Tuache siasa ,tuchukue jembe tukalime

Tabutupu

JF-Expert Member
Nov 26, 2010
13,108
18,325
Wakati wenzetu wanajadili mambo ya msingi jinsi ya kuboresha uchumi , sisi tumekomaa na siasa,siasa si ugali, afrika mashariki hakijaeleweka lakini tumesahau na kuanza kulumbana katk mambo ambayo yamejaa ubinafsi na chuki binafsi.

Japo ndivyo tulivyo pengine lakini sitaki uniambie kuwa huo ndio uwezo pekee tulio pewa watanzania. Sitaki unieleze propaganga na uzoefu ambao huna,nahitaji point za msingi na zenye weledi ili kupata suluhu la matatizo yanayo ikumba tanzania.

Leo tunazungumzia reli ya kati kwa kuwa kenya wamedhamilia kwa dhati kabisa kuwa kiongozi wa uchumi ktk ukanda huu. Tutafanya mambo kwa kuogopa kuachwa nyuma hadi lini.

Usiniambie hii ni serikali ya kijamaa wala serikali iliyo jaa wajinga, najua wana akili timamu, lakini kwanini tuendeshe nchi kama maisha ya kuku asiye juu kesho atakula nini ? Kama unabisha nieleze kwa vigezo vilivyo dhibitika.

Ili tanzania iwe nchi yenye watu wenye maisha bora haihitaji wapiga kelele majukwani, tena wanao taka mara nyingi kuzuia mvua ambayo tayari inanyesha.

Ngoja nimepata tharula narudi......
 
Back
Top Bottom