sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,026
Hakuna rais anaechezewa Rafu mbaya sana kama Trump, Ila cha kushangaza ni Kwamba Rais huyu huibuka kidedea na kuwaacha wengi midomo wazi ni vipi na kawezaje kuhimili mishale mingi kiasi hiki.
Siri ni Moja Tu, Trump Anamtanguliza sana mungu ambae ni Mwema mwenye rehema, Asiepatwa na usingizi waa kuchoka kutujali na Mwepesi wa kutusamehe Dhambi zetu tunapozitubu Mbele yake
Sio kitu kigeni kwa Trump kuwa muumini mzuri tu wa ukristo, Wachungaji wameenda ikulu kumuombea, Alisikitishwa sana na kitendo cha kanisa kuchomwa moto, Ni mhudhuriaji wa kanisani na anamsifu Mungu.
Ni majuzi hapo kaweka wazi hii Dunia tuwe kwenye Mateso ama bila Mateso bado msaada wa bosi hauepukiki na hakuna mtu maarufu kama Yesu.