Tsd majukumu yake ni yapi?

segwanga

JF-Expert Member
Mar 16, 2011
2,789
729
Wadau heshma kwenu
Nimepewa assignment na katibu wa mnoko wa Teachers service department (TSD) wa pande nilipo eti hawezi kupokea fomu zangu za kuomba tsd namba bila kujua majukumu ya tsd.Great thinkers nisaidieni
 
ni taasisi ndani ya wizara ya elimu.
1.kumfukuza na kumwajiri mwalimu kazi
2.kumsimamisha mwalimu kazi au kumpa nusu mshahara.
3.inaongeza vyeo vya walimu na kupandisha mishahara
4.kuingia mkataba na walimu wapya kwa niaba ya serikali.
kwa ufupi ndivyo niujuavyo.mia
 
figganiga upo sawa. tatizo nini segwanga?? pia tafuta public service act itakusaidia kujua taratibu nzima za utumishi wa umma.
 
ni taasisi ndani ya wizara ya elimu.
1.kumfukuza na kumwajiri mwalimu kazi
2.kumsimamisha mwalimu kazi au kumpa nusu mshahara.
3.inaongeza vyeo vya walimu na kupandisha mishahara
4.kuingia mkataba na walimu wapya kwa niaba ya serikali.
kwa ufupi ndivyo niujuavyo.mia
Haipo chini ya Wizara ya Elimu bali ni Idara ndani ya Ofisi ya Rais-Tume ya Utumishi wa Umma.
Kazi zake zipo kwenye Public Service Act ya 2002 as amended in 2008, Kanuni za Utumishi za mwaka 2003 na Teachers Scheme of service.
1.Kusajili Walimu (waliosoma na kufuzu)
2.Kushughulikia masuala ya nidhamu na maadili ya watumisihi wa kada ya ualimu
3.Kushughulikia mambo ya mirathi za walimu
4.Kuandaa na kutunza tange (seniority list) ya walimu wote waliopo katika utumishi wa umma.
5.Kupandisha walimu vyeo kwa kadri ya bajeti na mapendekezo ya mwajiri kupitia vikao vya kisheria
 
mkuu Gerrard asante kwa kunifumbua macho.mimi nilikua naijua jujuu.ni aktika hali ya kupeana mwanga.hata wewe upo sahihi kabisa.ngoja niendelee kufuatilia mambo yao.asante sana.mia
 
  • Thanks
Reactions: SG8
Greater thinkers nawashukuru na nitaendelea kuwashukuru kwa michango yenu.Niende mbele kidogo kwa kuelezea kisa cha mimi kuambiwa mpaka nijue majukumu ya tsd ndio fomu zangu zipokelewa.
Nilienda ofsi za tsd nikiwa nimevaa t-shirt (nzuri tu) na suruali ya kadet (nzuri pia) na ndipo msala ulianzia hapo. Nikaambiwa hayo mavazi hayatakiwi kwa mtumishi wa serikali.Mi nikajitetea nikasema ninapokuwepo kazn kwangu sivai hvyo.Akaniambia hata hapo (ofsi za tsd) niko ofsin kwangu na mm nikamkatalia na ndo chanzo cha kutoelewana.Wadau tuhabarishane hilo ni kosa?
 
Greater thinkers nawashukuru na nitaendelea kuwashukuru kwa michango yenu.Niende mbele kidogo kwa kuelezea kisa cha mimi kuambiwa mpaka nijue majukumu ya tsd ndio fomu zangu zipokelewa.
Nilienda ofsi za tsd nikiwa nimevaa t-shirt (nzuri tu) na suruali ya kadet (nzuri pia) na ndipo msala ulianzia hapo. Nikaambiwa hayo mavazi hayatakiwi kwa mtumishi wa serikali.Mi nikajitetea nikasema ninapokuwepo kazn kwangu sivai hvyo.Akaniambia hata hapo (ofsi za tsd) niko ofsin kwangu na mm nikamkatalia na ndo chanzo cha kutoelewana.Wadau tuhabarishane hilo ni kosa?
Mkoa gani huo Mkuu? Hata hivyo jambo la msingi sio mavazi ya kiofisi ila mavazi rasmi na T-shirt sio vazi rasmi labda kwa watu kama bank na NSSF kuna siku kama Ijumaa au J'mosi wanavaa T-shirt (sare). Kuna waraka wa mavazi kwa mtumishi wa umma, tafuta na usome utajua kwanini huyo Katibu alikusumbua. Kuna Mwalimu alikwenda kwenye semina ya kusimamia mitihani ya darasa la saba akiwa na rasta jamaa wakambana sana. Alijitetea akidai ni dini yake, Afisa Elimu kimya kimya akfuatilia mkataba aliojaza akiwa wilaya nyingine ikathibitika jamaa alijaza dini yake kama Mkristo basi ikala kwake
 
Back
Top Bottom