Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,893
- 940
Treni ya Mwendokasi Kutoka Dar es Salaam - Morogoro Kuanza Safari Mwezi Julai 2023
Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Atupele Mwakibete amesema safari za treni ya mwendokasi (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro zitaanza Julai mwaka huu.
Mwakibete ameyasema hayo Alhamisi Juni mosi 2023 wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Khadija Hassan Aboud. Aidha, Mwakibete amesema Juni yatawasili mabehewa yenye ghorofa huku vichwa vya treni hiyo vikitarajiwa kuwasili Julai.