Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Polisi kutumia mamilioni ya fedha kukabili mauaji ya albino
Na Paulina David, Mwanza
JESHI la Polisi nchini, limetenga Sh20milioni kwa ajili ya kuwazawadia watu watakaotoa taarifa zitakazofanikisha kukamatwa kwa wauaji wa vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi (albino).
Mkuu wa jeshi la Polisi nchini,, Said Mwema aliyasema hayo jana wakati akizungumza na askari polisi wa jeshi hilo, maafisa wa polisi na waandishi wa habari jijini hapa.
Alisema fedha hizo, zimetengwa kwa ajili ya kutoa zawadi kwa watu watakaotoa taarifa za uhalifu hususan za mauaji ya albino na vikongwe yanayoendelea kutokea nchini.
Alisema lengo la kutoa fedha hizo, ni kuhakikisha vitendo vya mauaji ya vikongwe na albino, vinatokomezwa nchini.
Alisema mpango huo, utafanikiwa endapo polisi watapata taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa watu wanaopewa kazi ya kuwakata mapanga albino, ili kuchukua viungo vyao kutokana na imani za kishirikina.
Alisema endapo watuhumiwa watakamatwa, ni wazi kuwa watawataja watu ambao wamewakodisha kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.
Tunatambua kuwa wahalifu wana mbinu nyingi na siye tunapopanga mikakati ya kukabiliana nao, wao pia wanabuni mbinu nyingine, ili wananchi watusaidie kuwadhibiti wauaji hao, alisema Mwema.
Alisema katika Mkoa wa Mwanza vitendo vya kuwakata mapanga vikongwe, albino na ajali za barabarani zimekuwa tishio, hivyo jeshi hilo, linafanya kila jitihada za kuhakikisha vitendo hivyo vinadhibitiwa.
Timu ya watu kutoka makao makuu wakiwemo ofisi ya mkemia, usalama wa taifa, polisi waliobobea kwenye upelelezi, wanasheria wanatarajia kufika jijini hapa kwa ajili ya kuona jinsi ya kukabiliana na vitendo hivi, alisema.
Akizungumzia suala la askari polisi kujihusisha na vitendo vya rushwa kutokana na kutoboreshewa mazingira ya kazi, alisema kosa moja haliwezi kuhalalisha kosa jingine, hivyo askari anayetaka kula rushwa kwa kisingizio cha maslahi kidogo, anapaswa kuondoka kwenye jeshi hilo kwa kuwa hastahili.
Alifafanua kama askari mla rushwa atabainika, atafukuzwa kazi na kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria, hivyo asisubiri hadi afukuzwe kazi na badala yake ajiondoe mwenyewe.
My Take:
Hatua hii japo ni ya kupongezwa na iliyopaswa kutekelezwa muda uliopiga bado naamini haijaweza kubadilisha odds za usaliti. Kiasi kilichotengwa bado ni kidogo kuvutia tamaa ya watu. Lakini zaidi mgawanyo wa zawazi ni vizuri uwekwe hadharani.
Kwa mfano:
a. Ataketoa taarifa ya mfanyabiashara anayetumia viungo vya Albino na Mfanyabiashara huyo akatiwa mbaroni na hatimaye kukutwa na hatia basi mtoa taarifa atapata Tsh. milioni tano no questions asked
b. Atakayetoa taarifa ya mganga mwenye kuagiza matumizi ya viungo vya albino au kutangaza fulani ni mchawi au mwenye kushirikiana na wafanyabiashara wa aina hiyo na mganga huyo akanyakwa, naye anapata milioni 4
c. Mwenye kutoa taarifa itakayozuia jaribio la kudhuru, kushambulia au kumuua Albino au kikongwe yeyote huyo anazawadiwa milioni mbili!
n.k
Kwa kufanya hivyo tunabadilisha odds za maisha kwa ndugu zetu Albino. Nashukuru kwamba pendekezo hili ambalo lilitolewa na wenu mtiifu karibu mwaka mmoja baadaye limeanza kufanyiwa kazi. Hata hivyo zaidi inahitajika.
Mtu atajiuliza kati ya kutoa taarifa ya kuzuia mauaji ya albino na kucheza bahati nasibu ya simu n.k ni kipi kinalipa. Kama mshindi wa kupiga simu analipwa milioni 50 au kama huyo mwingine aliyepewa gari ya mamilioni hivi majuzi. Pamoja na zawadi hizo kubwa, ni vizuri pia kutoa zawadi nyingine ndogondogo kama motisha.
Vinginevyo, nawaunga mkono kwa hatua hii na ninapendekeza dau liongezwe hadi kufikia kama milioni 200 hivi.
Na zaidi nawasihi wabunge ambao walichangia karibu milioni 400 kuchangia tibu ya Taifa baada ya kuifunga Togo, wawe wa kwanza kuchangia mfuko huu wa Polisi na iundwe timu maalum (inayowakilisha maalbino, wanasheria na asasi za kidini) ambayo itasimamia utoaji wa zawadi hizi ili watu wengine wasije kuwa mafisadi wengine!
Na Paulina David, Mwanza
JESHI la Polisi nchini, limetenga Sh20milioni kwa ajili ya kuwazawadia watu watakaotoa taarifa zitakazofanikisha kukamatwa kwa wauaji wa vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi (albino).
Mkuu wa jeshi la Polisi nchini,, Said Mwema aliyasema hayo jana wakati akizungumza na askari polisi wa jeshi hilo, maafisa wa polisi na waandishi wa habari jijini hapa.
Alisema fedha hizo, zimetengwa kwa ajili ya kutoa zawadi kwa watu watakaotoa taarifa za uhalifu hususan za mauaji ya albino na vikongwe yanayoendelea kutokea nchini.
Alisema lengo la kutoa fedha hizo, ni kuhakikisha vitendo vya mauaji ya vikongwe na albino, vinatokomezwa nchini.
Alisema mpango huo, utafanikiwa endapo polisi watapata taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa watu wanaopewa kazi ya kuwakata mapanga albino, ili kuchukua viungo vyao kutokana na imani za kishirikina.
Alisema endapo watuhumiwa watakamatwa, ni wazi kuwa watawataja watu ambao wamewakodisha kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.
Tunatambua kuwa wahalifu wana mbinu nyingi na siye tunapopanga mikakati ya kukabiliana nao, wao pia wanabuni mbinu nyingine, ili wananchi watusaidie kuwadhibiti wauaji hao, alisema Mwema.
Alisema katika Mkoa wa Mwanza vitendo vya kuwakata mapanga vikongwe, albino na ajali za barabarani zimekuwa tishio, hivyo jeshi hilo, linafanya kila jitihada za kuhakikisha vitendo hivyo vinadhibitiwa.
Timu ya watu kutoka makao makuu wakiwemo ofisi ya mkemia, usalama wa taifa, polisi waliobobea kwenye upelelezi, wanasheria wanatarajia kufika jijini hapa kwa ajili ya kuona jinsi ya kukabiliana na vitendo hivi, alisema.
Akizungumzia suala la askari polisi kujihusisha na vitendo vya rushwa kutokana na kutoboreshewa mazingira ya kazi, alisema kosa moja haliwezi kuhalalisha kosa jingine, hivyo askari anayetaka kula rushwa kwa kisingizio cha maslahi kidogo, anapaswa kuondoka kwenye jeshi hilo kwa kuwa hastahili.
Alifafanua kama askari mla rushwa atabainika, atafukuzwa kazi na kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria, hivyo asisubiri hadi afukuzwe kazi na badala yake ajiondoe mwenyewe.
My Take:
Hatua hii japo ni ya kupongezwa na iliyopaswa kutekelezwa muda uliopiga bado naamini haijaweza kubadilisha odds za usaliti. Kiasi kilichotengwa bado ni kidogo kuvutia tamaa ya watu. Lakini zaidi mgawanyo wa zawazi ni vizuri uwekwe hadharani.
Kwa mfano:
a. Ataketoa taarifa ya mfanyabiashara anayetumia viungo vya Albino na Mfanyabiashara huyo akatiwa mbaroni na hatimaye kukutwa na hatia basi mtoa taarifa atapata Tsh. milioni tano no questions asked
b. Atakayetoa taarifa ya mganga mwenye kuagiza matumizi ya viungo vya albino au kutangaza fulani ni mchawi au mwenye kushirikiana na wafanyabiashara wa aina hiyo na mganga huyo akanyakwa, naye anapata milioni 4
c. Mwenye kutoa taarifa itakayozuia jaribio la kudhuru, kushambulia au kumuua Albino au kikongwe yeyote huyo anazawadiwa milioni mbili!
n.k
Kwa kufanya hivyo tunabadilisha odds za maisha kwa ndugu zetu Albino. Nashukuru kwamba pendekezo hili ambalo lilitolewa na wenu mtiifu karibu mwaka mmoja baadaye limeanza kufanyiwa kazi. Hata hivyo zaidi inahitajika.
Mtu atajiuliza kati ya kutoa taarifa ya kuzuia mauaji ya albino na kucheza bahati nasibu ya simu n.k ni kipi kinalipa. Kama mshindi wa kupiga simu analipwa milioni 50 au kama huyo mwingine aliyepewa gari ya mamilioni hivi majuzi. Pamoja na zawadi hizo kubwa, ni vizuri pia kutoa zawadi nyingine ndogondogo kama motisha.
Vinginevyo, nawaunga mkono kwa hatua hii na ninapendekeza dau liongezwe hadi kufikia kama milioni 200 hivi.
Na zaidi nawasihi wabunge ambao walichangia karibu milioni 400 kuchangia tibu ya Taifa baada ya kuifunga Togo, wawe wa kwanza kuchangia mfuko huu wa Polisi na iundwe timu maalum (inayowakilisha maalbino, wanasheria na asasi za kidini) ambayo itasimamia utoaji wa zawadi hizi ili watu wengine wasije kuwa mafisadi wengine!
Last edited by a moderator: