Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuongea sio kazi saana. Tunaomba mchanganuo hasara hiyo inasababishwa na nini na inatokeaje. Msituletee mambo ya kijinga kila sehemu. Msifikiri tunafurahi shida tunazipata sisi wao wanakula per day tu, na huku watu wengine wanawabwetere kila siku.
kwa mujibu wa katiba ya jamuhuri ya muungano wa tanzania ya mwaka 1977
sehemu ya 3 haki na uhuru wa mawazo kifungu cha 18(1)
kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake....
sidhani kama mbunge alikuwa na nia mbaya kwa usafiri huu wa treni wakati mwingine kukosoa ni namna nyingine ya kuweka sawa au kutaka jambo liwe sawa . sijui kwa nini watu wamechukulia vibaya namna hiyo.
Watanzania kwa kutoa tathmini ni mabingwa sana. Ww kama mtanzania umefanya nn kuondoa tatizo?
Haka katoto (i.e. Mnyika) wakati mwingine kanatakiwa kupigwa "Makwenzi" tu............
Aliwahi kutuma taarifa hii kwetu: Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo: Mnyika- Majaribio Ya Usafiri Wa Treni DSM Ni Hatua Muhimu
Inaonyesha aunga mkono, anachotaka ni maboresho.
PM
Nimekumbuka msemo wa masaburi 'viongozi(wabunge ) wa dar wanafikiria kwa kutumia makalio'
Tusimukumu mnyika labda amefanya cost-benefit analysis.pia mali ya umma inafanywa shamba la bibi ktk utawala wa CCM.
... Ametoa taarifa mapema ili hasara isiendelee, hadi serikali ijipange kuiendesha project kibiasharaWatanzania kwa kutoa tathmini ni mabingwa sana. Ww kama mtanzania umefanya nn kuondoa tatizo?
Nathubutu kusema huyo mbunge ni mp.....mbavu,na mjue kuwe kuanza kula hasara mwanzoni sio tatizo,angalieni makampuni makubwa kama google,amazon,etc nyingi zilianza kula hasara for over 5 years mpaka zikaja kupost profit na kuwa mega companies,hilo lilikuwa wazo la waziri kutaka kupunguza tatizo,suala la utendaji,mkurugenzi wa trc si yupo?yeye ndio anatakiwa atoe mchanganuo wa namna ya kuendeleza huo usafiri uje kuwa profitable,huyo mbunge wa ubungo inaonyesha uwezo wake wa kufikiri kwa sababu asijaribu kujitoa hapo kwani yeye sio serikali?yeye akiwa kama kiongozi ametoa ushauri gani ili kuboresha?hii inaonyesha ana upeo finyu wa kufikiri.yeye alitoa wazo gani ili kupunguza tatizo la usafir?ama kajiona baada ya kukaa kwa dakika kadhaa na watu wake akinywa kahawa na kucheza bao anaona aikandie serikali,,mbunge wa ubungo chapa kazi,leta mawazo chanya katika kuboresha usafiri wa treni ama furaha yako ni kuona usafiri wa treni unakufa na wananchi wanarudi katika matatizo yao?samahani kama nimewaudhi lakini penye ukweli yatubidi tuseme ukweli
Humu vijana wetu wangekuwa wanapita mbona wangekuwa wanafaulu maana wanapata practical training na wakichanganya na za kwao wanatoka na kitu kizuri, nimependa maoni yako ila bado na maoni ya Mnyika yanatakiwa yachukuliwe kama tahadhari japokuwa alitakiwa aje na sotution au kubainisha hayo mapungufu kwa undani ili wayafanyie kazi yasitokee