Trend Setting: Mapendekezo ya JF kwa mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yanayotarajiwa hivi karibuni

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,337
113,179
Wanabodi,

Trend Setting ni kutengeneza mwelekeo au ku shape jambo linalokuja kutokea. Trend Setters ni wale watu ambao wakifanya jambo fulani, sehemu kubwa ya jamii hulifuata.

JF ni trend setter, baadhi ya mapendekezo yanayotolewa humu JF, serikali yetu sikivu huyatekeleza.

Baada ya zoezi la Uchaguzi Mkuu kukamilika, JF ilitengeneza trend ya Baraza jipya la Mawaziri na mimi naamini baadhi ya wateule kama Joyce Ndalichako was made from JF: Mapendekezo ya wananchi: Muundo wa Baraza la Mawaziri kwa Serikali ya Awamu ya Tano.

Kufuatia teuzi za baadhi ya wabunge wapya kwenye Bunge la Muungano, Trend reading zinaelekeza kufanyika kwa mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri hivi karibuni huku sura mpya kama Prof. Palamagamba Kabudi, Anne Kilango Malecela na Salma Kikwete wakitarajiwa kuwemo.

Japo kwa mujibu wa katiba yetu kazi ya kuteua mawaziri ni kazi ya rais wa JMT kwa mashauriano na Makamo wa Rais na Waziri Mkuu, viongozi wetu hawa nao ni binaadamu na wanaweza kukosea katika uteuzi au kuna watu wazuri tuu lakini jicho la rais haliwezi kuwaona ila jicho la JF ni kubwa.

Ni ukweli usiofichika kuwa kwenye Baraza hili kuna mawaziri ambao kweli ni ma performers wengine beyond expectations, kuna mawaziri non performers yaani wapo wapo tuu ili mradi wapo na kuna mawaziri kiukweli kabisa wame flop, hawa ni mawaziri mizigo, they should go.

Pia kwenye wabunge kuna wabunge ambao ni great potentials kumsaidia rais kuliko kuendelea kubeba mizigo hadi 2020.

Hivyo wana JF, hakuna ubaya kumshauri rais wetu, ambaye ni mtumishi wetu, sisi ndio waajiri wake kupitia kura zetu na ndio tunaomlipa mshahara wake kupitia kodi zetu, hivyo atazingatia maoni na ushauri wetu kwa jinsi ile ile anavyozihitaji kura zetu.

Nikianzia na maoni yangu;

1. First and Foremost anza na huyu kijana mpendwa wako, unayependezwa naye, ambaye japo sii Waziri na sii mbunge bali alikuwa ni zaidi ya Makamo wa Rais, ni zaidi ya Waziri Mkuu, ni zaidi ya Spika, ni zaidi ya Jaji Mkuu, ni zaidi ya IGP. Kijana shupavu, shujaa, hodari, mchapakazi Paul Makonda, he was an asset like a jewel on the sea, a very big asset na ni kweli amefanya makubwa katika kipindi kifupi, but its very unfortunately he has now turned into the biggest liability you have!, deal with it first, the sooner the better!.

2. Asante kututeulia wabunge wanawake 4. Bado mmoja, huyu mmoja. Kwa uteuzi wako mmoja wa mwisho uliobakia kwa mujibu wa katiba, ambaye lazima uwe wa mwanamke, tunakuomba ututeulie mwanamke kutokea upinzani, preferably Mama Ana Mngirwa.

Mkapa aliteua kutoka upinzani, Kikwete aliteua kutoka upinzani, why not you?. Japo hakuna sheria, kanuni wala taratibu inayokulazimisha umteue nani, lakini unapokuwa ni rais wa wote kuna vitu lazima uvifanye kuwaonyesha watu kuwa wewe ni rais wa wote, na huo uwote wako uonekane kwa wote, kama ilivyo kwenye kutoa haki, "justice must not be only done,but it must be seen to be done" kuwa haki sio lazima tuu itendeke, bali pia lazima ionekane kutendeka, hata kama huupendi vipi upinzani, hata kama huwapendi vipi wapinzani, ni watu ambao wapo kisheria kwa mujibu wa katiba japo kazi yao kubwa ni kukusoa wewe na serikali yako lakini amini usiamini ni watu wa muhimu sana kwako, kwa serikali yako na kwa taifa kwa ujumla tena wanakusaidia sana tuu hata kama hujui.

3. Kwa vile umeisha teua wanawake wengine wawili, katika mabadiliko madogo utakayoyafanya this time naamini yataakisi gender mainstreaming kwenye mabadiliko ya baraza lako. Pale mwanzo umetutelia mawaziri wanawake wanne tuu na hatukulaumu kwa hilo kwa sababu waelewa tunaelewa sababu, haupaswi kuziendeleza hizo sababu, kama rais wa nchi kuna vitu lazima ubadilike: Tuacheni Kumlaumu Rais Kuteua Wanaume, TZ Hatuna Wanawake Wenye Sifa na Vigezo vya Kuteuliwa!

4. Kwa maoni yangu, Kabudi mpe wizara ya Sheria, atakusaidia sana. Mwakyembe kwa vile kabla hajawa mwanasheria, alikuwa mwana habari, na ni mtu very sensational, mpe wizara ya habari, ila ivunje, ondoa michezo na utamaduni, mwache Nape.
Japo Prof. Maghembe umempa ili tuu usionekane umewabagua Wachagga, kwanza Mpare sio Mchagga, pili kiukweli huyu ni mzigo, alikuwa mzigo tangu kwa Kikwete, nahadi sasa ni mzigo. Maliasili na utalii inahitaji mawaziri vijana, damu chemka na smart, sio tuu smart kichwani, bali hata anavyoonekana, usione aibu kumrudisha Nyalandu, au tafuta smart lady or gentlemen smart kichwani but she must look attractive atuvutie watalii, kama ni mwanaume then awe HB, watu hawa bungeni unao.
Prof. Mpango japo ni mchumi mzuri, lakini hana uwezo wa kukusaidia, uless kama unachobabaikia ni huo uprofesa wake lakini hakuna kitu. Wizara ya fedha tafuta mtu anaijua pesa. Kwenye mabadiliko yako, achana na kasumba za Kisukuma za kutothamini wanawake!, ongeza idadi ya wanawake na watu kama Bashe, watakusaidia sana, watumie. na kuna wizara umeziunganisha ili uonekane umetengeneza baraza dogo, lakini muunganiko huo doesn't make any sense at all!. Muda huu umeishatosha kukuonyesha baadhi ya hizo wizara hazina tija na wastage of money and resources. Hili nililisema hapa.
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa ...

Sasa wana JF wenzangu, naomba tutoe maoni yetu nani ame perform anastahili kubaki, au alikuwa naibu anastahili kuwa waziri kamili, nani ameflop na hamsaidii tena rais hivyo apumzishwe. Pia kuangazia potentials zilizopo kama tulivyo muangazia Pro. Ndalichako na hatimaye akawepo.

Naomba kuwasilisha.
Paskali
 
Japo sipingi wazo lako lakini kipaombele chetu kwa sasa ni hali ya uchumi. Kwa ujumla uchumi unadorora huku tukilishwa ahadi za matumaini kama awamu zilizopita. Sifa tunazoziona ni kushikishana adabu tena kwa utashi wa viongozi. Kwa ujumla uteuzi wa mawaziri sioni ukileta tija zaidi ya faida binafsi za mteuliwa. Sitarajii hilo baraza jipya kuja na ule utoto ulioanza nao awamu hii ya kwenda kufungia mageti wachelewaji mbele ya camera. Pia ni vizuri mngetuambia mafanikio na mapungufu ya baraza hili na sio kutuletea sura mpya lakini matokeo ni hayohayo ya mawaziri kusema kutekeleza nia njema ya rais wetu.
 
Pascali nikushauri. Unapotoa ushauri kwa ngosha epuka lugha ya mafumbo maana ni ukweli yeye haelewi.

Mfano, hapo ulipo Sema hizo sifa za kijana wake kuwa ni zaidi ya uliowataja yeye hawezi kujua kuwa unamkebehi bali atadhani ni sifa za ukweli na mambo yataharibika kwa kudhani Paskali (home boy) kanishauri hivi kumbe wewe ulimaanisha vile.

Angalia Paskali (homeboy wa mzee) usije tuharibia nchi kwa mafumbo yako.
 
Tanzania ya viwanda haipimiki kiurahisi, sababu :-
1. Ni vigumu kuaccount inputs ya serikali kwa kuwa kazi kubwa ni kuhamasisha sekta binafsi na si serikali kujenga viwanda!!!

2. Tanzania yenye uchumi imara (hapa tukitegemea kulijenga upya kundi la asilimia 70 la wakulima. Hii ni countable, measurable kwa kuwa leo ukiunda kundi la vijana takribani 40 40 kisha kipindi wahitimupo chuo kikuu ukawapa trekta na shamba dunia nzima hushuhudia tukio hili.) in short ni kuwa tusipowekezs ktk kundi hili tutafikia mafanikio kwa kuchelewa.

Sasa nani afaa atolewe na sababu zake:-
1. Prof. Magembe - maliasili kwake ni mzigo (labda abadirishiwe wizara) - miti inaendelea kukatwa hovyo.

2. Waziri wa kilimo - huyu hana ubavu wa kusimamia kauli juu ya kujadili mtizamo wa Mhe. JPM. Wakati baadhi ya maeneo yakiwa na uhaba wa chakula yeye aliungana na wanaoamini chakula kimejaa kwenye maghala huku CCM kikitukanwa mitaani,

3. sina muda ningeandika mengi
 
mawazo yako mazuri ila hapo kwa Daudi bashite hapana kweli ni mchapa kazi ila amepoteza sifa za kuwa Waziri, ubunge sawa ila uwaziri hapana yani mtu mwenye sifa ya darasa la saba aongoze wizara jamani huu utani

Maana kama kidato cha nne alipata alama sifuri ni sawa na darasa la saba, uyo hana sifa za kuwa Waziri

ikiwa hizi tuhuma zinasemwa ni uzushi alete vyeti watu wavione tatizo lipo wapi mbona watumishi wa umma kutwa wanaitwa kwenye uhakiki wanapeleka vyeti.
 
Mawaziri wafuatao wawekwe pembeni kwani morali wao umekata:-

Mahiga ( Sera zake hazifanyi kazi kwa Jpm maana hajui masuala ya Diplomasia)

January(hawaelewani na Naibu wake )

Waziri wa Viwanda( Huyu mpaka muda huu hajui anafanya nini na anaelekea wapi)

Nape (Morali umekata kwa sababu anaona Chama kinavurugwa badala ya kujengwa,kumbuka huyu kakulia na kulelewa kichama ni kada mahiri)

Naibu Waziri wa Maji( huyu ni mpiga kelele tu hajui hata majukumu yake)

Maghembe aka Faru John( huyu pumzi imekata)
 
Alipoanza kumsifia yule division ZERO tu nikajua anaelekea wapi, kiufupi umetumwa kuja kumsafisha bwana Daudi , nikupe pole kwakuwa huyu hasafichiki hata kwa still wire.
Kwa haya madudu ya Daudi nimepata picha ni aina gani ya Mukulu ambae anatuongoza...kimsingi hatuna hatua tunayopiga bali tunarudi nyuma
 
Mwakyembe - Apangiwe kazi ingine.

J Makamba - Kazi ingine.

P. Mipango - kazi ingine (japokuwa huyu ni cake kwa raisi na ni ngumu Rais kumchomoa lkn hakuna namna ndiye chanzo cha kutufanya wananchi kwa Sasa tunaishi km mashetani kutokana na ushauri wake kwa Rais kuwa siyo Mzuri, yeye ndiye chanzo cha kuweka kodi kwenye miamala ya fedha, utalii, 15% ya bodi ya mikopo etc. Ameshindwa hata kumshauri Rais ni vipi vyanzo sahihi vya mapato kwa inchi anachoweza yeye ni kuwasukumia wananchi mzigo wote anasahau kuwa anatengeneza serikali corrupt kwa wananchi wake).

M. Nchemba - Kazi nyingine, hiyo wizara atafute mtu kutoka Ata kwa wastaafu WA jeshi la wananchi ataweza kuikimbiza.

Pia huyo mtu wako uliyempendekeza Hana Aiba ya uongozi aishie huko huko kwenye u- RC, hakuna wizara anayoiweza.

Tumechoswa na viongozi wanaotuongoza kwa mihemuko, weka ukabila pembeni tuivushe inchi.
 
mawazo yako mazuri ila hapo kwa Daudi bashite hapana kweli ni mchapa kazi ila amepoteza sifa za kuwa Waziri, ubunge sawa ila uwaziri hapana yani mtu mwenye sifa ya darasa la saba aongoze wizara jamani huu utani

Maana kama kidato cha nne alipata alama sifuri ni sawa na darasa la saba, uyo hana sifa za kuwa Waziri

ikiwa hizi tuhuma zinasemwa ni uzushi alete vyeti watu wavione tatizo lipo wapi mbona watumishi wa umma kutwa wanaitwa kwenye uhakiki wanapeleka vyeti.

Chakaza kasema ukweli Paskal homeboy aache kusema kwa mafumbo juu ya wizi wa Bashite ndo maana jamaa huyu 'utandu' hakukuelewa, yaani kaelewa kuwa umemshauri Rais apandishe cheo Daudi Bashite wakati wewe umeimanisha amfukuze kazi na ashitakiwe according to law!
 
Pascali nikushauri. Unapotoa ushauri kwa ngosha epuka lugha ya mafumbo maana ni ukweli yeye haelewi.
Mfano, hapo ulipo Sema hizo sifa za kijana wake kuwa ni zaidi ya uliowataja yeye hawezi kujua kuwa unamkebehi bali atadhani ni sofa za ukweli na mambo yataharibika kwa kudhani Paskali (home boy) kanishauri hivi kumbe wewe ulimaanisha vile. Angalia Paskali (homeboy wa mzee) usije tuharibia nchi kwa mafumbo yako
 
Kwa Tanzania cabinet reshuffling haina tija yeyote zaidi ya kuwapa wengine zamu ya kula, mnakumbuka alipoingia alisema atateua baraza dogo lenye ufanisi hata jua halijakuchwa, the rest ni story.

Hivi tumejiuliza kwanini waliopo wapo kimya wanahofu gani.

B
inafsi sishauri lolote, kwanza hashauriki kila kitu anataka afanye yeye, rais yeye, waziri yeye, Spika yeye, Jaji mkuu yeye hadi anatamani kuwa IGP.

Naungana na upinzani maintaining calmness, keeping low profile, wastage of time let him do what he wants to do, akimaliza muda wake atatuachia Tanzania yetu aliyoikuta.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom