Tsh 3,500,000 Kwa Daktari wa Watanzania ni aibu!

Hii hoja ya Eng Y. Bihagaze sidhani kama ina kosa lolote lile.

Ametoa hoja nzuri tu ya msingi kwamba serikali haijali raia wake ambao kwa bahati mbaya kwa miaka nenda rudi hawaoni kwamba kuna tofauti kubwa ya maisha kugawiwa kati ya walicho nacho na wasio nacho.

Serikali ya CCM ingejaribu kusema kwamba sasa (kwa mfano) kwamba kuna mpango wa miaka mitano ya kuboresha hali ya miji yetu na kwa kuanzia tunataka kuliimarisha jiji la Dar-es-Salaam kwa kila kitu- miundo mbinu kama barabara, huduma ya usafiri, na kusema kwamba wilaya zake zitakuwa zikifanya kazi kwa kujitegemea zaidi kwenye maeneo kama kwenye ukusanyaji kodi za maendeleo.

Kwa mfano barabara nyingi za jiji la Dar-es-Salaam kwa sasa zina foleni ndefu sana na huweza kuchukua masaa zaidi ya sita hii ni moja ya makosa kwani upangaji mzuri wa njia za usafiri haujafanywa na ni pesa ndio inahitajika.

Pili, pamoja na kuandaa usafiri wa mabasi ambayo inasemwa yatakuwa yakienda kwa kasi bado kuna maeneo mengi tu ambayo yanahitaji marekebisho na si kwa kuzibaziba tu bali hata kujenga upya. Barabara kama ya tabata relini haipaswi kufanywa ndo njia ya mkato kwenye mjini kutokana na foleni ndefu hapo katikati.

Mheshimiwa raisi kama mimi analifahamu vizuri jiji la Dar-es-Salaam kama alivyo mzee Balozi Skyes na viongozi wengine. Lakini hata siku moja sidhani kama mheshimiwa raisi katika miaka kumi ambayo amekaa madarakani amewaza kuboresha miundo mbinu ya jiji hili ambapo mvua ikinyesha tu jiji zima hufurika maji.

Sasa kwenye suala la wana taaluma wetu hasa madaktari, mheshimiwa raisi akaleta uamuzi wake kwamba kama hawataki hizo milioni 3.5 watafute mwajiri ambae ataweza kuwalipa pesa hizo. Halafu watu wengi nao wanaunga mkono wazo hili la raisi.

Hii ni kasoro kwenye jamii kwani jamii imekuwa imefungwa na haiwezi kufikiri.

Pale Muhimbili bado mpaka leo akina mama wajawazito wanalala chini, chumba cha maiti bado ni kidogo sana na hata kuna wakati niliwahi kushuhudia mama mmoja akiondoka kwa miguu huku akiwa ameshikilia mfuko wa Rambo ambao niligundua kuwa ni maiti ya kitoto kichanga ambacho kilipoteza maisha baada tu ya kuzaliwa kutokana na matatizo kadhaa.

Na kwakuwa nafasi zilijaa kwenye kachumba hako basi aliambaiwa maiti ya mtoto huyo isingeweza kukaa humo zaidi ya siku moja.

Jamii yetu ya Watanzania ambao wamebahatika kuwa kwenye nafasi mbalimbali imefungwa na hatuna nafasi ya kufikiri na kubuni mambo yetu wenyewe.

Hospitali ya Muhimbili ilitakiwa iwe ni mfano wa kuigwa wa hospitali nyingi nchini mwetu na hata nje ya mipaka yetu.

Hospitali hii ipo tokea tupate uhuru na ni miaka mingi imepita. Hopitali hii ingeendelezwa kwa kuwa na ukubwa unaostahili kutoa huduma zote muhimu zikiwemo hata za kuhudumia viongozi wetu na familia zao badala ya kwenda nje ya nchi.

Kwahio mheshimiwa raisi na serikali yake angeangalia upya sekta ya Afya na kutafuta mawazo labda kwamba aunde bodi au utawala au kwa kiingereza trust ambayo itakuwa na kazi ya kusimamia hospitali zote kubwa nchini. Bodi hii itajitegemea kwa kila kitu na itasimamia ajira za madaktari, manesi, idara ya huduma za dharura, na ajira za mpaka wapiga deki.

Bodi hii inakuwa inaundwa na watu ambao hawahusiani na serikali ingawa wanaweza kuulizwa maswali kuhusu bajeti zao na mambo mengine lakini kazi yao kuwa ni kuhakikisha inasimamia hospitali zote na kuhakikisha hospitali zinajiendesha katika viwango vinavyokubalika kimataifa.

Pamoja na mambo mengine bodi hii itasimamia pia malipo ya mishahara kwa wafanyakazi wa hospitali wakiwemo madaktari na pia itaangalia ubora wa huduma watoazo na pia kuwadaidia madaktari katika masuala mbalimbali kwa kushirikiana na chama chao na jumuiya zao.

Ndio tutaona hapo kwamba kila hospitali inakuwa na nafasi kwa kila mgonjwa ambae anahijtaji kulazwa, magari ya kutosha ya kubeba wagonjwa, huduma za hali ya juu kutoka kwa madaktari wenye uhakika wa kazi na maisha yao, na mambo mengine mengi tu ambayo yatakuwa yakiongezeka siku hadi siku hata kufikia kila hospitali siku moja kuwa na helikopta yake yenyewe na hata madaktari wa njiani au "paramedics"

Serikali kila mwaka katika bajeti yake isiyo na longolongo inakuwa inatenga fungu la kutosha kupitia wizara yake ya Afya ambayo inahakikisha fedha inakuwepo kwa hii bodi kwa ajili ya mishahara.

Kama kila mheshimiwa raisi aliepita na serikali yake na washauri wao mimi sijaona mambo haya isipokuwa kuwepo migomo au mawazo ya kutaka kugoma katika kila serikali hizi ambazo tokea uhuru hazijawa na ubunifu au hazijapanga vizuri mipango yenye kuleta maendeleo ambayo sisi wananchi tungeyaona.

Badala yake waheshimiwa maraisi wetu wote na viongozi wengine na washirika wao wamekuwa wakijisahau mara tu baada ya kutua Ikulu magogoni na wakipata tatizo la kiafya madaktari wao wanawashauri kuhusu hospitali za nje na wanakwenda kuangaliwa afya zao au kutibiwa huko.

Hizi hospitali za nje ya nchi haitoi huduma za bure, kuna pesa nyingi ya kutoka kwenye kodi za wananchi ndio zinalipwa kwa mfano katika hospitali za London Bridge na ile ya wanawake na watoto ya Portland zote za mjini London Uingereza, kuangaliwa tu afya, kufanyiwa uchunguzi, malazi, chakula na huduma nyingine tu za manesi kunaweza kugharimu si chini ya tshs 12,300,000 au £50,000 au zaidi kutegemea na urefu na namba ya siku kwa huduma hiyo.

Lakini mawazo yakitolewa kwamba nchi yetu ni tajiri wa kutupwa mpaka watu wanakufa njiani wakipita njia za mkato wakitafuta kuja kuishi na kujaribu kupora utajiri tulio nao lakini ambao hatuutumii, mawazo hayo yanaonekana ni ya kuleta vurugu na wanatafutwa watoaji wa mawazo hayo ili wang'olewe ukucha kavukavu.

Umefika wakati wa kukaa chini na kufikiri sana juu ya matatizo tuliyo nayo kwamba tumeyazoea au tumezoweshwa.

...
Kweli....
Ufikie muda sasa.. Tuitumikie nchi yetu.. Tusiidharau.. Lakini Richard, bodi zipo Na zinatoa mapendekezo mengi, Lakini kuna kiitikio toka serikalini..'SINA HELA'

Hii sina hela mpaka lini.. Serikali haikusanyi mapato Na inalalamika sina hela sasa nani akukusanyie mapato yako ee serikali..

Tukiachana na sekta ya madini, viwanda, mawasiliano, na nyinginezo

Tumulike kurunzi kwenye kijisekta kidogo cha usafiri

ukisoma jalada la Tanzania profile Dec 2005, nchi ilikadiriwa kuwa Na magari 382,000 Na Kwa kadirio la ongezeko la asilimia 17 hadi 18 Kwa mwaka..Na sasa inch inakadiriwa kuwa Na magari 1,204,000.

Tukiacha aina nyingine za kodi Na tuongelee road license tu ambayo ni lazima.. Magari madogo Hulipoa 130,000 Na penati ya 50,000 wakizidi grace time.. Mabasi Na magari mengine makubwa huenda zaidi ya milioni.. Na hapa hatujajumlisha magari ya serikali, jeshi au mashirika ya uma..

Tukichukulia wastani Wa 260,000 Tsh Kwa GARI tunapata zaidi ya billioni 313.. Hela hii inakusanywa?.. Au jibu ni mwekezaji?

Kila kitu siwezi, kila kitu sina pesa.. Halafu Mtu akisema hazina haina pesa, anapigiwa kelele za Kufa Mtu.. Kha sasa Kama hazina hela Ipo walipeni Basi waganga chao....'SINA PESA' .. Kujichanganya tu..

Serikali haikusanyi kodi , haiwazi njia za kutunisha kipato cha Taifa .. Inachojua ni kunyofoa kucha zetu Na meno yetu tisile nyama tena... AIBU
 
Last edited by a moderator:
Hili la bodi namaanisha taasisi ambayo ina wataalam (sio wa pale wizarani) hawa wanakuwa "independen"t na wanaaangalia kila kitu.

Mimi nataka pawepo ufanisi ambao utaonekana na madaktari watakuwa wakilipwa na pia kuwekwa kiwango maalum cha kuwalipa madaktari lakini wizara isihusike.

La pili kuhusu kodi, hio ipo wazi kwamba serikali haikusanyi kodi ipasavyo na inawaachia wale wote wanaofaidika na mfumo ambao umewekwa na serikali yenyewe.

TRA wanapaswa khakikisha wana taarifa za kila mwananchi na vyanzo yake vya pesa. Pia kama ulivyosema kuwa na taarifa za kumbukumbu za magari yote tena kukawa na integrated system inayoonyesha kwamba kodi imelipwa iwe na ushuru wa barabara, uingizaji wa gari, bima, MOT na hata mtu akiwa anashauku atapata jibu.

Sasa yote haya yanahitaji ubunifu na kujituma na kuwa tayari kuwatumikia wale waliokupa dhamana.

Hapo Eastern Europe nchini Poland wazungu wa nchi za magharibi walikuwa wakiziponda nchi za Ukraine na Poland kuhusiana na maandalizi ya mashindano ya Euro 2012 kwamba maandalizi yalikuwa mabovu na yalikuwa yakichelewa.

Lakini mji wa Warswa umebadilika ndani ya miezi 24 tu na kuna njia mpya za reli, uwanja mpya wa mpira, na barabara mpya na zenye kuvutia.

Uwanja mpya wa manispaa wa Poznan umejengwa kwa ubunifu na ufundi wa hali ya juu na kila mtu wa kutoka magharibi alikatwa ngebe kwa jinsi Ulaya mashariki inavyobadilika.

Sasa hawa watu nao wakati mwingine wanapata pesa kutoka kwa mkopo kutoka Eurozone na wakazitumia ipasanyo kwa kuweka mabo wazi, vipi sisi wenye kuzungukwa na utajiri wa kutupwa na tukawaachia wasiohusika na wkatoweka nao na hata kuficha Uswiss?

Wazo la kulipa kodi ni suala muhimu na ndilo lenye kuleta maendeleo mahali popote pale.
 
viumbe dizaini ya mbopo ndo ilitakiwa mnyofolewe kucha bila ganzi pumbafu wewe

Na wanyofoa kucha huwa wanajua nani wamnyofoe na kuharibu nyeti.

Huwezi kuninyamazisha kwa sababu eti ni fikra mbadala kwa sababu ya ukasuku wenu na ushabiki wa kisiasa. Madktari waliogoma tena kipumbavu kama hawa ni lazima waonyeshwe kwamba they are not indispensable na hiyo ni hata kama kutakuwa na gharama ya ziada kwa ajili ya kutetea principle. Mgomo ni haramu kwa sababu haukufuata taratibu za kisheria na vile vile madai ni ya kijinga na yasiyozingatia hali halisi ya uchumi. Kwa nini utumie bilioni zote hizo kulipa watu ambao hawastahili na ni watumishi kama wengine.

Kwa hiyo endeleeni kutukana kwa connivance ya moderator basi the truth remains that these ****** who listen to your asinine advice are wrong and are now left to consume a bread of sorrow and a drink of regret.
 
Craaaaaaaaaaaaaaap hakuna kitu hapo zaidi ya porojo tulizo kwisha zizoea. Mkuu wa nchi ameisha waambia kama wanaona mshahara wanao upata ni mdogo waache kazi, sasa shida iko wapi mpaka utokwe na povu lote hilo? mie nilitegemea uwahamasishe madaktari waache kazi na sio kuleta ***** humu ndani

we ndo umetoa crapiest isiyo na mfano kisa kamrija ka kunyonyea ulikopewa na mkuu wako wa kaya ndo kana kupa kiburi. Ole wenu siku zenu zilizombaya kwenu zaja mnatakiwa kutubu kwa watanzania ambao mmeendelea kuwashidndilia kwenye lindi la umaskini.

 
.... Eng Y BIHAGAZE umenena na sina haja ya kurudia..... kuna mengi na wakati mwingine napata hasira kuyaelezea....

naomba tujadili nini tufanye....muda wa kuzungumza umekwisha tunataka vitendo...
 
Mbopo

Tazama ramani ya AFRICA kuhusu migodi ya madini inayofanya kazi kwa mujibu wa ANGRO ASHANT, Tanzania ndio iko mingi inayofanya kazi ikifuatiwa na SA. Katika kile kinachopatikana Tanzania inapata mrahaba wa 3% na ni mikataba ya 100yrs jamani hapohapo wana Tax exemption (Capital allowance) ya miaka mitano. VENEZUELA mikataba yote kati ya serikali na wawekezaji kuna clauz ya kukatisha mkataba bila malipo ya fidia pindi utakapogundulika hauna maslahi ya chi yao. Tanzania waziri anasaini mkataba hotelini kashalala na malaya na pombe za kirusi usiku kucha kwa nini asisaini madudu??????????......

Toka kwenye box and think without bias, hii nchi yaweza kua katika level za nchi zinazochimba mafuta kama Libya. Uranium inakaribia kuanza kuchimbwa na Wamarekani sasa hebu katazame Mikataba ambayo CCM imeingia na wachimbaji (eti wawekezaji). Tuna gesi na makaa ya mawe hivi serikali inashindwa kuchukua msaada kwa minajiri ya kuwekeza katika sekta hizi (Government owned mines) na kufaidika kwa 100% ya rasilimali zetu?

TANZANIA IS A SLEEPING GIANT

Uranium haitachimbwa na Wamarekani,research then uje hapa utuandikie FACTS
 
Unazungumzia hazina bila kuzungumzia kilichopo. Unazungumzia potential wakati wenzie tunazungumzia hali ilivyo kwenye hazina yetu. Kama msingi wa mgomo wa watu hawa mnaowaita madktari ni wingi wa rasilimali bila extraction na bila kuangalia kinachoingia hazina then tunalo tatizo la kichwa hapa kwetu.

Kama ungekuwa unafuatilia mikataba ya sasa ungeelewa kwamba baada ya kugundulika tu, nchi iko entitled to 12.5% ya proceeds zote na hiyo ni kabla ya kuingiza USD 1.8 billion that would entitle us to 37% of the stakes. Kwa vile watu hapa ni activists ambao hawajali stats ndiyo maana wanapiga makelele. Hatujaambiwa kama madktari wa Venezuela au South Africa wanalipwa ngapi, na je ni sawa na aggregate ya TZS 7.5 million wanayodai hawa wauguzi (hawana sifa ya udaktari) wetu? Je adherence to professionl and ethical standards za doctors wa huko nje ni sawa na hawa wajawa tamaa wenu?

Maelezo uchwara ya wanaounga mkono vitendo vya wahuni hawa yanadhihirisha kwamba mgomomule haramu umechochewa na sababu nyingine ambazo si za kisheria wala za kimantiki. Hawa waganga wanajua kwamba serikali hulipa mishahara kutoka na vyanzo vyake ambavyo vinafahamika. Kama leo unazungumzia hazina ya samaki na dagaa wa ziwa tanganyika walioko mita elfu nne chini ya usawa wa bahari, au uranium ambayo haijaanza kuchimbwa na ile gesi iliyoko kilomita mbili chini ya sakafu ya bahari, kama ndiyo basis ya kuongezewa mishahara basi kumbe wao ni wagonjwa kuliko wale wnaowatibu kwenye ile wodi ya vichaa.

Muanzisha thread hii na wengine wote wanaotumia mgomo huu ku-settle political score hawazungumzii jinsi wahuni hawa walivyopuuza sheria na amti ya mahakama kuhusu uharamu wa mgomo huu. Lakini lords of impunity wanauchekea upuuzi huu. I say this is sheer non sense and tightly so!

Very funny! Mtu anasema anaweza kulipa tsh 15M kwa mwezi just because kuna Uranium ambayo haijaanza hata kuchimbwa!mafuta ambayo hayajaanza kuchimbwa! Fukuza hao wazungu tuone kama utachimba hio uranium na mafuta kwa nyundo na tindo zenu! Hamjui hata gharama ya EXPLORATION then unataka ugawane 50/50 na mtu aliyerisk ££billions! Explore na chimba mwenyewew utapata 100percent!
 
.... Eng Y BIHAGAZE umenena na sina haja ya kurudia..... kuna mengi na wakati mwingine napata hasira kuyaelezea....

naomba tujadili nini tufanye....muda wa kuzungumza umekwisha tunataka vitendo...

...
Kwanza serikali ifufue shirika la Simu, liendeshwa Kwa engo ya ishirini..

Ifufue TRA, iendeshwe Kwa engo ya Sabini..

Ifufue kilimo kijazie engo ya kumi ( ingawa kilimo kinaweza kwenda hadi engo ya 60..)

Mpaka hapo tumeshapata engo zetu Mia zenye lengo la bilioni 50,000 ( trillion 50. ) Kwa mwaka..

Kama haiwezekani wanipe mimi maeneo hayo tu niwaendeshee... kwanini kuwa waoga..!!TUNAWEZA..

Mawasiliano yakipewa jicho makini, ni muhimili tosha wa sekta nyingine kuegemea..
Hakuna mwekezaji hata mmoja atayeguswa Kwa mfumo huu, mwenyewe Kwa hiari atafungasha virago Na kuondoka manake biashara zitafanyika miongoni mwetu..
 
Watanzania wenzangu tuache siasa za ushabiki lakini tuangalie hali halisi. Kuwa na mito mingi na maziwa mengi bado hakujatoa jawabu la madaktari kutaka kulipwa sh 3,500,000 kwa mwezi. Tuna mambo mengi na muhimu zaidi ya kuwalipa madaktari. Hizo pesa wanazotaka hatuna na kama hawataki wafuge vilago wakatafute kazi sehemu nyingine.
 

Similar Discussions

29 Reactions
Reply
Back
Top Bottom