Tuache kabisa kuchezea sheria za nchi kukomoana. Ugaidi si jambo dogo

Prof Koboko

JF-Expert Member
Aug 15, 2020
350
2,549
Wasalaam wanajukwaa,

Naweza kudiriki kusema kwamba kuna mahali kama taifa tumeshiba sana tuna la amani na ulivyo na amani tuliyonayo ndiyo maana kikundi kidogo cha watu wachache wasiofikiria mbali hakioni aibu kumbambikia kiongozi mkubwa kesi mbaya ya ugaidi ilimradi tu akose dhamana akae mahabusu asifanye kile ambacho kinawakera wao. Ubinadamu imetoweka kabisa, huruma haipo tena mtu haoni taabu kumtesa mwenzake ili yeye atulie afanye atakacho.

Hii haiingii akilini wala haieleweki kwa mtu ambaye alishawahi kuhudhuria moja ya mahakama nchini Kenya kusikiliza kesi za ugaidi zinazowakabili watuhumiwa walioshukiwa kua ni Al-shaabab agents, hakika angaweza kuona kituko kinachofanyika nchini mwetu.Ugaidi anaojiapisha kwa Mungu IGP wa polisi ni wa kufadhiliwa kwa shilingi 600,000? Ugaidi ni wa kupanga kwa bastola yenye risasi 3? Yaani gaidi upangwe kwa Sabaya ambaye ana kesi za uporaji mahakamani hivi sasa?

IGP umeliharibu sana jeshi la polisi wala hakuna mtu atakayekuamini tena wewe, ndiye IGP pekee ambaye jeshi la polisi limetuhumiwa na mkuu wa nchi hadharani kua na kesi nyingi za kubambikizia. Hii maana yake IGP hana weledi wowote wala hofu ya Mungu hana anafanya mambo kuridhisha waliomteua.

Tuache kuchezea sheria za nchi kukomoana na kutesa watu ikiwa tumepewa mamlaka la kulinda raia na mali zao, tuheshimu mhimili wa mahakama kwa kupeleka kesi zenye uhalisia ili kuepusha usumbufu unaojitokeza matumizi ya rasilimali za umma bila sababu maana kuna mambo mengi ya kufanya ya kulijenga taifa.Tunajenga chuki itakayolitafuna taifa miaka nenda rudi kwa sababu ya tamaa za madaraka kwa watu wachache.

Mwalimu Nyerere aliijenga nchi hii kwa gharama kubwa kwa misingi ya utu wa kuheshimiana, kutanguliza busara na hekima. Hakujenga kukomoana na wala hakuliandaa taifa la watu wanaobambikiza watu kesi kwa tuhuma za kutengeneza. Tuheshimu sheria za nchi ili tuweze kujenga taifa imara na lenye nguvu kubwa.

Huwezi kujiaminisha kua wewe ndio wewe kwenye taifaa watu milion zaidi ya 60 wanaofikiri tofauti, siku wakikuchoka utaelewa haya nisemayo.
 
Hii si kesi ya kwanza ya ugaidi, nyingine ya aina hii iliwahi kupangwa miaka michache iliyopita nayo ilikuwa na madai ya Manka kupanga kuchoma vituo vya mafuta Arusha! Bahati nzuri ilionekana ni ugaidi wa kiwango cha igizo la kwenye shule ya msingi.
 
Watanzania wengi ni watumwa wa kazi zetu, ndio maana WE CAN DO ANYTHING ili kulinda vibarua hata kama tunajivunjia heshima zetu na kuonekana watu wa hovyo. Mahita alileta visu vya CUF, Kova akalutea Mkenya aliyemteka Ulimboka, Sirro akaleta picha za tecno akisema CCTV; ujinga hauishi
 
iweke vizuri mkuu isomeke kwa usahihi neno kwa neno, mkato kwa mkato, nukta kwa nukta.

Mfano hapo ulipoandika 'tuna' nadhani ulitaka kuandika 'tunda'.
 
 
Subirini Mahakama itaamua, acheni kiherehere!! Kesi ipo mahakamani, nyinyi mnawashwa washwa na nini?
Hakuna yoyote anayewashwa maana maana nchi haiishi leo na yote yatapita.hadi sasa hii nchi bado ni masikini wa kutupa.viongozi wako hawalioni hili kwasababu wana uwezo wa kuchukua kodi nakuzichezea kwa mambo yao binafsi na ya ovyo.Sasa badala tutumie akili kidogo na huu utulivu tulionao kufanya mambo ya msingi ili wajukuu zetu waje waikute nchi iko pazuri sisi tunatumia muda na akili zetu kuchezea kodi za wananchi na kutaka kuharibu huu utulivu kidogo tulionao bila sababu za msingi.
 
Wasalaam wanajukwaa,

Naweza kudiriki kusema kwamba kuna mahali kama taifa tumeshiba sana tuna la amani na ulivyo na amani tuliyonayo ndiyo maana kikundi kidogo cha watu wachache wasiofikiria mbali hakioni aibu kumbambikia kiongozi mkubwa kesi mbaya ya ugaidi ilimradi tu akose dhamana akae mahabusu asifanye kile ambacho kinawakera wao. Ubinadamu imetoweka kabisa, huruma haipo tena mtu haoni taabu kumtesa mwenzake ili yeye atulie afanye atakacho.

Hii haiingii akilini wala haieleweki kwa mtu ambaye alishawahi kuhudhuria moja ya mahakama nchini Kenya kusikiliza kesi za ugaidi zinazowakabili watuhumiwa walioshukiwa kua ni Al-shaabab agents, hakika angaweza kuona kituko kinachofanyika nchini mwetu.Ugaidi anaojiapisha kwa Mungu IGP wa polisi ni wa kufadhiliwa kwa shilingi 600,000? Ugaidi ni wa kupanga kwa bastola yenye risasi 3? Yaani gaidi upangwe kwa Sabaya ambaye ana kesi za uporaji mahakamani hivi sasa?

IGP umeliharibu sana jeshi la polisi wala hakuna mtu atakayekuamini tena wewe, ndiye IGP pekee ambaye jeshi la polisi limetuhumiwa na mkuu wa nchi hadharani kua na kesi nyingi za kubambikizia. Hii maana yake IGP hana weledi wowote wala hofu ya Mungu hana anafanya mambo kuridhisha waliomteua.

Tuache kuchezea sheria za nchi kukomoana na kutesa watu ikiwa tumepewa mamlaka la kulinda raia na mali zao, tuheshimu mhimili wa mahakama kwa kupeleka kesi zenye uhalisia ili kuepusha usumbufu unaojitokeza matumizi ya rasilimali za umma bila sababu maana kuna mambo mengi ya kufanya ya kulijenga taifa.Tunajenga chuki itakayolitafuna taifa miaka nenda rudi kwa sababu ya tamaa za madaraka kwa watu wachache.

Mwalimu Nyerere aliijenga nchi hii kwa gharama kubwa kwa misingi ya utu wa kuheshimiana, kutanguliza busara na hekima. Hakujenga kukomoana na wala hakuliandaa taifa la watu wanaobambikiza watu kesi kwa tuhuma za kutengeneza. Tuheshimu sheria za nchi ili tuweze kujenga taifa imara na lenye nguvu kubwa.

Huwezi kujiaminisha kua wewe ndio wewe kwenye taifaa watu milion zaidi ya 60 wanaofikiri tofauti, siku wakikuchoka utaelewa haya nisemayo.
Swali dogo, unakumbuka Kilwa Kibiti Lindi? Magaidi wa UAMSHO walikuwa wanawaua Polisi na makada wa CCM tu, CUF hawaguswi. CHADEMA hawakusika (huwakuti sehemu kama hizo), Katibu Mkuu Mnyika akasema Bungeni kuwa CCM wamejitakia. Kabla sijaendelea, hawo ni magaidi? I mean akiwemo Mnyika?
 
Wasalaam wanajukwaa,

Naweza kudiriki kusema kwamba kuna mahali kama taifa tumeshiba sana tuna la amani na ulivyo na amani tuliyonayo ndiyo maana kikundi kidogo cha watu wachache wasiofikiria mbali hakioni aibu kumbambikia kiongozi mkubwa kesi mbaya ya ugaidi ilimradi tu akose dhamana akae mahabusu asifanye kile ambacho kinawakera wao. Ubinadamu imetoweka kabisa, huruma haipo tena mtu haoni taabu kumtesa mwenzake ili yeye atulie afanye atakacho.

Hii haiingii akilini wala haieleweki kwa mtu ambaye alishawahi kuhudhuria moja ya mahakama nchini Kenya kusikiliza kesi za ugaidi zinazowakabili watuhumiwa walioshukiwa kua ni Al-shaabab agents, hakika angaweza kuona kituko kinachofanyika nchini mwetu.Ugaidi anaojiapisha kwa Mungu IGP wa polisi ni wa kufadhiliwa kwa shilingi 600,000? Ugaidi ni wa kupanga kwa bastola yenye risasi 3? Yaani gaidi upangwe kwa Sabaya ambaye ana kesi za uporaji mahakamani hivi sasa?

IGP umeliharibu sana jeshi la polisi wala hakuna mtu atakayekuamini tena wewe, ndiye IGP pekee ambaye jeshi la polisi limetuhumiwa na mkuu wa nchi hadharani kua na kesi nyingi za kubambikizia. Hii maana yake IGP hana weledi wowote wala hofu ya Mungu hana anafanya mambo kuridhisha waliomteua.

Tuache kuchezea sheria za nchi kukomoana na kutesa watu ikiwa tumepewa mamlaka la kulinda raia na mali zao, tuheshimu mhimili wa mahakama kwa kupeleka kesi zenye uhalisia ili kuepusha usumbufu unaojitokeza matumizi ya rasilimali za umma bila sababu maana kuna mambo mengi ya kufanya ya kulijenga taifa.Tunajenga chuki itakayolitafuna taifa miaka nenda rudi kwa sababu ya tamaa za madaraka kwa watu wachache.

Mwalimu Nyerere aliijenga nchi hii kwa gharama kubwa kwa misingi ya utu wa kuheshimiana, kutanguliza busara na hekima. Hakujenga kukomoana na wala hakuliandaa taifa la watu wanaobambikiza watu kesi kwa tuhuma za kutengeneza. Tuheshimu sheria za nchi ili tuweze kujenga taifa imara na lenye nguvu kubwa.

Huwezi kujiaminisha kua wewe ndio wewe kwenye taifaa watu milion zaidi ya 60 wanaofikiri tofauti, siku wakikuchoka utaelewa haya nisemayo.
Unaposema tuache kuchezea sheria za nchi na unaingia uhuru wa mahakama. Unashindwa kueleweka unachoongolea usichanganye hisia na utashi wako kuhusu sheria. Kila mtu hana hatia mpk pale itakapothibitishwa kuwa ana hatia.
 
Back
Top Bottom