Tuache siasa, sukari ina madhara makubwa kiafya, iendelee kupanda bei

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,100
Wanabodi, Sukari inapopanda bei ni jambo la heri kwa upande wa kiafya, hii sukari ya madukani au artificial ina madhara makubwa sana kiafya.

Watu ni wagonjwa wa kisukari lakini kutokana na uraibu wa vitu vyenye sukari kuacha inakuwa ngumu.

Leo hii magonjwa yasiyoambukiza kama presha na kisukari ni Janga la kitaifa. Serikali ilijaribu kuanzisha mazoezi sio kwa kupenda bali gharama za tiba kwa magonjwa haya zimeongezeka mara dufu.

Tusiendekeze kila kitu tunachopika kujaza sukari, Tujifunze kupunguza baadhi ya vitu.

Ni mambo ya kusikitisha familia ya watu wanne au watatu wanamaliza mfuko wa sukari kwa siku moja kupikia keki, maandazi na kunywa chai, hii familia itakuwa na afya?

Wakati huu sukari inapopanda bei tushukuru izidi kupanda bei zaidi, Mazoezi watu hawafanyi kupunguza kiasi cha sukari mwilini bali wanahitaji sukari iongezeke mwilini.

Wale watu wa kati na wa chini wanaotumia bima za afya ya Taifa, Kuna madawa ya haya magonjwa yameondolewa kwenye listi inakupasa ujinunulie mwenyewe.

Chukua hatua, chukua tahadhari, Jikinge na magonjwa yasiyoambukiza kisukari na Presha.

Povu linaruhusiwa kwa watu wenye uraibu na sukari bila sukari wao hawawezi kuishi.
 
Sema ina madhara kwa wenye matatizo ya kiafya. Unadhani kwamba watu wameanza kutumia sukari katika awamu hii ya tano?
Watu walitumia hadi sukari gulu kwa taarifa yako.
Kuna muda huwa mnaandika vichekesho hapa JF

Je, bodaboda na bajaji zilikuwepo wakati wa kutumia sukari gulu? au watu walikula na kutoa jasho kwa kutembea kwa miguu hivyo wali weka mizania sawa ya afya

Uzi unaongelea sukari ina madhara makubwa kiafya wewe unaongelea wenye matatizo kiafya, Hayo matatizo kiafya ya kisukari unajua wameyatoa kwenye vitu vinavyotengenezwa na sukari

Ugonjwa wa kisukari ni tatizo, Hao waliokula sukari guru walitembea kwa miguu hakukuwa na boda boda au bajaji
 
Aliekuambia kisukari kinasababishwa na ulaji wa sukari pekee ni nani?
Kajisomee vyakula vinavyochangia kisukari pamoja na sababu zingine za mfumo wa maisha.
Wewe umesoma uzi vizuri na kuelewa

Umeambiwa artificial sugar ina madhara zaidi, kuna vitu vingi vinasababisha kisukari ikiwemo vitu vya wanga kama ugali mweupe

Sasa ulitaka mleta uzi ajadili mambo ya darasani hapa, Haya ni Madhara ya elimu za shule za kata kila wakati mnakuwa na inferiority complex lazima muingize story za shule

Jadili hoja sio vioja

Je, gharama za matibabu ya kisukari zimeongezeka au hapana?

Je, watu wanafanya mazoezi kupunguza sukari?

Soma uzi vizuri mleta uzi ameandika mengi
 
Haya ndio yale ya "sizitaki mbichi hizi".

Katika vitu vyenye madhara makubwa ni pombe na sigara. Lakini hampigi kelele kuhusu hivyo. Mnakuja kupayuka kuhusu madhara ya sukari.
 
Wewe umesoma uzi vizuri na kuelewa

Umeambiwa artificial sugar ina madhara zaidi, kuna vitu vingi vinasababisha kisukari ikiwemo vitu vya wanga kama ugali mweupe

Sasa ulitaka mleta uzi ajadili mambo ya darasani hapa, Haya ni Madhara ya elimu za shule za kata kila wakati mnakuwa na inferiority complex lazima muingize story za shule

Jadili hoja sio vioja

Je gharama za matibabu ya kisukari zimeongezeka au hapana?

Je watu wanafanya mazoezi kupunguza sukari?
Wahusika watafute mbinu ya kudumu kukabiliana na tatizo, haiwezekani miaka nenda rudi issue ni sukari tu, sokoine kahangaika na sukari mpaka sasa sukari
Soma uzi vizuri mleta uzi ameandika mengi

Sikujibu mpaka niende kusoma shule ya kata maana mpaka sasa elimu yangu ya darasa la nne la mkoloni hainiambii kisukari kinaletwa na ulaji wa sukari bali kufeli kwa mfumo na ulaji mbaya hasa vyakula vya wanga.

Pia uwepo wa magonjwa ya kisukari sio justification ya kufanya sukari isipatikane na wananchi wateseke.
 
Sukari Tanzania INA nini lakini?
Mbona tatizo kila siku ni sukari?
Wasomi nao wafanye research kujua shida
 
Sikujibu mpaka niende kusoma shule ya kata maana mpaka sasa elimu yangu ya darasa la nne la mkoloni hainiambii kisukari kinaletwa na ulaji wa sukari bali kufeli kwa mfumo na ulaji mbaya hasa vyakula vya wanga.
Pia uwepo wa magonjwa ya kisukari sio justification ya kufanya sukari isipatikane na wananchi wateseke.
Ni vyema ukaficha ujinga wako kiongozi, Hujaelewa mleta uzi anaongelea kitu gani?

Wewe umeshikilia notes zako za kuclaim darasani, Hebu Jaribu kufikiri nje ya notes ulizojibia mitihani

Item za mleta mada ni kama nne hivi
Anaongelea artificial sugar yaani sukari za viwandani

Anaongelea gharama za matibabu ya kisukari kwenye bima ya afya

Anaongelea watu hawafanyi mazoezi you kukabiliana na kisukari

Wewe unawashwa washwa na kuanza kuandika vitu vingine vinavyosababisha kisukari, kweli vipo vingi sana na ulishajibiwa, Hapa Jadiri hoja

Nina mashaka na uwezo wako wa kufikiri, Yawezekana umesoma na unavyeti lakini capacity yako ya kuchuja mambo ni zero
 
Sikujibu mpaka niende kusoma shule ya kata maana mpaka sasa elimu yangu ya darasa la nne la mkoloni hainiambii kisukari kinaletwa na ulaji wa sukari bali kufeli kwa mfumo na ulaji mbaya hasa vyakula vya wanga.
Pia uwepo wa magonjwa ya kisukari sio justification ya kufanya sukari isipatikane na wananchi wateseke.

Achana na huyu graduate wa St.Kayumba schools na VodaFasta!
Ndicho alichofundishwa kuwa ugonjwa wa KISUKARI unatokana na kunywa/kuramba Sukari!
Kama ingelikuwa ni hivo kila mtu Duniani angelikuwa na KISUKARI...!!!
 
Ndio imesha panda , japo wanaostahili kuishusha wanajitahidi kila hali kuishusha lakini bado imegoma hapo juu
 
Ni vyema ukaficha ujinga wako kiongozi, Hujaelewa mleta uzi anaongelea kitu gani?

Wewe umeshikilia notes zako za kuclaim darasani, Hebu Jaribu kufikiri nje ya notes ulizojibia mitihani

Item za mleta mada ni kama nne hivi
Anaongelea artificial sugar yaani sukari za viwandani

Anaongelea gharama za matibabu ya kisukari kwenye bima ya afya...
Usinilazimishe nijadili hoja zote wakati nimechagua kujibia moja ya sukari kupanda bei ni sahihi kwakuwa ina madhara, hii sukari tunayonywea chai inasababisha kisukari ndio upupu uliosoma huko shule?

Hizo hoja zingine sina shaka Nazo, kwahiyo huwa tunatumia sukari ya kuweka kwenye soda kwa matumizi ya kawaida ya majumbani?

Kuna aina kadhaa za sukari kulingana na matumizi nazo zina madhara pia kama ilivyo kwa bidhaa nyingine! Hoja ya sukari ya matumizi ya nyumbani iliyopanda bei kuwa iendelee kupanda eti inaleta kisukari ni haina mashiko.

Otherwise elimu nyingine ya kuhusu mazoezi na ulaji wa articifial sugar inaweza make sense.
Elimu yangu ya darasa la nne sio ya kubeza .

Shule zikifunguliwa nitaenda memkwa nisome secondary
 
Achana na huyu graduate wa St.Kayumba schools na VodaFasta!
Ndicho alichofundishwa kuwa ugonjwa wa KISUKARI unatokana na kunywa/kuramba Sukari!
Kama ingelikuwa ni hivo kila mtu Duniani angelikuwa na KISUKARI...!!!
Wewe Itakuwa chadema
 
Usinilazimishe nijadili hoja zote wakati nimechagua kujibia moja ya sukari kupanda bei ni sahihi kwakuwa ina madhara, hii sukari tunayonywea chai inasababisha kisukari ndio upupu uliosoma huko shule?
Hizo hoja zingine sina shaka Nazo, kwahiyo huwa tunatumia sukari ya kuweka kwenye soda kwa matumizi ya kawaida ya majumbani?

Kuna aina kadhaa za sukari kulingana na matumizi nazo zina madhara pia kama ilivyo kwa bidhaa nyingine! Hoja ya sukari ya matumizi ya nyumbani iliyopanda bei kuwa iendelee kupanda eti inaleta kisukari ni haina mashiko.
Otherwise elimu nyingine ya kuhusu mazoezi na ulaji wa articifial sugar inaweza make sense.
Elimu yangu ya darasa la nne sio ya kubeza .

Shule zikifunguliwa nitaenda memkwa nisome secondary
Wewe Itakuwa Chadema kila kitu mnapiga

Hapa mlitaka kuchukua point kuwa ccm imepandisha bei sukari

Ahaaa kuitetea Chadema sasa ni kazi kweli kweli

Chadema hii mada imewauma sana, Naona imepiga penyewe
 
Back
Top Bottom