Tuache Siasa, Riba ya Mabenki ya biashara kukopesha Raia ni suala la Vihatarishi na sio maamuzi ya Serikali

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,100
Riba ya Mabenki kukopesha wateja wao sio suala la kisiasa, Huwezi ukasema kuanzia Leo Mabenki ya biashara riba ya kukopesha iwe asilimia kumi 10%

Mabenki kukopesha Raia au wateja wake kinachoangaliwa ni:
1. Vihatarishi (Risk) vinavyoizunguka biashara au kazi ya mteja husika, Biashara au kazi isiyoeleweka yaani tia maji tia maji ni ngumu sana Benki kujilipua kukukopesha kwa riba ndogo kwani hawajui hatima ya pesa zao( Na hizi pesa Bank inakopesha sio zao bali baadhi ya Raia waliozidiwa na pesa na hawana matumizi nazo kwa wakati huo wameamua kuzitupa pesa zao Bank)

Siku waliozidiwa na pesa na kuamua kuziweka Bank wakizihitaji pesa zao hakuna mjadala na Bank, Bank Inatakiwa kuzitoa bila kusingizia hazijarudi kwa kukopesha makapuku kwa riba ndogo

2. Uwezo wa mkopaji kurudisha deni( Creditworthiness of the borrower). Mteja ambaye yupo vizuri na amekamilika ni rahisi kupunguza riba kuliko kapuku asiye na kitu chochote, Kapuku ni ngumu kufahamu matarajio ya biashara au kazi yake ndani ya miaka miwili au mmoja ujao, Hatari iliyopo kwa kapuku ni kubwa kuliko kwa Tajiri,

Wanaosubiri Mabenki kushusha riba kwa Matamko ya kisiasa, Hii kitu kwenye uchumi huria haipo,

Ni bora ukaweka riba kubwa ili pesa yako irudi kwa wingi haraka haraka hasa kwa wafanyabiashara na wafanyakazi tia maji tia maji kuliko ukaweka riba ndogo itakayofanya mrejesho uwe kidogo na kupata hasara kubwa kapuku akishindwa kulipa deni lake

Serikali hata wakashusha riba zao za Bank za biashara kukopa Bank kuu(BoT) yaani landing rate hii haiathiri riba za Mabenki kukopesha Raia zaidi inasaidia Mabenki Kuongeza Deposits(Pesa za kukopesha Raia)

Riba ya mkopo ni Negotiable( Inajadilika) kama tu upo vizuri na unaeleweka mbele za wakopeshaji

Mtu kama Bakhresa au Asas Ltd anaweza kopeshwa na Mabenki dollar za marekani hata kwa riba ya asilimia nne 4% lakini sio wewe Kapuku, Hatari ya kuweka riba ndogo kwa kapuku ni kubwa zaidi

Mtu mwenye Fixed Deposit Bank ni rahisi zaidi kumkopesha pesa, Akishindwa kulipa tayari Bank ina fixed deposit yake kama dhamana, Mtu wa Mtindo huu unaangalia tofauti ya riba uliyompa kwenye fixed deposit na Kuongeza kidogo kwenye mkopo

N. B
Kumbuka Bank ni neno tu, Bank zipo pale kutokana na Pesa za wateja wao walioziweka, Hizo pesa ndio Bank inapata kiburi cha kukopesha Raia, Bila watu kuweka pesa Bank, Hakuna biashara ya Bank za biashara

Ni nani aliyetayari kuweka pesa Bank yaani kuikopesha Bank Halafu baada ya mwaka unaambiwa pesa zako tulimkopesha Mwanaidi Binti CCM hajarudisha, Utawaelewa?

Je watanzania sisi tupo kundi gani la kukopesheka? Level ya kapuku, Level ya kati au Matajiri

Nchi tajiri zinakopeshwa kwa riba ndogo kuliko nchi maskini, Huo ndio uhalisia
 
U
Ebu fafanua, inakuaje BOT wakubali kushusha rates zao kwa ma bank ila bank bado waone kwao hailipi ? Riba za Tz kiukweli ki kubwa sana, utakuta mtu amepigwa riba ya 18 % tena non reducing rate, after 5 yrs huyu ni kama amelipa 90% riba, sasa huu si wizi .
Po sahihi
 
Ebu fafanua, inakuaje BOT wakubali kushusha rates zao kwa ma bank ila bank bado waone kwao hailipi ? Riba za Tz kiukweli ki kubwa sana, utakuta mtu amepigwa riba ya 18 % tena non reducing rate, after 5 yrs huyu ni kama amelipa 90% riba, sasa huu si wizi .
Riba ambayo inaongelewa na BoT ni lending rate, Riba ambayo Bank wanaweza kukopa toka Bank kuu, Hii Riba ipo siku zote kama Monetary policy, BoT wanapotaka Kuongeza liquidity au ukwasi kwenye uchumi wanapunguza Riba ili Mabenki yaweze kukopa zaidi na kuzungusha pesa na kinyume chake wanaongeza Riba pale wanapoona pesa inaweza kusababisha mfumuko wa bei

Wewe mtu binafsi kukopa Bank ya biashara ni tofauti, Lazima ufanyiwe rating kama una vigezo au huna, Hivyo riba za Mabenki kwa Raia ni suala la tahadhari na uwezo wa wakopaji kurudisha deni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Riba ambayo inaongelewa na BoT ni lending rate, Riba ambayo Bank wanaweza kukopa toka Bank kuu, Hii Riba ipo siku zetu kama Monetary policy, BoT wanapotaka Kuongeza liquidity au ukwasi kwenye uchumi wanapunguza Riba ili Mabenki yaweze kukopa zaidi na kuzungusha pesa na kinyume chake wanaongeza Riba pale wanapoona pesa inaweza kusababisha mfumuko wa bei

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa kama hiyo lending rate ya BOT ilikuwa 8% ikapunguzwa hadi 4% au chini zaidi kwa nini haya mabenki na yenyewe yanashindwa kupunguza rate ya kukupesha wateja wao, hatuwezi kushindani na nchi kubwa wakati wafanyabiashara wao wanapata mikopo kwa chini ya 6% tena reducing rate wakati sisi tunapata mikopo kwa 18% tena kwa non reducing rate.
 
Sasa kama hiyo lending rate ya BOT ilikuwa 8% ikapunguzwa hadi 4% au chini zaidi kwa nini haya mabenki na yenyewe yanashindwa kupunguza rate ya kukupesha wateja wao, hatuwezi kushindani na nchi kubwa wakati wafanyabiashara wao wanapata mikopo kwa chini ya 6% tena reducing rate wakati sisi tunapata mikopo kwa 18% tena kwa non reducing rate.
Upo sahihi riba zipo juu sn
 
Sasa kama hiyo lending rate ya BOT ilikuwa 8% ikapunguzwa hadi 4% au chini zaidi kwa nini haya mabenki na yenyewe yanashindwa kupunguza rate ya kukupesha wateja wao, hatuwezi kushindani na nchi kubwa wakati wafanyabiashara wao wanapata mikopo kwa chini ya 6% tena reducing rate wakati sisi tunapata mikopo kwa 18% tena kwa non reducing rate.
Uwezo wako wa kulipa au kurudisha deni( ability to pay back) uko vipi, Pia thamani yetu ya pesa pia baada ya muda fulani( Time value of money)

Nakukopesha Leo million 7,je baada ya miaka mitatu milion7 thamani yake Itakuwa hivyo hivyo au itashuka

Vitu vinavyonunuliwa kwa million 7 mwaka huu 2021 vitaweza kununuliwa kwa milion7 mwaka 2022

ili kufidia thamani ya pesa Isipotee kwa mkopeshaji unafidia kwenye riba pia

Thamani yetu ya pesa haitabiriki pia

Fikiria shs 10 na shs 20 ya Leo hazina thamani tena hata Pipi ya mtoto huwezi Nunua, Miaka 10 iliyopita Pipi zilikuwepo za shs 10 na 20.Kufidia huu utofauti unaongeza kwenye riba pia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Riba ambayo inaongelewa na BoT ni lending rate, Riba ambayo Bank wanaweza kukopa toka Bank kuu, Hii Riba ipo siku zote kama Monetary policy, BoT wanapotaka Kuongeza liquidity au ukwasi kwenye uchumi wanapunguza Riba ili Mabenki yaweze kukopa zaidi na kuzungusha pesa na kinyume chake wanaongeza Riba pale wanapoona pesa inaweza kusababisha mfumuko wa bei

Wewe mtu binafsi kukopa Bank ya biashara ni tofauti, Lazima ufanyiwe rating kama una vigezo au huna, Hivyo riba za Mabenki kwa Raia ni suala la tahadhari na uwezo wa wakopaji kurudisha deni

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa maana hiyo mtu mwenye biashara ya uhakika Kuna benk inaweza mkopesha kwa riba ya let's say 6%?
 
Mpaka sasa Mimi nawafahamu waliokopa kwa 9% na 10%.kwa 6% bado sina data kwa sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
Inaonekana wewe ni mfanyakazi wa bank hapa Tz, je serikali kushusha hiyo lending rate haiwapi ahueni yoyote kwenu mabank? Inflation Tz imekuwa stable na chini at 3-4% kwa miaka mitano sasa, lending rate government imeshusha mbona hakuna ahueni yoyote sasa? Nchi nyingine zinawezaji commercial banks zao kutoa mikopo kwa 6% na chini ya hapo tena bila longo longo yoyote.
 
Riba ya Mabenki kukopesha wateja wao sio suala la kisiasa, Huwezi ukasema kuanzia Leo Mabenki ya biashara riba ya kukopesha iwe asilimia kumi 10%

Mabenki kukopesha Raia au wateja wake kinachoangaliwa ni:
1. Vihatarishi (Risk) vinavyoizunguka biashara au kazi ya mteja husika, Biashara au kazi isiyoeleweka yaani tia maji tia maji ni ngumu sana Benki kujilipua kukukopesha kwa riba ndogo kwani hawajui hatima ya pesa zao( Na hizi pesa Bank inakopesha sio zao bali baadhi ya Raia waliozidiwa na pesa na hawana matumizi nazo kwa wakati huo wameamua kuzitupa pesa zao Bank)

Siku waliozidiwa na pesa na kuamua kuziweka Bank wakizihitaji pesa zao hakuna mjadala na Bank, Bank Inatakiwa kuzitoa bila kusingizia hazijarudi kwa kukopesha makapuku kwa riba ndogo

2. Uwezo wa mkopaji kurudisha deni( Creditworthiness of the borrower). Mteja ambaye yupo vizuri na amekamilika ni rahisi kupunguza riba kuliko kapuku asiye na kitu chochote, Kapuku ni ngumu kufahamu matarajio ya biashara au kazi yake ndani ya miaka miwili au mmoja ujao, Hatari iliyopo kwa kapuku ni kubwa kuliko kwa Tajiri,

Wanaosubiri Mabenki kushusha riba kwa Matamko ya kisiasa, Hii kitu kwenye uchumi huria haipo,

Ni bora ukaweka riba kubwa ili pesa yako irudi kwa wingi haraka haraka hasa kwa wafanyabiashara na wafanyakazi tia maji tia maji kuliko ukaweka riba ndogo itakayofanya mrejesho uwe kidogo na kupata hasara kubwa kapuku akishindwa kulipa deni lake

Serikali hata wakashusha riba zao za Bank za biashara kukopa Bank kuu(BoT) yaani landing rate hii haiathiri riba za Mabenki kukopesha Raia zaidi inasaidia Mabenki Kuongeza Deposits(Pesa za kukopesha Raia)

Riba ya mkopo ni Negotiable( Inajadilika) kama tu upo vizuri na unaeleweka mbele za wakopeshaji

Mtu kama Bakhresa au Asas Ltd anaweza kopeshwa na Mabenki dollar za marekani hata kwa riba ya asilimia nne 4% lakini sio wewe Kapuku, Hatari ya kuweka riba ndogo kwa kapuku ni kubwa zaidi

Mtu mwenye Fixed Deposit Bank ni rahisi zaidi kumkopesha pesa, Akishindwa kulipa tayari Bank ina fixed deposit yake kama dhamana, Mtu wa Mtindo huu unaangalia tofauti ya riba uliyompa kwenye fixed deposit na Kuongeza kidogo kwenye mkopo

N. B
Kumbuka Bank ni neno tu, Bank zipo pale kutokana na Pesa za wateja wao walioziweka, Hizo pesa ndio Bank inapata kiburi cha kukopesha Raia, Bila watu kuweka pesa Bank, Hakuna biashara ya Bank za biashara

Ni nani aliyetayari kuweka pesa Bank yaani kuikopesha Bank Halafu baada ya mwaka unaambiwa pesa zako tulimkopesha Mwanaidi Binti CCM hajarudisha, Utawaelewa?

Je watanzania sisi tupo kundi gani la kukopesheka? Level ya kapuku, Level ya kati au Matajiri

Nchi tajiri zinakopeshwa kwa riba ndogo kuliko nchi maskini, Huo ndio uhalisia
Kuna Jambo ambalo muandika mada hulielewi hapa,
BOT kwenye hii policy mpya anatoa punguzo la riba kwa mabenki yatayokopa BOT kwa kukubaliana na hii policy maalum.Mabenki ambayo yatakubaliana na Policy hii maalum ya BOT yatapaswa kisheria kushusha riba chini ya 10% kwa lazima.Benki zitakazokubaliana na masharti ya BOT watapewa motisha mbalimbali ikiwemo kupunguziwa reserve ratio requirement and etc.Benki itakapokubaliana na kupokea hii financing kutoka kwenye hiyo basket ya 1Trillion itafungwa kisheria automatically kushusha riba kwa lazima kwendana na requirement za policy.
 
Bank gan hapa Tanzania inakopesha kwa 9-10% mkuu?
Tz mizinguo sana, eti hiyo ni kwa special customers walio na minimum risks ya ku default the likes of Bakhresa na Asas. Serikali inabidi itafute solution ya mikopo iwe kwa riba rafiki, riba za Tz ni wizi mtupu, mtu anapewa mkopo riba 18% halafu non reducing rate, after 5yrs analipa 90% ya mkopo kama riba so kama alichukua 100m, atalipa riba 90m, jumla aliyolipa 190m, huu kama sio wizi ni nini kwa kweli ?
 
Inaonekana wewe ni mfanyakazi wa bank hapa Tz, je serikali kushusha hiyo lending rate haiwapi ahueni yoyote kwenu mabank? Inflation Tz imekuwa stable na chini at 3-4% kwa miaka mitano sasa, lending rate government imeshusha mbona hakuna ahueni yoyote sasa? Nchi nyingine zinawezaji commercial banks zao kutoa mikopo kwa 6% na chini ya hapo tena bila longo longo yoyote.
Ukweli ni kwamba-Bank zimepewa option ya kukubaliana na hiyo policy mpya au lah.
 
Riba ambayo inaongelewa na BoT ni lending rate, Riba ambayo Bank wanaweza kukopa toka Bank kuu, Hii Riba ipo siku zote kama Monetary policy, BoT wanapotaka Kuongeza liquidity au ukwasi kwenye uchumi wanapunguza Riba ili Mabenki yaweze kukopa zaidi na kuzungusha pesa na kinyume chake wanaongeza Riba pale wanapoona pesa inaweza kusababisha mfumuko wa bei

Wewe mtu binafsi kukopa Bank ya biashara ni tofauti, Lazima ufanyiwe rating kama una vigezo au huna, Hivyo riba za Mabenki kwa Raia ni suala la tahadhari na uwezo wa wakopaji kurudisha deni

Sent using Jamii Forums mobile app
Policy umeisoma vizuri lakini na kuielewa? manake tusijekuwa tunapiga tu ndaro hapa
 
Kuna Jambo ambalo muandika mada hulielewi hapa,
BOT kwenye hii policy mpya anatoa punguzo la riba kwa mabenki yatayokopa BOT kwa kukubaliana na hii policy maalum.Mabenki ambayo yatakubaliana na Policy hii maalum ya BOT yatapaswa kisheria kushusha riba chini ya 10% kwa lazima.Benki zitakazokubaliana na masharti ya BOT watapewa motisha mbalimbali ikiwemo kupunguziwa reserve ratio requirement and etc.Benki itakapokubaliana na kupokea hii financing kutoka kwenye hiyo basket ya 1Trillion itafungwa kisheria automatically kushusha riba kwa lazima kwendana na requirement za policy.
Haitafanya kazi hilo unaloliongea labda Serikali iamue kufanya biashara

Je Chanzo kikubwa cha pesa za Bank ni kitu gani?

Chanzo kikuu cha pesa Bank ni dhamana za wateja yaani Deposits

Hawa wateja wakubwa hawaweki pesa zao Benki bure wanahitaji riba pia kutoka kwenye pesa zao

Itawezaje Bank kutoa riba kwenye deposits kwa asilimia 11 %mpaka 16% Halafu wao wanunue hati fungani za muda mfupi wapate asilimia chini 7%.Hii Itakuwa biashara kichaa

Policy zipo, Yes lakini ni ngumu kufanya kazi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bank gan hapa Tanzania inakopesha kwa 9-10% mkuu?
Hii ni negotiable, unakaa mezani wanaangalia vigezo, Hakuna Bank utaenda sasa kichwa kichwa watakukopesha kwa asilimia 9%au 10% Tanzania

Hiyo riba kwanza ni hasara kwa Bank wanafanya hivyo kwa Special Persons

Hakuna Bank hiyo kwa sasa Tanzania, Hiyo riba ni Personal ya majadiliano sio kwa kila mtu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haitafanya kazi hilo unaloliongea labda Serikali iamue kufanya biashara

Je Chanzo kikubwa cha pesa za Bank ni kitu gani?

Chanzo kikuu cha pesa Bank ni dhamana za wateja yaani Deposits

Hawa wateja wakubwa hawaweki pesa zao Benki bure wanahitaji riba pia kutoka kwenye pesa zao

Itawezaje Bank kutoa riba kwenye deposits kwa asilimia 11 %mpaka 16% Halafu wao wanunue hati fungani za muda mfupi wapate asilimia chini 7%.Hii Itakuwa biashara kichaa

Policy zipo, Yes lakini ni ngumu kufanya kazi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu usiongelee porojo-Be specific kwendana na policy requirements manake naona unazunguka zunguka tu,Hapa tunaongelea legal issues.
 
Back
Top Bottom