Inasikitisha kuona baadhi ya watu wakibedha uongozi wa Baba wa Taifa Hayati Mwl. J.k. Nyerere kwamba alikuwa mbaguzi kwenye suala/tasinia ya elimu.
Binafsi, naona ni kumvunjia hadhi na heshima hayati Mwl. Nyerere kwa mazuri aliyoyafanya kwa watanganyika.
Tukumbuke kwamba kabla ya uhuru wa Tanganyika na baada ya uhuru sekta ya elimu ilikuwa ya kibaguzi; ililenga makundi mahususi ya watu. Ilizingatia udini na matabaka yaliyokuwepo wakati huo.
Tabaka la udini lilikuwa bayana kabisa. Madhehebu ya Kikatoliki kupitia mashirika yake mengi ndio walikuwa na shule nyingi za msingi, sekondari na hata vyuo vya ufundi.
Madhehebu mengine kama waluteli na waanglikana hakuwa nyuma. Kundi jingine ilikuwa ni wahindi ambao walikuwa na shule chache maeneo ya mijini.
Wajerumani walipoanza kuitawala Tanganyika miaka ya 1880, gavana wao wakati huo Von Soden alitoa ruzuku kwa shule za misheni. Lengo ilikuwa kupata watu wachache watakao saidia utawala katika kazi zao za kila siku.
Hadi kufikia 1911 serikali ya kikolloni ilikuwa na shule 83 na wamishenari walikuwa na shule takribani 918. Shule za serikali zilikuwa na wanafunzi 3,000 na missheni wanafunzi 65,000. Waingereza nao baadaye kuanzia 1918 wakaendeleza ya wajerumani kusaidia shule za misheni.
Hawa wakawa waandalizi wa kuwaandaa watanganyika kupata uhuru wao. Wakaanza, kama wajerumani, kuwaandaa watanganyika wachache kushika madaraka ya nchi. Na ilikuwa ni kupitia elimu ya kimaghariibi tu kwamba watanganyika wangejitawala.
Kwa mantiki hiyo, ni wazi kuwa watawala waliondaliwa na wakoloni wangetokea maeneo yale ambayo wamishenari wa kikristo walishajijenga na kuanzisha shule.
Hapa ina maanisha kwamba watu kutoka Kilimanjaro, Arusha, Kagera, Mara, Ruvuma na Mbeya ndio waliokuwa wakipewa nafasi ya kuwa watawala wa Tanganyika huru.
Baada ya uhuru mfumo huu ulionekana wazi ni wa kibaguzi. Mathalan, wamishenari wengi walijikita katika maeneo muhimu kiuchumi. Wakajenga makanisa na shule mikoa ya kaskazini, Kilimanjaro,Arusha.
Kanda ya ziwa Kagera. Na kusini wakajenga Iringa, Mbeya,Ruvuma nk. Maeneo mengi ya pwani hawakujihusisha sana. Huko walibaguliwa na hawakupendwa sana na waislamu ambao walikuwa wengi maeneo hayo.
Kwa hiyo, baada ya uhuru Mwl. Nyerere akaona ipo haja ya kufuta mfumo huo wa kibaguzi kielimu. Kupitia sera ya ujamaa na kujitegemea (1967)Mwl. Nyerere akataifisha shule na vyuo vyote vilivyokuwa vya wamishenari.
Hapa akatoa haki kwa watanzania wote kupata elimu sawa. Kufikia mwaka 1977 Mwl. Nyerere akatangaza Elimu Kwa Wote (UPE) ndipo kila mkoa, kila wilaya, kila tarafa, kila kata kukawa na shule za msingi. Watoto waliofikia umri
Binafsi, naona ni kumvunjia hadhi na heshima hayati Mwl. Nyerere kwa mazuri aliyoyafanya kwa watanganyika.
Tukumbuke kwamba kabla ya uhuru wa Tanganyika na baada ya uhuru sekta ya elimu ilikuwa ya kibaguzi; ililenga makundi mahususi ya watu. Ilizingatia udini na matabaka yaliyokuwepo wakati huo.
Tabaka la udini lilikuwa bayana kabisa. Madhehebu ya Kikatoliki kupitia mashirika yake mengi ndio walikuwa na shule nyingi za msingi, sekondari na hata vyuo vya ufundi.
Madhehebu mengine kama waluteli na waanglikana hakuwa nyuma. Kundi jingine ilikuwa ni wahindi ambao walikuwa na shule chache maeneo ya mijini.
Wajerumani walipoanza kuitawala Tanganyika miaka ya 1880, gavana wao wakati huo Von Soden alitoa ruzuku kwa shule za misheni. Lengo ilikuwa kupata watu wachache watakao saidia utawala katika kazi zao za kila siku.
Hadi kufikia 1911 serikali ya kikolloni ilikuwa na shule 83 na wamishenari walikuwa na shule takribani 918. Shule za serikali zilikuwa na wanafunzi 3,000 na missheni wanafunzi 65,000. Waingereza nao baadaye kuanzia 1918 wakaendeleza ya wajerumani kusaidia shule za misheni.
Hawa wakawa waandalizi wa kuwaandaa watanganyika kupata uhuru wao. Wakaanza, kama wajerumani, kuwaandaa watanganyika wachache kushika madaraka ya nchi. Na ilikuwa ni kupitia elimu ya kimaghariibi tu kwamba watanganyika wangejitawala.
Kwa mantiki hiyo, ni wazi kuwa watawala waliondaliwa na wakoloni wangetokea maeneo yale ambayo wamishenari wa kikristo walishajijenga na kuanzisha shule.
Hapa ina maanisha kwamba watu kutoka Kilimanjaro, Arusha, Kagera, Mara, Ruvuma na Mbeya ndio waliokuwa wakipewa nafasi ya kuwa watawala wa Tanganyika huru.
Baada ya uhuru mfumo huu ulionekana wazi ni wa kibaguzi. Mathalan, wamishenari wengi walijikita katika maeneo muhimu kiuchumi. Wakajenga makanisa na shule mikoa ya kaskazini, Kilimanjaro,Arusha.
Kanda ya ziwa Kagera. Na kusini wakajenga Iringa, Mbeya,Ruvuma nk. Maeneo mengi ya pwani hawakujihusisha sana. Huko walibaguliwa na hawakupendwa sana na waislamu ambao walikuwa wengi maeneo hayo.
Kwa hiyo, baada ya uhuru Mwl. Nyerere akaona ipo haja ya kufuta mfumo huo wa kibaguzi kielimu. Kupitia sera ya ujamaa na kujitegemea (1967)Mwl. Nyerere akataifisha shule na vyuo vyote vilivyokuwa vya wamishenari.
Hapa akatoa haki kwa watanzania wote kupata elimu sawa. Kufikia mwaka 1977 Mwl. Nyerere akatangaza Elimu Kwa Wote (UPE) ndipo kila mkoa, kila wilaya, kila tarafa, kila kata kukawa na shule za msingi. Watoto waliofikia umri