Elvis Legacy
JF-Expert Member
- Aug 10, 2017
- 3,385
- 4,711
Habari wakuu.
Kulingana na ukweli kuwa Demokrasia ya Marekani ni tofauti sana na yetu ambapo matokeo ya Urais yanaamuliwa na Electoral college votes, kwenye majimbo 50 kila jimbo linakuwa na namba ya Electoral collage votes kulingana na idadi ya raia katika jimbo(state) husika.
Ili uwe mshindi ni sharti upate Electoral college votes 270. Endapo mtalingana basi maamuzi yatafanywa na House of Representatives kwa Rais na Senate kwa makamu wa Rais.
Mpaka sasa Joe Biden wa Democrat ana Electoral college votes 238 wakati Donald Trump wa Republican ana Electoral college votes 214.
Joe Biden anahitaji Electoral college votes 32 ili aweze kuwa Rais mpya wa marekani ambapo anategemea majimbo hayo matatu, Nevada, Wisconsin na Michigan ambayo yana jumla ya Electoral college votes 32. Mpaka sasa anaongoza kwenye kura za wananchi kwenye majimbo hayo japo Trump anamfukuzia kwa ukaribu sana.
Kura za wananchi hazina maamuzi ya nani atakuwa Rais maana hata Hillary Clinton alishinda kwa kura zaidi ya milioni tatu lakini Trump alishinda hizo za Electoral college votes na kuwa Rais.
Lolote linaweza kutokea Marekani. Japo Trump ameshaanza kulalamika kuibiwa kura.
Kulingana na ukweli kuwa Demokrasia ya Marekani ni tofauti sana na yetu ambapo matokeo ya Urais yanaamuliwa na Electoral college votes, kwenye majimbo 50 kila jimbo linakuwa na namba ya Electoral collage votes kulingana na idadi ya raia katika jimbo(state) husika.
Ili uwe mshindi ni sharti upate Electoral college votes 270. Endapo mtalingana basi maamuzi yatafanywa na House of Representatives kwa Rais na Senate kwa makamu wa Rais.
Mpaka sasa Joe Biden wa Democrat ana Electoral college votes 238 wakati Donald Trump wa Republican ana Electoral college votes 214.
Joe Biden anahitaji Electoral college votes 32 ili aweze kuwa Rais mpya wa marekani ambapo anategemea majimbo hayo matatu, Nevada, Wisconsin na Michigan ambayo yana jumla ya Electoral college votes 32. Mpaka sasa anaongoza kwenye kura za wananchi kwenye majimbo hayo japo Trump anamfukuzia kwa ukaribu sana.
Kura za wananchi hazina maamuzi ya nani atakuwa Rais maana hata Hillary Clinton alishinda kwa kura zaidi ya milioni tatu lakini Trump alishinda hizo za Electoral college votes na kuwa Rais.
Lolote linaweza kutokea Marekani. Japo Trump ameshaanza kulalamika kuibiwa kura.