TTCL na huduma ya internet

Tiba

JF-Expert Member
Jul 15, 2008
4,604
3,163
Naleta mbele yenu kisa hiki ambacho kimenipata mimi mwenyewe. Ukipita mitaa mingi ya Dar Es Salaam kuna mabango kila mahali yanayoonyesha kwamba TTCL wanatoa huduma ya internet. Pamoja na kwamba kuna makampuni mengi sasa hivi yanatoa huduma hii, mimi nilishawishika kuwajaribu TTCL kwa maana nzima ya kulipiga tafu shirika letu la umma pamoja na kuonywa na rafiki yangu mmoja kwamba TTCL ni wasumbufu na kwamba itanichukua muda mrefu kupata huduma hiyo. Lakini kinachoendelea kwa sasa huwezi kuamini kwamba ndio watu wale wale walitumia mamilioni ya shillingi kuweka matangazo kwamba wanatoa huduma hii. Tarehe 21 December 2009 nilikwenda pale TTCL Ubungo plaza na kuulizia uwezekano wa kuunganishiwa internet nyumbani kwangu. Nilipewa fomu nikajaza na kuonyesha nitachukua package ipi kati ya zilizokuwepo baada ya kupewa maelezo na kushauriwa nitumie landline ili niweze kupata huduma nzuri zaidi. Niliwafahamisha kuwa ninayo landline nyumbani kwangu na hivyo nikaambiwa atatumwa fundi kuja kuangalia eneo. Ni kweli fundi alikuja na baadae walinitaka nikalipie. Nililipia connection fee ya Tshs. 25,000 na baada ya hapo ikawa kimya. Baada ya kuwafuatilia nikataarifiwa kuwa siwezi kupewa huduma hiyo kwa sasa kwa kuwa wameishiwa modem. Nikaulizia uwezekano wa kununua modem yangu mwenyewe wakasema sawa ninunue halafu niwataarifu waje kufunga. Pamoja na kulipia hiyo gharama ya internet ya mwezi mmoja tarehe 21 January 2010, mpaka leo fundi hajaja kuniunganishia hiyo huduma. Ukienda pale ofisini kwao wanakwambia fundi alikuja hakukuta mtu nyumbani, ukimpigia fundi simu kuuliza anadai alikuwa busy sana bado hajaja!!! (Contradiction)

Swali langu ni je hali hii imeishamkuta mtu mwingine au imetokea kwa bahati mbaya kwangu tu? Je hawa jama zetu kwa mtindo huu ni kweli wamejiandaa kufanya biashara kwa ushindani? Je wakubwa huko makao makuu wanajua madudu yanayofanywa na watendaji wao hawa?

Natabiri kufa na kuzikwa kwa TTCL muda si mrefu endapo hali hii haikutokea kwa bahati mbaya tu.

Tiba
 
Pole, That is one isolated case, TTCL broadband is the fastest, cheapest na most reliable!. 40,000/= per month, you enjoy unlimited wireless 24/7.
 
Naleta mbele yenu kisa hiki ambacho kimenipata mimi mwenyewe. Ukipita mitaa mingi ya Dar Es Salaam kuna mabango kila mahali yanayoonyesha kwamba TTCL wanatoa huduma ya internet. Pamoja na kwamba kuna makampuni mengi sasa hivi yanatoa huduma hii, mimi nilishawishika kuwajaribu TTCL kwa maana nzima ya kulipiga tafu shirika letu la umma pamoja na kuonywa na rafiki yangu mmoja kwamba TTCL ni wasumbufu na kwamba itanichukua muda mrefu kupata huduma hiyo. Lakini kinachoendelea kwa sasa huwezi kuamini kwamba ndio watu wale wale walitumia mamilioni ya shillingi kuweka matangazo kwamba wanatoa huduma hii. Tarehe 21 December 2009 nilikwenda pale TTCL Ubungo plaza na kuulizia uwezekano wa kuunganishiwa internet nyumbani kwangu. Nilipewa fomu nikajaza na kuonyesha nitachukua package ipi kati ya zilizokuwepo baada ya kupewa maelezo na kushauriwa nitumie landline ili niweze kupata huduma nzuri zaidi. Niliwafahamisha kuwa ninayo landline nyumbani kwangu na hivyo nikaambiwa atatumwa fundi kuja kuangalia eneo. Ni kweli fundi alikuja na baadae walinitaka nikalipie. Nililipia connection fee ya Tshs. 25,000 na baada ya hapo ikawa kimya. Baada ya kuwafuatilia nikataarifiwa kuwa siwezi kupewa huduma hiyo kwa sasa kwa kuwa wameishiwa modem. Nikaulizia uwezekano wa kununua modem yangu mwenyewe wakasema sawa ninunue halafu niwataarifu waje kufunga. Pamoja na kulipia hiyo gharama ya internet ya mwezi mmoja tarehe 21 January 2010, mpaka leo fundi hajaja kuniunganishia hiyo huduma. Ukienda pale ofisini kwao wanakwambia fundi alikuja hakukuta mtu nyumbani, ukimpigia fundi simu kuuliza anadai alikuwa busy sana bado hajaja!!! (Contradiction)

Swali langu ni je hali hii imeishamkuta mtu mwingine au imetokea kwa bahati mbaya kwangu tu? Je hawa jama zetu kwa mtindo huu ni kweli wamejiandaa kufanya biashara kwa ushindani? Je wakubwa huko makao makuu wanajua madudu yanayofanywa na watendaji wao hawa?

Natabiri kufa na kuzikwa kwa TTCL muda si mrefu endapo hali hii haikutokea kwa bahati mbaya tu.

Tiba

Mkuu pole, hujafa hujaumbika. kwani wewe ni mgeni na utaratibu wetu ukitaka huduma ? hasa kwenye mashirika yetu haya? hebu tafakari kuna mahali UNAKOSEA.
 
nilienda kuulizia kuhusu huduma zao kwanza customer care ilikuwa mbovu, hovyo kabisa.....na pia nilijibiwa kwa wakati huo modem hazipo nijaribu kupitia baada ya mwezi...hawa ndugu zetu naona wako mahututi na huu ushindani wa biashara nawatakia kila la kheri
 
Pole, That is one isolated case, TTCL broadband is the fastest, cheapest na most reliable!. 40,000/= per month, you enjoy unlimited wireless 24/7.

mkuu nadhani hiyo unazungumzia ya 45.000 per month ambayo ni shared 1/50. sidhani kama inaweza kuwa as fast kama ya kwako mwenyewe ambayo kuna package za kuanzia 1G kwa 30,000 kwa mwezi
 
Pole ndugu Tiba. Naona ya kwako ni isolated case zaidi, sehemu nyinginezo huduma zao ni relatively good, isipokuwa kwa upande wa customer care, they have some problems. Nakushauri uende kwenye matawi mengine hapo Dar ili upresent issue yake. Otherwise wapigie customer care ili wakusaidie.
 
mkuu nadhani hiyo unazungumzia ya 45.000 per month ambayo ni shared 1/50. sidhani kama inaweza kuwa as fast kama ya kwako mwenyewe ambayo kuna package za kuanzia 1G kwa 30,000 kwa mwezi

Nipo nawe kabisa Kaizer hapa. Mimi nimechukua package ya 2G kwa elfu 60 kwa mwezi. Ni huduma bomba si kawaida.

Ni kweli kuna usumbufu kidogo katika kuunganishwa. Tena hapo Ubungo Plaza wanamtegemea fundi mmoja kijana anaitwa Ngasapa. Hana makuu, ila tu mizunguko ya mijini ni mingi.
 
Pole ndugu Tiba. Naona ya kwako ni isolated case zaidi, sehemu nyinginezo huduma zao ni relatively good, isipokuwa kwa upande wa customer care, they have some problems. Nakushauri uende kwenye matawi mengine hapo Dar ili upresent issue yake. Otherwise wapigie customer care ili wakusaidie.


Buchanan sijui kama umemsaidia umesema upande wa customer care ndiyo mbovu mwishoni ukamwambia awapigie tena hao hao customer care ili wamsaidie which is which!
 
Nipo nawe kabisa Kaizer hapa. Mimi nimechukua package ya 2G kwa elfu 60 kwa mwezi. Ni huduma bomba si kawaida.

Ni kweli kuna usumbufu kidogo katika kuunganishwa. Tena hapo Ubungo Plaza wanamtegemea fundi mmoja kijana anaitwa Ngasapa. Hana makuu, ila tu mizunguko ya mijini ni mingi.
Fair explanations, we are together.
 
Buchanan sijui kama umemsaidia umesema upande wa customer care ndiyo mbovu mwishoni ukamwambia awapigie tena hao hao customer care ili wamsaidie which is which!

Ni kweli inaonekana kama sijamsaidia lakini sivyo. Mimi kuna siku nilijibiwa vibaya sana na mtu wa customer care lakini nilipopiga tena alipokea mwingine aliyenihudumia vizuri sana! Ndio maana nilisema kuwa kuna "some problems" kwenye customer care!
 
Tiba pole,
Nakushauri uende TTCL pale nyerere road katibu na kamapuni ya sigara, wale jamaa wanasikiliza shida za wateja na kufanyia mteja kitu anachohitaji. Mimi nimenunua modem EC226 sikupata usumbufu sasa nakula internet kama kawa. Yawezekana hilo ni tatizo la mtu mmoja lakini sio sera ya TTCL
 
Tiba pole,
Nakushauri uende TTCL pale nyerere road katibu na kamapuni ya sigara, wale jamaa wanasikiliza shida za wateja na kufanyia mteja kitu anachohitaji. Mimi nimenunua modem EC226 sikupata usumbufu sasa nakula internet kama kawa. Yawezekana hilo ni tatizo la mtu mmoja lakini sio sera ya TTCL

Hiyo modem EC226 inagharimu kiasi gani kwa sasa mkuu?
 
Mkuu pole, hujafa hujaumbika. kwani wewe ni mgeni na utaratibu wetu ukitaka huduma ? hasa kwenye mashirika yetu haya? hebu tafakari kuna mahali UNAKOSEA.

Mkuu Kaizer,

Wapi nakosea Mzee nisaidie!!!!

Tiba
 
Pole, That is one isolated case, TTCL broadband is the fastest, cheapest na most reliable!. 40,000/= per month, you enjoy unlimited wireless 24/7.

Mkuu Pasco,

Ndio maana nimeuliza kama kuna mwingine aliishakutana na hadha hii au is just an isolated case kama ulivyosema!!!.

Tiba
 
nilienda kuulizia kuhusu huduma zao kwanza customer care ilikuwa mbovu, hovyo kabisa.....na pia nilijibiwa kwa wakati huo modem hazipo nijaribu kupitia baada ya mwezi...hawa ndugu zetu naona wako mahututi na huu ushindani wa biashara nawatakia kila la kheri

Kama mambo yenyewe ndio hayo kwa nini walijitangaza kwa nguvu kutoa huduma hii? Wana sababu gani za msingi za kuishiwa na modem? Wanaye qualified supplies director?

Tiba
 
Pole ndugu Tiba. Naona ya kwako ni isolated case zaidi, sehemu nyinginezo huduma zao ni relatively good, isipokuwa kwa upande wa customer care, they have some problems. Nakushauri uende kwenye matawi mengine hapo Dar ili upresent issue yake. Otherwise wapigie customer care ili wakusaidie.

Mkuu Buchanan,

Nakushukuru kwa ushauri wako. Itabidi sasa nikamwone meneja wa kanda ambaye nimeambiwa anakaa ofisi ya Osterbay. Hao customer care nikiwapigia wananipa taarifa za uongo mara fundi amekuja hajakuta mtu, mara walimkuta mtu lakini amekataa kuwafubgulia mlango mambo ambayo ni uongo mtupu!!!

Tiba
 
Nipo nawe kabisa Kaizer hapa. Mimi nimechukua package ya 2G kwa elfu 60 kwa mwezi. Ni huduma bomba si kawaida.

Ni kweli kuna usumbufu kidogo katika kuunganishwa. Tena hapo Ubungo Plaza wanamtegemea fundi mmoja kijana anaitwa Ngasapa. Hana makuu, ila tu mizunguko ya mijini ni mingi.


Mkuu The Invicible,

Na mimi nimeomba na kulipia hiyo package ya 2GB kwa Tshs. 60,000 kwa mwezi lakini ndiyo hivyo bado sijabahatika kufungiwa hiyo huduma pamoja na kununua modema yangu mwenyewe.

Tiba
 
Tiba pole,
Nakushauri uende TTCL pale nyerere road katibu na kamapuni ya sigara, wale jamaa wanasikiliza shida za wateja na kufanyia mteja kitu anachohitaji. Mimi nimenunua modem EC226 sikupata usumbufu sasa nakula internet kama kawa. Yawezekana hilo ni tatizo la mtu mmoja lakini sio sera ya TTCL


Mkuu Fungwe,

Asante kwa ushauri ingawaje umesema hiyo sera ya TTCL (OF COURSE SIO) lakini pamoja na hiyo isolated case yangu kama mnavyosema, inakuwaje hawana moden mpaka wateja tununue wenyewe? Suala hapa kwa mtindo huu hawa jamaa wamejiandaa kushindana kweli kwenye ili soko huria? Nakumbuka wakati naomba nifungiwe line ya simu some 10 years ago, it did not take that much long pamoja na kwamba they were only service provider available. Iweje leo wakati watoa huduma za internet wako kibao?

Tiba
 
Nilikua mteja wa Sasatel nikaachananao bada ya kuhesabu MB nikaona zinakwend aupesi hata kama nimefungua webpage isiyo na picha wala video. nimeamua kuachana nao.

Swali langu, mimi natumia sana Net kucheki shows kweney Youtube, sija jua ni mtandao gani utakau kidogo afadhali maana hizo 1GB ni najidanganya , je Africa online wao wako vipi?,Thanx
 
Back
Top Bottom