Nimekuwa mwanachama wa JF siku nyingi kidogo. Uzuri wa JF ni kwamba wanachama wengi wamesoma angalao kufika form IV. Huwa kila siku nasoma makala na si mimi tu hata maprofesa na wasomi wengi ni wanachama. Sasa naomba ili JF iendelee kuwa blog makini tujaribu kujadili mambo makubwa ya kulijenga taifa. Tz tuna matatizo ya rushwa, umaskini, katiba, mbovu nk. Tujikite huko kuliko kujadili mambo madogo kama vile baraza la mawaziri lina wakristo na waislamu wangapi nk. Kujadili mambo madogo haya ni kuonyesha uchanga wa fikra. Ni ushauri tu lakini