mkorinto
JF-Expert Member
- Jun 11, 2014
- 30,699
- 37,296
SEHEMU YA 8
nikiwa natafakari nini nifanye,ndoo iko njiani mercury imejaa ni nzito haitikisiki.nikasikia ngoma zinapunguzwa mlio,ishara ya babu kuachwa aongee na bibi mtunza mercury.
nikashusha pumzi na kujaribu kuisogeza upya ndoo ile.ajabu safari hii wala haikuwa nzito nilifanikiwa kuinyanyua.nikaisogeza kwa kupitia njia moja wapo ya mlango wa pango na kujibanza nayo pembeni nisubiri nini kitatokea,nikazima tochi.
baada ya dakika kadhaa nikasikia vishindo na mwanga wa kienge kama mtu anaingia ndani,nikajua ni yule babu karuhusiwa kuingia kukinga tone kama kawaida,wasi wasi ukawa atakuja upande niliopo au atapita mlango mwingine!!!nikiwa sielewi nikajipa ujasiri na kuwa mtulivu.nikashtuka kwamba babu anakuja upande niliopo,kikajua leo mambo yashakiwa magumu,anyway sio ishu huu ni utafutaji hata akinikuta ananijua na anaijua nia yangu.ajabu baba alifika mpaka pale hakuniona pamoja na mimi kujirishidha kwamba sikuwa nimejificha kiasi hicho,akapitiliza.hapo nikachoka,kiasi ujasiri niliokuwa nao ukageuka na kuanza kuwa hofu nzito,hata ile kiu ya mercury ikaanza kutoweka.nikaanza kuwaza kurudi nyumbani,ghafla mzee akawa anageuza kutoka,nikafikiria kuungana naye,lakini wacha nichukue na ndoo yangu,ajabu ndoo ikawa nzito kama awali,na mzee anazidi kuchanja mbuga kuelekea nje.nikaona wacha niachane nayo nitoke ile napiga hatua ya kwanza tu nikashikwa mkono na mtu nisiyemjua wala kumwona,nikaanza kuishiwa nguvu tena,najaribu kuwasha tochi lakini haina ushirikiano,nimeanza kutetemeka na kuhema kwa pupa,fahamu zikanitoka.
nikaja kushtuka nipo jirani na chupa,inaonekana sababu ya mwanaga wa michirizi myekundu inayoangusha matone yale yanayosubiriwa siku kadhaa.akili ikaanza kuwaza,hii ya kwenye ndoo ni tofauti na hii ama nini maana ya kufanyiwa haya!!!
nikiwa nimeanza kupiteza nuru ya matumaini,maswali yakaanza kunijia,aliyenishika ni nani???nibyule joka aliyenitoa nje na kuongea na mimi ama mzimu mwingine!!!taratiibu nikaanza kukumbuka fadhira za yule joka,tuliongea,tukawasiliana,akanibeba mpaka nje,hakuruhusu nibabaike.taratiibu nikaanza kujisikia huzuni na kujutia maamuzi yangu,kwanini sikufata utaratibu wa wazee wale wa kijijini!!!nikaanza kuichukia pesa.
wazo likanijia,nikaita kilugha (bibi),kimyaaa sana bila majibu zaidi ya mwangwi.
nikajiuliza kwanini hata popo hawajatawanyika kama mwanzo??kwani nimekuwaje??nimekufa au nimefanywaje???
itaendelea............
nikiwa natafakari nini nifanye,ndoo iko njiani mercury imejaa ni nzito haitikisiki.nikasikia ngoma zinapunguzwa mlio,ishara ya babu kuachwa aongee na bibi mtunza mercury.
nikashusha pumzi na kujaribu kuisogeza upya ndoo ile.ajabu safari hii wala haikuwa nzito nilifanikiwa kuinyanyua.nikaisogeza kwa kupitia njia moja wapo ya mlango wa pango na kujibanza nayo pembeni nisubiri nini kitatokea,nikazima tochi.
baada ya dakika kadhaa nikasikia vishindo na mwanga wa kienge kama mtu anaingia ndani,nikajua ni yule babu karuhusiwa kuingia kukinga tone kama kawaida,wasi wasi ukawa atakuja upande niliopo au atapita mlango mwingine!!!nikiwa sielewi nikajipa ujasiri na kuwa mtulivu.nikashtuka kwamba babu anakuja upande niliopo,kikajua leo mambo yashakiwa magumu,anyway sio ishu huu ni utafutaji hata akinikuta ananijua na anaijua nia yangu.ajabu baba alifika mpaka pale hakuniona pamoja na mimi kujirishidha kwamba sikuwa nimejificha kiasi hicho,akapitiliza.hapo nikachoka,kiasi ujasiri niliokuwa nao ukageuka na kuanza kuwa hofu nzito,hata ile kiu ya mercury ikaanza kutoweka.nikaanza kuwaza kurudi nyumbani,ghafla mzee akawa anageuza kutoka,nikafikiria kuungana naye,lakini wacha nichukue na ndoo yangu,ajabu ndoo ikawa nzito kama awali,na mzee anazidi kuchanja mbuga kuelekea nje.nikaona wacha niachane nayo nitoke ile napiga hatua ya kwanza tu nikashikwa mkono na mtu nisiyemjua wala kumwona,nikaanza kuishiwa nguvu tena,najaribu kuwasha tochi lakini haina ushirikiano,nimeanza kutetemeka na kuhema kwa pupa,fahamu zikanitoka.
nikaja kushtuka nipo jirani na chupa,inaonekana sababu ya mwanaga wa michirizi myekundu inayoangusha matone yale yanayosubiriwa siku kadhaa.akili ikaanza kuwaza,hii ya kwenye ndoo ni tofauti na hii ama nini maana ya kufanyiwa haya!!!
nikiwa nimeanza kupiteza nuru ya matumaini,maswali yakaanza kunijia,aliyenishika ni nani???nibyule joka aliyenitoa nje na kuongea na mimi ama mzimu mwingine!!!taratiibu nikaanza kukumbuka fadhira za yule joka,tuliongea,tukawasiliana,akanibeba mpaka nje,hakuruhusu nibabaike.taratiibu nikaanza kujisikia huzuni na kujutia maamuzi yangu,kwanini sikufata utaratibu wa wazee wale wa kijijini!!!nikaanza kuichukia pesa.
wazo likanijia,nikaita kilugha (bibi),kimyaaa sana bila majibu zaidi ya mwangwi.
nikajiuliza kwanini hata popo hawajatawanyika kama mwanzo??kwani nimekuwaje??nimekufa au nimefanywaje???
itaendelea............