Trump aendelea kukubalika licha ya kuziita nchi za Afrika 'sithole'

FikraPevu

JF-Expert Member
Jan 2, 2010
303
236
Licha ya Rais wa Marekani, Donald Trump kutoa kauli ya kibaguzi dhidi ya nchi za Afrika, inaelezwa kuwa bado wananchi wa bara hilo wanaukubali uongozi wa rais huyo.

Wakati akiingia madarakani mwaka 2016, Rais Trump aliahidi kutekeleza sera za kimataifa za kujitenga na kutanguliza maslahi ya Marekani mbele ambapo siku chache zilizopita alishangaa Marekani kupokea wahamiaji kutoka katika nchi za Afrika huku akitumia neno ‘shithole’ (tundu la choo) akimaanisha ni nchi za Afrika Haiti na El Salvador na kwamba Marekani haihitaji wahamiaji kutoka katika nchi hizo, badala yake inataka wahamiaji kutoka Norway.

Dunia imesimama na kupinga sera za Trump na kuitaka Marekani kuheshimu misingi ya demokrasia ili kudumisha diplomasia na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa.

Kura ya maoni iliyoratibiwa na mtandao wa Gallup (2018) inaonyesha nchi za Afrika zina ukubali kwa asilimia 51 utawala wa Marekani unaongozwa na Rais Trump dhidi ya asilimia 20 ambao hawaukubali.

Hata hivyo, kukubalika kwa utawala wa Marekani kumeshuka kwa asilimia 10 katika nchi 11 za Afrika na inatabiriwa kuwa kukubalika huko kutashuka zaidi siku zijazo ikiwa Trump ataendelea kutekeleza sera za kibaguzi dhidi ya mataifa ya Afrika.

Kura hiyo ambayo ilishirikisha watu 1,000 kutoka nchi 134 ili kufahamu maoni yao juu ya utawala wa Ujerumani, Marekani, Urusi na China, ilibaini kuwa kukubalika kwa Marekani chini ya Trump kumeshuka kwa pointi 18 ukilinganisha na uongozi wa Barack Obama. Trump alipata asilimia 43 nyuma ya uongozi wa Vladimir Putini wa Urusi na Xi Jinping wa China.

Sababu kubwa ya Trump kutokukubalika ni hatua yake ya kuimarisha mahusiano na Israel ukilinganisha mtangulizi wake Obama ambaye hakuonyesha waziwazi kuisaidia nchi hiyo. Ikumbukwe kuwa Trump alikuwa Rais wa kwanza kulitambua jiji la Yerusalemu kuwa mji mkuu wa Israeli na kutangaza kuhamishia ubalozi wa Marekani kutoka Tel Aviv hadi katika jiji hilo.

Zaidi, soma hapa => Trump aendelea kukubalika Afrika, kauli ya ‘Sithole’ yazua mjadala kila kona | FikraPevu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom