Tuache siasa kwenye matibabu ya wazee

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,239
4,464
Nimekuwa nashangaa sana kuona wanasiasa wanajigamba majukwaani kwa utoaji wa vitambulisho vya Wazee kama utambulisho wa kupata huduma bure za matibabu pale waendapo hospitali za serikali. Ni wazo zuri lakini sio kwa namna hiyo.

Duniani kote, afya bure haijawahi kufanikiwa. Ukipewa kitambulisho cha kupata huduma ya Afya bure, nani atalipia gharama zako? Je, kuna mtu yeyote anachangangia kwenye hiyo pool ya wazee? Tuseme ukweli, Serikali haijakuwa mwaminifu kupeleka pesa kwenye hospitali zake za umma ambazo yamkini pamoja na kuhudumia hawa wazee wanaopewa vitambulisho zingeweza ku sustain service.

Afya bure bila ya mtu kuchangia gharama za yule anayehudumiwa bure, huishia kuua huduma nzima ya afya; na hivyo kuwaathiri hata wale wanaoendesha huduma za Afya kupitia cash au mifuko ya bima.

Kama serikali inaweza, ikawafungulie hawa wazee bima ya Afya. Tena sio zile CHF za kulipia elfu 5 kwa mwaka. Na ikiwezekana waachane kabisa na huo mpango wa pensheni za uzeeni bali wawasajili hawa wazee wetu kwenye mifuko ya bima.

Kutoa kitambulisho cha kupata huduma za afya bure bila mtu kuchangia, ni sawa na kumkamua maziwa ng'ombe bila kumpa majani.

e4b36628c2006e60c75d174f939c84df.jpg
 
Hakuna cha bure hapo bora tulipe tu kama bado hawajajipanga.

Nakumbuka nilimpeleka bibi yangu hospital ya serikali, alianguka, daktar alimuona buree, X-ray alipimwa buree, twende Kwenye Dawa, aliandikiwa Dawa za pressure, na mkono wafunge hogo hospital Haina vifaa ilibidi twende nje Kwenye maduka ya Dawa kutafuta ilinitoka sh 65,000 cash .

Hii bure wanayoisemea hapo ni bure ya nini Kama vifaa havitoshi.
 
sasa kama una escrow,kivuko kibovu,ndege inadakwa canada,epa,richmond,meremeta meli ya samaki na makinikia utaweza kufanikisha hayo hapo bado hujahonga wabunge wapitishe miswada mibovu ya kuipa upendeleo serikali.
 
sasa kama una escrow,kivuko kibovu,ndege inadakwa canada,epa,richmond,meremeta meli ya samaki na makinikia utaweza kufanikisha hayo hapo bado hujahonga wabunge wapitishe miswada mibovu ya kuipa upendeleo serikali.
Hahahaha
 
Back
Top Bottom