Sam Gidori
Senior Member
- Sep 7, 2020
- 165
- 414
Aliyekuwa Rais wa Marekani, Donald Trump amemtaka mrithi wake, Joe Biden ajiuzulu baada ya wanamgambo wa Taliban kudhibiti Mji Mkuu wa Afghanistan, Kabul, pamoja na Ikulu ya Rais siku ya Jumapili.
Trump amemlaumu Biden kwa ‘kuruhusu’ Wataliban kutawala Afghanistan katika ushindi mwanana licha ya uwepo wa wanajeshi wa Marekani nchini humo kwa zaidi ya miaka 20.
Wanamgambo wa Taliban wamechukua udhibiti wa Mji Mkuu ikiwa ni wiki mbili kabla ya tarehe ya mwisho iliyowekwa na Jeshi la Marekani kukamilisha kuwaondoa wanajeshi wake wote nchini humo - Agosti 31. Hata hivyo, mipango ya kuwaondoa wanajeshi wa Marekani ilianza wakati wa utawala wa Trump kwa makubaliano yaliyosainiwa Doha, nchini Qatar, mwezi Februari mwaka 2020, kwa makubaliano ya kuwaondoa wanajeshi wote wa Marekani ifikapo mwishoni mwa mwezi Mei, huku Wataliban wakitakiwa kukidhi vigezo kadhaa ikiwamo kuvunja uhusiano na Al Qaeda.
Baada ya Biden kuchukua madaraka, alisogeza mbele tarehe ya mwisho ya Marekani kuondoa uwepo wake nchini humo kufikia mwezi Agosti bila kuweka masharti yoyote. Trump anamlaumu Biden, akidai Marekani ingeweza kujiondoa kwa njia nzuri zaidi na yenye mafanikio.
“Alichokifanya Biden kitabaki kama moja ya maanguko mabaya zaidi katika historia ya Marekani,” Trump alisema siku ya Jumapili.
Kwa sasa, Marekani ipo katika hatua za dharura kuwaondoa wafanyakazi katika ubalozi wake mjini Kabul, ikiwa ni chini ya mwezi mmoja tu tangu Biden aliposema kuwa Wataliban hawataweza kuchukua utawala wa Afghanistan na kuwa serikali na jeshi la Afghanistan lipo imara dhidi ya Taliban.
Chanzo: AFP
Wanamgambo wa Taliban wameitangaza Afghanistan rasmi kuwa "Ufalme wa Kiislamu wa Afghanistan" (Islamic Emirate of Afghanistan) baada ya kuteka Ikulu ya Rais. [Picha na AP]
Trump amemlaumu Biden kwa ‘kuruhusu’ Wataliban kutawala Afghanistan katika ushindi mwanana licha ya uwepo wa wanajeshi wa Marekani nchini humo kwa zaidi ya miaka 20.
Wanamgambo wa Taliban wamechukua udhibiti wa Mji Mkuu ikiwa ni wiki mbili kabla ya tarehe ya mwisho iliyowekwa na Jeshi la Marekani kukamilisha kuwaondoa wanajeshi wake wote nchini humo - Agosti 31. Hata hivyo, mipango ya kuwaondoa wanajeshi wa Marekani ilianza wakati wa utawala wa Trump kwa makubaliano yaliyosainiwa Doha, nchini Qatar, mwezi Februari mwaka 2020, kwa makubaliano ya kuwaondoa wanajeshi wote wa Marekani ifikapo mwishoni mwa mwezi Mei, huku Wataliban wakitakiwa kukidhi vigezo kadhaa ikiwamo kuvunja uhusiano na Al Qaeda.
Baada ya Biden kuchukua madaraka, alisogeza mbele tarehe ya mwisho ya Marekani kuondoa uwepo wake nchini humo kufikia mwezi Agosti bila kuweka masharti yoyote. Trump anamlaumu Biden, akidai Marekani ingeweza kujiondoa kwa njia nzuri zaidi na yenye mafanikio.
“Alichokifanya Biden kitabaki kama moja ya maanguko mabaya zaidi katika historia ya Marekani,” Trump alisema siku ya Jumapili.
Kwa sasa, Marekani ipo katika hatua za dharura kuwaondoa wafanyakazi katika ubalozi wake mjini Kabul, ikiwa ni chini ya mwezi mmoja tu tangu Biden aliposema kuwa Wataliban hawataweza kuchukua utawala wa Afghanistan na kuwa serikali na jeshi la Afghanistan lipo imara dhidi ya Taliban.
Chanzo: AFP