Setuba Noel
JF-Expert Member
- Mar 9, 2012
- 426
- 210
Hao watu wamefariki, safari yao ya duniani imeisha mengine anayajua Mungu huko mbele ya safari. Lakini huku bado tuna vimbelembele mara maaskofu mara wachungaji wanaotaka kutudanganya kuwa hawa walikuwa wakristo sana, wa kuigwa! Ya kweli haya jamani au ni unafiki tu? Mtu aliyekufa katika mazingira ya ulevi na ugomvi na mtu anayedaiwa ni mpenzi (si mke) wake, ameishi ukristo gani? Au mwenye wake wawili anafuata ukristo gani? Au mtu akishakuwa maarufu ndiyo basi maaskofu wanamwona ni 'kete' ya kujipandishia chati? Tukubaliane kuwa hawa watu walikuwa maarufu na wazuri kwa vigezo vya mambo yaliyowapa umaarufu, ambayo hayawafutii mifano ya kupinga ukristo waliyoonesha. Tuwasifu kwa waliyotufurahisha nayo na si kwa kutumia ukristo maana hawakuwa mabalozi wa ukristo hawa. Nimemwona Kardinali Pengo akimsifia Sokoine kuhusu uimara na umakini wa imani ya kikristo, nikashangaa sana. Najua marehemu Sokoine alizingatia imani yake ya kimasai na hata akawa na wake wawili kwa mujibu wa mila zake, hilo ni sawa na ni sahihi sana kwa mujibu wa mila zake, lakini ni tofauti na imani ya kikristo. Tumpongeze kwa msimamo wake wa kisiasa, wa dini tuuache maana hakuifuata hivyo. La marehemu Kanumba nililiona na kulisikia siku ya ibada ya mazishi iliyoongozwa na yule askofu wa AIC. Jamani sifa za uongo hazimpeleki mtu mbinguni. Kanumba anazo sifa zake za kutosha zinazotokana na kazi zake za usanii, hizo nyingine za kumtungia baada ya kifo acheni jamani zitawapotosha wakristo wengine wanaojitahidi kufuata imani ya kikristo.