JEKI
JF-Expert Member
- Aug 16, 2013
- 4,846
- 2,936
Ndugu zangu mimi ni mkazi inapopita treni ya daladala ya tazara, treni hii imegeuka kero kwa wakazi inamopita, yaani treni inapiga mahoni yasiyokuwa na kichwa wala miguu, njia nzima ni mahoni tuuu, likipita saa 11 asubuhi ni mahoni unaamka kichwa chakuuma, hadi unajiuliza lengo ni nini?
Yaani inakuwa lengo ni kutuamsha au kutuletea kero tu, maana wasafiri wanajua ratiba tayari, ya nini kuamshana kuja kupanda, hivi madereva wa gari nyie mnapiga honi kila wakati? mimi sikumbuki mara ya mwisho kupiga honi, sasa kama gari ni ngumu kupiga honi, treni ambayo barabara yake inaheshimika itakuwaje?
Pia honi ya treni inatembea kilomita nyingi sana, kiasi kwamba kwa njia ya tazara ingetakiwa kupiga honi mara 3 tu na kila mtu anajua inakuja, sasa utakuta hata hakuna mtu njiani linapiga honi tu.
Sijui haka kadereva wamekatoa wapi tu, zamani haikuwa hivi.
Yaani inakuwa lengo ni kutuamsha au kutuletea kero tu, maana wasafiri wanajua ratiba tayari, ya nini kuamshana kuja kupanda, hivi madereva wa gari nyie mnapiga honi kila wakati? mimi sikumbuki mara ya mwisho kupiga honi, sasa kama gari ni ngumu kupiga honi, treni ambayo barabara yake inaheshimika itakuwaje?
Pia honi ya treni inatembea kilomita nyingi sana, kiasi kwamba kwa njia ya tazara ingetakiwa kupiga honi mara 3 tu na kila mtu anajua inakuja, sasa utakuta hata hakuna mtu njiani linapiga honi tu.
Sijui haka kadereva wamekatoa wapi tu, zamani haikuwa hivi.