True story: Nimeamua kumkataa mtoto rasmi

Naunga mkono hoja, mara nyingi sisi wanaume huwa tunakosa maamuzi halafu tunasingizia limbwata. Mtoa mada tangu aliposhtukia kuhusu mimba ya kwanza ilipotolewa angechukua hatua ngumu haya yote yasingetokea
Alafu mwandishi anataka tumpongeze,hataki kukubali kuwa kuna sehemu anakwama
 
Haya mambo wanaume karibu wote hututokea ila wengine tukishaona dalili tu za kugeuzwa boya huwa tunaacha kimoja sasa sijui mleta mada akifeli wapi
Wakati yanatokea nilikuwa na umri mdogo kuyajua haya
 
Aliyeisoma yote na vipande vyake, anisaidi kuniwekea summary hapa chini. Nina njaa na hii story ilivyo ndefu naweza zimia sijamaliza yote
 
Mimi naona wote mlikuwa na matatizo, ulipooa na mke kuwa mbali kikazi ulitakiwa upange jinsi ya kukufana zamu za kutembeleana, kingine kushindwa kulipa mahali kitakuwa kilikwaza familia ya upande wa mke, kingine nilichokuona nacho ulipenda kuoa mke wa kuwa naye karibu akupikie na kukufulia hivyo huyo mwanamke hakuwa anakufaa, kwasasa umeshamove on kaa na familia uliyonayo Sasa huyo mtoto mwache mama yake aamue aishije hasa kuishi kwa Bibi ni vizuri kuliko kuishi na mama anayeshinda kazini na ujana bila mtu wa kumdhibiti kurudi nyumbani mapema kuhusu kulelewa na mama wa kambo hata hilo siyo jema, mwache huko kwa mama yake.
 
Mkuu naona mambo mengi uliyo yapitia yanafanana kabisa na mambo ambayo nilipitia mm pia mda hui
Kama yanafanana sana pitia ushauri wa wadau humu ufanye haraka, ushauri huo haunisaidii mimi sababu yalitokea siku zilizopita na wanachoshauri nilishakifanya
Kwa ambae anapitia sasa ndio wakati wa kuutumia
 
Mimi naona wote mlikuwa na matatizo, ulipooa na mke kuwa mbali kikazi ulitakiwa upange jinsi ya kukufana zamu za kutembeleana, kingine kushindwa kulipa mahali kitakuwa kilikwaza familia ya upande wa mke, kingine nilichokuona nacho ulipenda kuoa mke wa kuwa naye karibu akupikie na kukufulia hivyo huyo mwanamke hakuwa anakufaa, kwasasa umeshamove on kaa na familia uliyonayo Sasa huyo mtoto mwache mama yake aamue aishije hasa kuishi kwa Bibi ni vizuri kuliko kuishi na mama anayeshinda kazini na ujana bila mtu wa kumdhibiti kurudi nyumbani mapema kuhusu kulelewa na mama wa kambo hata hilo siyo jema, mwache huko kwa mama yake.
Mkuu suala la kutembeleana na kutoa mahari ni vitu vimetokea ndani ya muda mfupi sana

Yaani mfunge ndoa mwezi wa nane halafu mwezi wa kumi unaanza kuhisi tofauti, mahari ingetolewa wakati gani?

Baada ya kuona mambo sio mambo ndio nikaghairi kabisa kutoa mahari labda hilo liliwakwaza yawezekana hawakujua kwanini sikutoa na ni kwa sababu hawakujishughulisha kujua tatizo

Kwa taarifa yako miaka yote hii zaidi ya saba na masekeseke yote hakuna ndugu upande wao alipiga simu kwangu au kuniita zaidi ya mjomba wake aliposikia nakwenda mahakamani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom