendeza watawala. Lakini zenye kuwaondolea 'uaminifu' kwa wapiga kura. Kuchagua kuendelea na HARAKATI au kuachana na HARAKATI na kuchukua mkondo wa HARAKATI katika siasa za kidhalimu za Afrika. Siasa za Afrika pasipokuwa na HARAKATI ni uongo. Mikakati iwepo, isiachwe lakini muhimu ni HARAKATI. watawala hawapendi HARAKATI.

MMM
 
Godbless Lema anazuiwa kufanya mikutano yake 'halali' kama mbunge wa jimbo la ARUSHA mjini, ANALALAMIKA..

Peter Msigwa anazuiwa kufanya mikutano yake rasmi ya kibunge jimboni kwake, ANALALAMIKA...

SUGU anakamatwa, anapewa 'kesi' isiyokuwa na macho, anatupwa ngome, ananyimwa dhamana kwa kesi yenye dhamana, anakaa ngome siku 24, MNALAANI.

Wabunge wa upinzani wanakamatwa ovyo, wanatolewa bungeni ovyo, wanafungiwa vikao vya Bunge kwa kipindi kirefu..., MNALAANI..

Linatolewa zuio/katazo haramu la kutokufanya shughuli za kisiasa hadi 2020 kwa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu.., MNALAANI..

Mawazo, Mvungi, Mbwambo, Daniel John, Wanauwawa kikatili kwa kuchinjwa, wengine mchana wa Jua kali kabisa.., MNALAANI.

Tundu Lissu, Mbunge, Rais wa TLS, mnadhimu wa KUB, mwanasheria wa CDM.., anapigwa risasi zaidi ya 38 hadharani mchana kweupee (hii ni hatari zaidi aise)..., MNALAANI..

Ben RABIU Focas wa Saanane anapote(a)zwa kwa Zaidi ya mwaka sasa, watu wako kimya kabisa na wamemsahau 'mpiganaji' mwenzao. Hatujui yuko HAI au MFU.., MNALAANI..

Mkutano wa CHADEMA Arusha pale SOWETO watu wanapigwa bomu na risasi za SMG, watu wanakufa na kujeruhiwa.., MNALAANI...

Mwangosi analipuliwa bomu.., utumbo unamwagika nje, na maisha yanaendelea, bado tu mnaendelea, MNALAANI..

Wabunge wa upinzani (Halima Mdee, Esther Bulaya) wamafungiwa kutohudhuria vikao vya bunge kwa mwaka mzima, mnaendelea KULAANI.

Waandamanaji wasiokuwa na silaha wanafyatuliwa risasi za moto, watu wenu wanajeruhiwa, wanakufa, MNALAANI.

HIVI, mmewahi kujiuliza hata kidogo, "laana" zenu zimewahi kutenda miujiza!? "malalamiko" yenu yamewahi kusikilizwa!? To be is to do.., kama hamuwezi kuwa chama cha siasa tena basi jaribu kuanzisha taasisi ya kidini.., itafaa zaidi.. Wakati ni sasa, it's either 'HARAKATI' or 'dieing with MIKAKATI'.

MTAKWISHA, hii ni Afrika, usiposhtuka, utazikwa ukiwa HAI.. waonesheni 'WATESI' wenu upande wenu wa pili. Simameni mpate kuhesabiwa. Mkipenda 'viyoyozi' kamwe hamtoweza kutoka hapo mlipokwama. Good morning compatriots.

MMM
 
Kuna 'options' kadhaa.. Tutumie "AU" katika kutoa ushauri wetu kwa wanasiasa wa upinzani haswaa CUF na CHADEMA na NCCR-MAGEUZI kwenye mtanziko huu wa kisiasa.


"AU" YA KWANZA..

Wabunge wa upinzani ambao wapo bungeni, aidha wajiondoe katika ubunge wao, waliache bunge likiwa na upande mmoja wa CCM kwa sababu ni wazi hawataki kuona upande wa upinzani ukishamiri ndani ya bunge la Jamhuri ya muungano. mtakuwa tayari kwa hili? Ngumu kidogo.

"AU" YA PILI.

Viongozi wa Taasisi hizo watangaze sasa rasmi kurejesha vuguvugu la UKUTA. hii ni Moja ya 'AU' ngumu, yenye hatari nyingi lakini yenye manufaa makubwa sana. Wataumia watu, watakufa lakini nafikiri baada ya hapo mambo yatakuwa sawa. UKUTA ni muhimu sasa kuliko hata septemba mosi ya 2016. UMOJA WA KUPAMBANA NA UDIKTETA..... Simama, tuhesabiwe.

"AU" YA TATU

Endeleeni na ubunge wenu, lakini ndani ya UKAWA na ikiwezekana na wengine wenye kuwaunga mkono, endelezeni 'harakati' za kuitaka katiba Mpya kwa machozi, jasho na damu. Katiba yenye kutambua muundo Mpya wa tume ya uchaguzi, yenye sheria Mpya ya uchaguzi na kanuni zake. Hii ni kabla ya 2019. Hii pia Kuna kupoteza UHAI na kupata majeraha. Lakini ni bora.

"AU" YA NNE.

Tuendelee kuisho kwa maigizo haya yanayoendelea sasa. Watu wenu na ninyi wenyewe mkiendelea kuteswa na kuumizwa. Mkiendelea kuishi kwa 'hofu' ndani ya nchi yenu wenyewe. Naamini, wale wachache wenye KUKEMEA ndio wapo kwenye hatari, wale wenye kunufaika na siasa hata wakiwa upande huu wa 'upinzani' wataendelea kuwa salama, maana sio 'wakosoaji'.

"AU" YA TANO.

Kuchagua kufanya siasa zenye kuwapendeza watawala. Lakini zenye kuwaondolea 'uaminifu' kwa wapiga kura. Kuchagua kuendelea na HARAKATI au kuachana na HARAKATI na kuchukua mkondo wa HARAKATI katika siasa za kidhalimu za Afrika. Siasa za Afrika pasipokuwa na HARAKATI ni uongo. Mikakati iwepo, isiachwe lakini muhimu ni HARAKATI. watawala hawapendi HARAKATI.

MMM

Ni majanga ndugu zangu. 'Political landscape' ya tanzania ni chafu na ni hatari. Nasikitika sana kuwa siasa za maji taka zilizokuwa zikiendeshwa na Nduli / mbabe Salamin Amour kule znz aliyewagawa wazanzibari kwa misingi ya uchama, mtu alikozaliwa , sasa siasa hizo zimehamia tanzanai bara. Ni huzuni kubwa. Matumizi mabaya ya vyombo vya dola dhidi ya wapinzani na raia nayo pia yanaongezeka kwa kasi sambamba na vitendoi vya ukatili, mauaji, watu kupotea na kwengine kuumizwa.

Nifikiri SMT//SMZ/CCM wangekaa chini kama watu wazima wakatafakari mwenendo wanaokwenda sio na hautalifikisha taifa la tanzania pahala popote. Viongozi waliopita Mwinyi, mzee wa legacy na falsafa ya upumbavu ( mkapa) na mzee wa matanuzi Kikwete pamoja na kasoro zao nyingi kama viongozi na kama binadamu hawakuwahi kuandika historia hii nyeusi ya watu kuuliwa ovyo, ( ukiacha mauaji ya watu 45 ya wenzetu kutoka pemba mwaka 2001), hawakuingia mkenge. Lkn utawala huu umekuwa kama kichaa aliyepewa rungu la chuma lenye umeme na sumu. Ni aibu kwa tanzania kuingia ktk hali hii. Ndy, pengine best practice ktk leadership huwa inaigwa lakni best practice iliyo nzuri na inayoipleka nchi sehmu nengine ya upendo, umoja, amani na mshikamano wa watanzania ndiyo inayotakiwa kuigwa na kutumika. Sio kuiga leadership style ya akina kagame, mseveni, na burundi inayogawa na kubomoa misingi ya utaifa.

Tunaipenda tanzania yetu lkni kwa mwendo huu , tunauunda raia ambao watapoteza uzalendo na kinachopandwa na kuoteshwa leo tutavuna mavuno mabaya miaka ijayo. Trust me. Tusitafute mchawi. wachawi ni watawala na chama kinachosimamia serikali. Tukumbuke kuwa kesho iliyo nzuri na yenye matumaini hujengwa leo.

Narudi Zimbabwe.
 
Chuki inayojengwa kwa sasa mwisho wake ni mbaya sana ,..
 
AU" YA PILI.

Viongozi wa Taasisi hizo watangaze sasa rasmi kurejesha vuguvugu la UKUTA. hii ni Moja ya 'AU' ngumu, yenye hatari nyingi lakini yenye manufaa makubwa sana. Wataumia watu, watakufa lakini nafikiri baada ya hapo mambo yatakuwa sawa. UKUTA ni muhimu sasa kuliko hata septemba mosi ya 2016. UMOJA WA KUPAMBANA NA UDIKTETA..... Simama, tuhesabiwe.

"AU" YA TATU
Endeleeni na ubunge wenu, lakini ndani ya UKAWA na ikiwezekana na wengine wenye kuwaunga mkono, endelezeni 'harakati' za kuitaka katiba Mpya kwa machozi, jasho na damu. Katiba yenye kutambua muundo Mpya wa tume ya uchaguzi, yenye sheria Mpya ya uchaguzi na kanuni zake. Hii ni kabla ya 2019. Hii pia Kuna kupoteza UHAI na kupata majeraha. Lakini ni bora.


Hakika hii ya tatu nimeipanda sana hasa ahpo kwenye UKAWA,
Kammanda Mbowe,na CDM yako yooote, NCCR Mageuzi, NRA, TADEA, CUF na wengine weeengi wanaojiita wapinzani, haki ya MUNGU nnayemwabudu kila kukicha nawaambia msipoacha makandokando yeni na kusimaia UKAWA kwa nguvu zoti mtabaku kua kuti kavu karibu na moto uwakao.

Muda ufike sasa muwe Kitu kimoja, kiongozi mmoja anayekubalka na wote bila unafiki, kamati moja yenye viongozo wanaotambuana, hapo hakika ccm LAZIMA MUWAKALISHE. Siitaji sias ila ukewli ndo huu.

Narudia tena, Bila UKAWA upinzani Tanzania ni sawa na tela ambalo kawaida haliwezi kuvuta gari.
 
Back
Top Bottom