Ndugu zangu Wahehe wana msemo; Isenga imbofu na isenga indenyoofu. Kwamba ng'ombe kipofu ni sawa tu na ng'ombe aliyevunjika mguu, wote watakufa njaa. Ng'ombe kipofu hawezi kuyaona majani, na yule aliyevunjika mguu hawezi kujikokota kwenda kutafuta nyasi za kula.
Tafakuri yangu iliyopita nilimalizia kwa kuuliza swali: Je, unafikiaje uamuzi wa ama kuingia vitani, au la? Huu ni mwendelezo wa nilipoishia. Naam. Tunavyoenenda kama jamii wakati mwingine ni sawa na ng'ombe kipofu na yule aliyevunjika mguu. Unaweza kuliona hilo nyumbani kwako, katika ukoo wako na hata mahala pako pa kazi. Tumekuwa jamii ya ovyo ovyo. Tunafanya mambo ya ovyo ovyo. Ni kutoka ngazi ya familia na hata ngazi ya kitaifa.
Ona migongano ya wanasiasa wetu sasa. Ona wanavyogawanyika katika makundi yao. Hawatangulizi hata kidogo maslahi ya wengi. Wanajigawa kwenye makundi kugombania mamlaka. Nikasema huko nyuma; aliye gizani humwona aliye kwenye mwanga na aliye kwenye mwanga hamwoni aliye gizani. Na wakati mwingine, hata yule anayejiona yuko kwenye mwanga, naye pia yuko gizani. Wengi walio gizani ni watu wadogo sana. Ni wanyonge waliobakishwa gizani bila ya walio kwenye mwanga kufanya jitihada za dhati kuwatoa gizani.
Leo kuna makundi ya wanasiasa yanayopigana vita isiyo na tija kwa mtu wa kawaida. Wametafuta visingizio vya kuingia vitani. Kuna wanaodai wanapigana kuwatetea wanyonge walio gizani. Walio gizani nao wameanza kuona katika giza hilo hilo, maana wamekuwa gizani kwa muda mrefu. Wameshtuka. Wanahoji mantiki ya vita vinavyopiganwa kwa niaba yao.
Na walioamua kuingia vitani nao wanaonekana kutojiandaa vema na vita hivyo, wanaelekea kushindwa, maana wanapigana vita vya kinafiki. Na kamwe usiingie kwenye vita ambavyo hujajiandaa vema ili ushinde. Mwingine atasema vita vingine havina budi kupiganwa hata kama hujajiandaa kupigana na kushinda. Hapana, huendi vitani ili mradi tu unakwenda vitani , kama vile unakwenda harusini. Vita si lelemama.
Katika dunia hii inasemwa; chagua vita vyako. Haina maana uchague vita kama unachagua mashati ya mitumba Kariakoo. Ina maana kubwa. Pima kwanza, soma alama za nyakati. Chagua vita inayoshindika, iliyo ya muhimu kupiganwa na unayokuwa na hakika ya kuwa umejiandaa vema kulipa gharama ya ushindi.
Miaka mingi iliyopita kulikuwa na Mfalme wa Epilus aliyeitwa Pyrrhic. Mfalme huyu aliamua kuingia vitani kulikabili jeshi kubwa na lenye nguvu nyingi, ni jeshi la Warumi. Lakini kabla ya Mfalme kuingia baharini na vikosi vyake kuitafuta Italia ya Warumi, msaidizi wake wa karibu, Cineas, aliomba mazungumzo ya faragha na Mfalme. Alitaka kumwuliza maswali na kumshauri.
Cineas alimtamkia Mfalme; " E bwana Mfalme, Warumi wanasadikika kuwa na jeshi kubwa , lenye nguvu na lenye mashujaa wengi. Ndio maana wameteka nchi nyingi. Je, Mungu akitusaidia, tukaja kuwashinda Warumi, tutafanya nini na ushindi wetu?
Mfalme akajibu: " Mbona hilo ni swali jepesi sana. Mara ile tukiwashinda Warumi, hakutatokea jeshi kutoka mji wowote wa Italia litakaloweza kupambana nasi."
Cineas alitulia kidogo, kisha akamwuliza Mfalme: " Tukishaikamata Italia ya Warumi, kipi kitafuatia?"
Mfalme akajibu: Sicily ni kisiwa chenye hazina za thamani kubwa, itakuwa rahisi sana kukiteka kisiwa hicho."
Cineas aliendelea kuuliza: " Bwana Mfalme unaongea juu ya mambo ya kusadikika, lakini una maana kukitwaa kisiwa cha Sicily kutakuwa na maana ya kukoma kwa vita?"
Mfalme akajibu: " Hapo tutakuwa tumeikaribia Afrika. Na tukishaikamata Afrika ni nani hapa duniani atathubutu kutukabili kivita?"
" Hakuna" Alijibu Cineas, kisha akauliza; " Na baada ya hapo tutafanya nini?"
Mpaka hapo Mfalme hakujua Cineas alikuwa anampeleka wapi kwa lojiki ya kifikra. Mfalme akajibu:
" Baada ya hapo, tutapumzika, tutakula raha. Tutakula na kunywa . Tutabaki tukichekeshana na kucheka, siku nzima."
Kama ni hivyo, alisema Cineas; " Ni kitu gani kinachotuzuia kufanya hayo yote sasa bila kwenda vitani?
Mfalme hakuielewa mantiki ya Cineas. Akakaidi ushauri. Akavipeleka vikosi vyake kupambana na Warumi. Baada ya vita ngumu, jeshi la mfalme liliwashinda Warumi. Hata hivyo lilipata hasara kubwa ya kupoteza watu na kuwa na majeruhi wengi. Jeshi lake likadhohofika sana. Likajaribu kuitwaa Sparta, likashindwa vibaya sana. Mfalme aliwindwa na hatimaye akakakamatwa na kuawa kwa kupigwa mawe kwenye mitaa ya Argos. Isenga imbofu na isenga indenyoofu. Ng'ombe kipofu ni sawa tu na ng'ombe aliyevunjika mguu, wote watakufa njaa. Wanasema ndugu zangu Wahehe. Naendelea kutafakari, nawe tafakari pia.
Maggid ( Mwalimu Wa Zamu)
Iringa,
Februari 4, 2010
+255 788 111 765http://www.kwanzajamii.com
Tafakuri yangu iliyopita nilimalizia kwa kuuliza swali: Je, unafikiaje uamuzi wa ama kuingia vitani, au la? Huu ni mwendelezo wa nilipoishia. Naam. Tunavyoenenda kama jamii wakati mwingine ni sawa na ng'ombe kipofu na yule aliyevunjika mguu. Unaweza kuliona hilo nyumbani kwako, katika ukoo wako na hata mahala pako pa kazi. Tumekuwa jamii ya ovyo ovyo. Tunafanya mambo ya ovyo ovyo. Ni kutoka ngazi ya familia na hata ngazi ya kitaifa.
Ona migongano ya wanasiasa wetu sasa. Ona wanavyogawanyika katika makundi yao. Hawatangulizi hata kidogo maslahi ya wengi. Wanajigawa kwenye makundi kugombania mamlaka. Nikasema huko nyuma; aliye gizani humwona aliye kwenye mwanga na aliye kwenye mwanga hamwoni aliye gizani. Na wakati mwingine, hata yule anayejiona yuko kwenye mwanga, naye pia yuko gizani. Wengi walio gizani ni watu wadogo sana. Ni wanyonge waliobakishwa gizani bila ya walio kwenye mwanga kufanya jitihada za dhati kuwatoa gizani.
Leo kuna makundi ya wanasiasa yanayopigana vita isiyo na tija kwa mtu wa kawaida. Wametafuta visingizio vya kuingia vitani. Kuna wanaodai wanapigana kuwatetea wanyonge walio gizani. Walio gizani nao wameanza kuona katika giza hilo hilo, maana wamekuwa gizani kwa muda mrefu. Wameshtuka. Wanahoji mantiki ya vita vinavyopiganwa kwa niaba yao.
Na walioamua kuingia vitani nao wanaonekana kutojiandaa vema na vita hivyo, wanaelekea kushindwa, maana wanapigana vita vya kinafiki. Na kamwe usiingie kwenye vita ambavyo hujajiandaa vema ili ushinde. Mwingine atasema vita vingine havina budi kupiganwa hata kama hujajiandaa kupigana na kushinda. Hapana, huendi vitani ili mradi tu unakwenda vitani , kama vile unakwenda harusini. Vita si lelemama.
Katika dunia hii inasemwa; chagua vita vyako. Haina maana uchague vita kama unachagua mashati ya mitumba Kariakoo. Ina maana kubwa. Pima kwanza, soma alama za nyakati. Chagua vita inayoshindika, iliyo ya muhimu kupiganwa na unayokuwa na hakika ya kuwa umejiandaa vema kulipa gharama ya ushindi.
Miaka mingi iliyopita kulikuwa na Mfalme wa Epilus aliyeitwa Pyrrhic. Mfalme huyu aliamua kuingia vitani kulikabili jeshi kubwa na lenye nguvu nyingi, ni jeshi la Warumi. Lakini kabla ya Mfalme kuingia baharini na vikosi vyake kuitafuta Italia ya Warumi, msaidizi wake wa karibu, Cineas, aliomba mazungumzo ya faragha na Mfalme. Alitaka kumwuliza maswali na kumshauri.
Cineas alimtamkia Mfalme; " E bwana Mfalme, Warumi wanasadikika kuwa na jeshi kubwa , lenye nguvu na lenye mashujaa wengi. Ndio maana wameteka nchi nyingi. Je, Mungu akitusaidia, tukaja kuwashinda Warumi, tutafanya nini na ushindi wetu?
Mfalme akajibu: " Mbona hilo ni swali jepesi sana. Mara ile tukiwashinda Warumi, hakutatokea jeshi kutoka mji wowote wa Italia litakaloweza kupambana nasi."
Cineas alitulia kidogo, kisha akamwuliza Mfalme: " Tukishaikamata Italia ya Warumi, kipi kitafuatia?"
Mfalme akajibu: Sicily ni kisiwa chenye hazina za thamani kubwa, itakuwa rahisi sana kukiteka kisiwa hicho."
Cineas aliendelea kuuliza: " Bwana Mfalme unaongea juu ya mambo ya kusadikika, lakini una maana kukitwaa kisiwa cha Sicily kutakuwa na maana ya kukoma kwa vita?"
Mfalme akajibu: " Hapo tutakuwa tumeikaribia Afrika. Na tukishaikamata Afrika ni nani hapa duniani atathubutu kutukabili kivita?"
" Hakuna" Alijibu Cineas, kisha akauliza; " Na baada ya hapo tutafanya nini?"
Mpaka hapo Mfalme hakujua Cineas alikuwa anampeleka wapi kwa lojiki ya kifikra. Mfalme akajibu:
" Baada ya hapo, tutapumzika, tutakula raha. Tutakula na kunywa . Tutabaki tukichekeshana na kucheka, siku nzima."
Kama ni hivyo, alisema Cineas; " Ni kitu gani kinachotuzuia kufanya hayo yote sasa bila kwenda vitani?
Mfalme hakuielewa mantiki ya Cineas. Akakaidi ushauri. Akavipeleka vikosi vyake kupambana na Warumi. Baada ya vita ngumu, jeshi la mfalme liliwashinda Warumi. Hata hivyo lilipata hasara kubwa ya kupoteza watu na kuwa na majeruhi wengi. Jeshi lake likadhohofika sana. Likajaribu kuitwaa Sparta, likashindwa vibaya sana. Mfalme aliwindwa na hatimaye akakakamatwa na kuawa kwa kupigwa mawe kwenye mitaa ya Argos. Isenga imbofu na isenga indenyoofu. Ng'ombe kipofu ni sawa tu na ng'ombe aliyevunjika mguu, wote watakufa njaa. Wanasema ndugu zangu Wahehe. Naendelea kutafakari, nawe tafakari pia.
Maggid ( Mwalimu Wa Zamu)
Iringa,
Februari 4, 2010
+255 788 111 765http://www.kwanzajamii.com