Mil 12.9 zatafunwa shule ya sekondari Lugarawa
Na Amiri Kilagalila,NjombeMkuu wa wilaya ya Ludewa mkoani Njombe Andrea Tsere ameagiza jeshi la polisi kuwakamata wote walio husika na upotevu wa Mil 12.9 fedha iliyochangwa na wananchi kwa ajili ya chakula cha wanafunzi wa shule ya sekondari Lugarawa wilayani hapo.
Aidha Mkuu huyo wa wilaya ya Ludewa mkoani Njombe wa kushoto amekagua na kuridhishwa na vyumba vipya vya madarasa katika shule ya sekondari ya Lugarawa vilivyojengwa ili kupunguza changamoto ya miundombinu katika shule hiyo.