TTCL bado hawajaweza kujipanga na kupambana na mabadiliko ya soko huria

kinjumbi one

JF-Expert Member
May 27, 2015
1,694
2,132
TTCL bado hawajaweza kujipanga na kupambana na movement za soko huria. Nasema hivyo kwasababu mwaka 2010 walikuja kujaribu kuleta line za simu ya mkononi, na vocha zake kama ilivyo mitandao mengine na code yao wao walitumia 073. Ilikua poa na vocha zao zikaanza kuuzika kwa kiasi flani.

Lakini pamoja na uzuri huo, ila kuna kasoro kubwa waliifanya hima kwa makusudi au ndo ujuaji sana, hata sijui. Ni kwamba line yao ilikua huwezi kuweka katika simu yeyote ispokua katika simu yao tu yani ilikulazimu kama unataka line ya TTCL, ni lazima ununue na simu yao. Hii ilipunguza morali au kushusha kabisa muamko wa mtandao wao, kama ilivyoshuka Sasatel.

Leo wamekuja tena na matangazo kemkem na hashtag ya "rudi nyumbani kumenoga". Kwa kiasi flani wapo poa na watu wameanza kuwaelewa. Ila sasa kasoro yao kubwa ile ya miaka nane iliyopita wameileta tena, eti line yao haisomi katika simu za kawaida hadi iwe ya 4g au kwa uchache zipo za 3g, lile tabaka la 2010 wamelileta tena, lakini kwa namna nyingine.

Kwa maoni yangu hata iweje kwa style hii ya kutoa bidhaa za ajabuajabu huku wenyewe wakijiona ndo wanafanya jambo la maana hawataweza kutoboa, yani kuwashinda akina Voda, Tigo na Airtel bado ni ndoto za mchana.

Nawasilisha.
 
Masahihisho:
CDMA ya ttcl iliingia mwaka 2006 na siyo 2010
Line za 4G zinweza kutumika kwenye device yenye 3G bila shida.

Shida yao kwa upande wangu ni kuenea katika maeneo machache, kutopatikana kwa vocha mahali pengi na spidi ndogo ya internet ( angalau huku ninakoishi). Tatizo lingine litakalowagharimu ni visibility.. maana ya kujitangaza. Wasipojikita kurekebisha hizi kasoro, pasi na shaka ttclmobile itakufa kifo kibaya sana
 
Masahihisho:
CDMA ya ttcl iliingia mwaka 2006 na siyo 2010
Line za 4G zinweza kutumika kwenye device yenye 3G bila shida.

Shida yao kwa upande wangu ni kuenea katika maeneo machache, kutopatikana kwa vocha mahali pengi na spidi ndogo ya internet ( angalau huku ninakoishi). Tatizo lingine litakalowagharimu ni visibility.. maana ya kujitangaza. Wasipojikita kurekebisha hizi kasoro, pasi na shaka ttclmobile itakufa kifo kibaya sana
kwanini line zao sisome ktk device zote hata kama hiyo line ni ya 4g? Mbona wenzao wana line za 4g lakini bado zinasoma hata ktk simu za "tochi"?
 
Hawa TTCL naona wanajitangaza Twitter tu, kwengine siwaoni. Network yao mpanga uwe maeneo ya wazi kama kwenye kiwanja cha mpira ukiingia ndani ya nyumba hamna kitu. Kama uko kitandani inakulazimu ulalie ubavu wa kushoto ndio utaipata ukigeuka ubavu wa kulia inapotea.
 
Technology inakua ,nadhan wamecounter ilo,baada ya miaka kadha 2G itabak kua historia
 
Hili shirika litakufa kifo cha mende ktk hii telecom industry kwa huu uzembe wao.
 
Technology inakua ,nadhan wamecounter ilo,baada ya miaka kadha 2G itabak kua historia
Hata USA na nchi nyingine zilizoendelea bado wanatumia GSM network, iweje wao TTCL waamue kuikacha mapema kiasi hicho? Wanalenga soko gani? Yani kama simu ina line mbili, niki-switch 3/4G kwenye line ya Airtel, Ile ya pili ya TTCL inakata mawasiliano, that's rubbish.
 
Mimi ninayo mambo yangu, nikiandika humu nahisi kuna mtu anaweza fukuzwa kazi, ngoja tu niache but kwa ujumla TTCL ni mfano mmoja wapo wa mashirika ya serikali ambayo yanaonesha kwamba "Serikali haiwezi fanya biashara" eneo lolote lenye ushindani. Kwa ufupi jamaa wana udhi sana.
 
Mimi ninayo mambo yangu, nikiandika humu nahisi kuna mtu anaweza fukuzwa kazi, ngoja tu niache but kwa ujumla TTCL ni mfano mmoja wapo wa mashirika ya serikali ambayo yanaonesha kwamba "Serikali haiwezi fanya biashara" eneo lolote lenye ushindani. Kwa ufupi jamaa wana udhi sana.

Waharibie tu mkuu.. hili kampuni lina kodi zetu zimezikwa hapo.. halafu wafanyakazi wanalipwa mishahara.. tena shindani ili kuwa karibu na operators wengine.. halafu wanazingua..
.
 
Waharibie tu mkuu.. hili kampuni lina kodi zetu zimezikwa hapo.. halafu wafanyakazi wanalipwa mishahara.. tena shindani ili kuwa karibu na operators wengine.. halafu wanazingua..
.
Tena wana boa sana hawa jamaa, shida moja inayo niudhi mimi ni hi, managing director wake pamoja na mameneja wa mikoa wanazo degree, tena the former CEO wa hi kampuni alikua anazo degree 3 halafu mambo wanayo yafanya utadhani ni wa darasa la saba.
 
Nipo tofauti na nyie, mimi nawaona wapo poa, wana roll out taratibu kwa sababu investment katika telecoms inahitaji pesa ya kutosha. Nadhani itafika wakati mtawapenda. Kwa sababu huduma zao zipo mijini, walengwa wao ni wenye smartphone. Swali langu utaishije mjini bila kuwa na smart phone? Hivyo visimu vyenu vyenye 2G wapelekee ndugu zenu vijijini, msitumie ulofa wenu kuwasema vibaya TTCL.
 
Nipo tofauti na nyie, mimi nawaona wapo poa, wana roll out taratibu kwa sababu investment katika telecoms inahitaji pesa ya kutosha. Nadhani itafika wakati mtawapenda. Kwa sababu huduma zao zipo mijini, walengwa wao ni wenye smartphone. Swali langu utaishije mjini bila kuwa na smart phone? Hivyo visimu vyenu vyenye 2G wapelekee ndugu zenu vijijini, msitumie ulofa wenu kuwasema vibaya TTCL.
biashara haipo hivyo. biashara inaangalia kona zote. Ndiyo maana makampuni yenye akili wanaendana na mabadiliko ya ki uchumi duniani lkn hayaachani na ya kale. Karibu mitandao yote inatoa line za 4G, lkn karibu mitandao yote inayotoa line za 4G zake zinasoma ktk network ya GSM. Ni ujinga kuleta bidhaa zenye upungufu upungufu, alafu mkipitwa ki biashara mnaita watu mafisadi.
 
TTCL bado hawajaweza kujipanga na kupambana na movement za soko huria. Nasema hivyo kwasababu mwaka 2010 walikuja kujaribu kuleta line za simu ya mkononi, na vocha zake kama ilivyo mitandao mengine na code yao wao walitumia 073. Ilikua poa na vocha zao zikaanza kuuzika kwa kiasi flani.

Lakini pamoja na uzuri huo, ila kuna kasoro kubwa waliifanya hima kwa makusudi au ndo ujuaji sana, hata sijui. Ni kwamba line yao ilikua huwezi kuweka katika simu yeyote ispokua katika simu yao tu yani ilikulazimu kama unataka line ya TTCL, ni lazima ununue na simu yao. Hii ilipunguza morali au kushusha kabisa muamko wa mtandao wao, kama ilivyoshuka Sasatel.

Leo wamekuja tena na matangazo kemkem na hashtag ya "rudi nyumbani kumenoga". Kwa kiasi flani wapo poa na watu wameanza kuwaelewa. Ila sasa kasoro yao kubwa ile ya miaka nane iliyopita wameileta tena, eti line yao haisomi katika simu za kawaida hadi iwe ya 4g au kwa uchache zipo za 3g, lile tabaka la 2010 wamelileta tena, lakini kwa namna nyingine.

Kwa maoni yangu hata iweje kwa style hii ya kutoa bidhaa za ajabuajabu huku wenyewe wakijiona ndo wanafanya jambo la maana hawataweza kutoboa, yani kuwashinda akina Voda, Tigo na Airtel bado ni ndoto za mchana.

Nawasilisha.
Zamanj walikuwa wanatumia technologia ya WCDMA wakati wenzao walikuwa wanatumua GSM.. sijui nani aliwaingiza choo cha kike.. WCDMA ili prove failure Africa.. ilifanikiwa sana South America..
kwa sasa hvi nadhan SIM card zao zinatakiwa kussuport both 2G and 4G. ila nahisi tatizo ni coverage. watakuwa na site chache sna
 
biashara haipo hivyo. biashara inaangalia kona zote. Ndiyo maana makampuni yenye akili wanaendana na mabadiliko ya ki uchumi duniani lkn hayaachani na ya kale. Karibu mitandao yote inatoa line za 4G, lkn karibu mitandao yote inayotoa line za 4G zake zinasoma ktk network ya GSM. Ni ujinga kuleta bidhaa zenye upungufu upungufu, alafu mkipitwa ki biashara mnaita watu mafisadi.
Hata sumsung wanatengeneza smart phone ya kizazi kijacho lakini haijaacha kutengeneza sim za elfu 20.

Ni unjinga mkubwa. Labda waseme wao wamelenga corporate customers, watu wenye kipato kikubwa tu.

Watu wenye kipato kikubwa wanataka huduma bora na ya uhakika, sio hyo ya ttcl ambayo ukilalia ubavu wa kulia haipatikani.
 
Mimi ninayo mambo yangu, nikiandika humu nahisi kuna mtu anaweza fukuzwa kazi, ngoja tu niache but kwa ujumla TTCL ni mfano mmoja wapo wa mashirika ya serikali ambayo yanaonesha kwamba "Serikali haiwezi fanya biashara" eneo lolote lenye ushindani. Kwa ufupi jamaa wana udhi sana.
Kwanini Tanesco nayo isishindanishwe na makampun mengine kama TTCL ili ikafie mbali hawa wasingeshindanishwa wangetutesa sana kama TANESCO wanavyotusema kukatika kwa umeme kupandisha bei miundombinu ya zamani uzembe na matizo kibao, tungekua tunapata bando za units na umeme wa wireless na maubunifu kibao kwenye umeme,Hawa jamaa awategemei mauzo kijiendesha wanategemea ruzuku kutoka serekali kwaiyo awana presha.
 
Back
Top Bottom