Treasury Bonds/T-bonds/T-Bills/Bonds/Hati Fungani ni Uwekezaji "Kichaa"

Mtamba wa Panya

JF-Expert Member
Aug 6, 2017
695
1,712
Hati fungani ni biashara "kichaa" na watu pekee ambao wanawekeza kwenye hii biashara ni wale waoga wakupoteza thamani ya mitaji ya pesa zao. Mabenki, mashirika ya bima, mifuko ya mafao pamoja na mashirika mengine bila shaka hutumia njia hii ya uwekezaji ili kutunza mitaji yao pengine ni kutokana na ukubwa wa mitaji ambao ni vigumu kuwekezwa kwenye sekta zenye "Higher Risk but greater return".

Tukichukulia mfano wa Hati fungani za miaka 20 za serikali zinazotoa riba ya 15.49% p.a: Angalia mtiririko ufuatao;

Tuchukulie umewekeza kiasi cha Tsh x kwa muda wa miaka hiyo 20, jumla kuu ya malipo utakayopata baada ya miaka 20 ni Tsh;

1569250687913.png
lakini kumbuka kuna kitu kimoja ambacho huzikumba FIAT Currency zote duniani, nacho ni Inflation au Mfumuko wa bei . Tukichukulia wastani wa 3.7% p.a (kwa mujibu wa takwimu za NBS [1], hapa naomba tusifikirie suala la "kupikwa" takwimu na naomba tuunge mkono juhudi) kwa muda wa miaka 20 hiyo ya uwekezaji wako. Then mtaji wako wa Tsh x baada ya miaka hiyo 20 utakuwa na thamani ya Tsh;

1569251391545.png
Hii inamaanisha faida ya uwekezaji wako kwa muda wa miaka 20 ni Tsh;

1569251887884.png
ambayo ni faida ya asilimia 100 kwa muda wa miaka 20; ambayo yenyewe kiuhalisia ni Tsh;

1569252938331.png
yaani kwa mahesabu ya "pesa yako ya kweli" ya miaka 20 iliyopita, faida yako ni asilimia 48.4 tu.

Hebu tuangalie mfano mwingine, iwapo mtu atawekeza kiasi kilekile cha Tsh x kwa muda wa miaka 20. Tukichukulia wastani wa faida ya asilimia 10 kwa mwaka, then baada ya miaka 20 mtaji wake utakuwa ni Tsh;

1569252313033.png
ambapo faida yako itakuwa ni Tsh;

1569252629255.png
yaani mara 4.659 ya mtaji wako wa awali, ambayo kiuhalisia ni faida ya Tsh;

1569253276070.png
yaani asilimia 225.3 kwa mahesabu halisi ya miaka 20 iliyopita.

sasa unaweza kuona kwamba kwa wastani wa faida ya asilimia 10 tu kwenye biashara yako kwa miaka 20 faida unapata asilimia 225.3 wakati kama utakuwa umewekeza kwenye hati fungani utakuwa umepata faida asilimia 48.4 tu japo utakuwa kwenye "risk free investment".

Je, kama utafanikiwa kupata faida ya wastani wa asilimia 20 kwa muda wa miaka 20 unaweza kupiga hesabu ni kwamba utapata faida kubwa zaidi. Yaani;

Baada ya miaka 20 mapato yatakuwa ni Tsh;

1569253746128.png
kumaanisha faida yako itakuwa ni Tsh;

1569253946211.png
ambayo kiuhalisia ni Tsh;

1569254155239.png
yaani faida ni mara 17.538 ya mtaji ulioanza nao "miaka 20 iliyopita"

Sasa unaweza kuona kwa faida ya kufanya biashara ukapata wastani wa 20% profit kwa miaka ishirini ni 1753.8% wakani hati fungani ni 48.4%.

Hakuna mfanyabiashara anayeelewa biashara akawekeza kwenye hati fungani labda kama hakuna namna na yeye anataka kulinda mtaji wake usishuke thamani.

Ahsanteni.
 

Attachments

  • 1569251638684.png
    1569251638684.png
    4.3 KB · Views: 93
  • 1569251680456.png
    1569251680456.png
    4.2 KB · Views: 90
  • 1569252416265.png
    1569252416265.png
    2.6 KB · Views: 94
Tatizo letu watanzania tumeshazoea kuwaza Iran vs USA. Lakini mambo sensitivities kama haya uwezi kuwaona hata maswali wanayouliza mpaka unaweza ukasikitika, na huyo mtu ana familiar ya watoto 4 mpaka 5.

Yaani watanzania akili zetu ni ndogo sana kuanzia maprofesa mpaka wasiosoma ni upuuuzi upuuuzi tuuu umasikini ndio umeshamiri tuuu na wengine maprofesa lakini akili kama watoto wa darasa la pili? Apo ungezungumzia kuhusu Iran vs USA sasa ivi tungekuwa tushafika mchangiaji wa 350.

Watanzania tunatakiwa tuwekeze kwy maswala ya mahesabu ya kibihashara na uwekezaji ili kuwa na jamiii bora isiyokuwa na shida ya maswala ya kifedha na kwy mitahara yetu wafundishe maswala ya fedha na uwekezaji maana mitahara yetu iko tofauti sana. Bado tunatumia mitahara ya zamani sana haiendani na dunia ya sasa

Ugali Maharagwe umeharibu akili za watanzania
 
Wataalam wa uchumi wanasema "Compound interest is eighth wonder of the world" wengi wanaoenda kuwezeza kwenye hizi bond hawana elimu ya kutosha unakuta mtu anachukua 50m ana nunua gov-bond kwa 10yrs for 12%cp-interest.

Akipewa ile certificate anaenda kuficha kwenye droo yake ya chuma huko chumbani ana subiri miaka kumi iishe hajui kua anaweza kuitumia hiyo hiyo kupata mkopo hadi 75% invested money(50m).

Hamna kitu kinalipa kama investiment kwenye Money market, capital market na stock market.

Hata mm kunakitu nimepamga kufanya juu ya hii sector, sema haitabiriki
 
Wataalam wa uchumi wanasema "Compound interest is eighth wonder of the world" wengi wanaoenda kuwezeza kwenye hizi bond hawana elimu ya kutosha unakuta mtu anachukua 50m ana nunua gov-bond kwa 10yrs for 12%cp-interest. akipewa ile certificate anaenda kuficha kwenye droo yake ya chuma huko chumbani ana subiri miaka kumi iishe hajui kua anaweza kuitumia hiyo hiyo kupata mkopo hadi 75% invested money(50m). hamna kitu kinalipa kama investiment kwenye Money market, capital market na stock market.

Hata mm kunakitu nimepamga kufanya juu ya hii sector, sema haitabiriki
Financial sekta ya Tanzania bado iko chini mnoo
 
Wataalam wa uchumi wanasema "Compound interest is eighth wonder of the world" wengi wanaoenda kuwezeza kwenye hizi bond hawana elimu ya kutosha unakuta mtu anachukua 50m ana nunua gov-bond kwa 10yrs for 12%cp-interest. akipewa ile certificate anaenda kuficha kwenye droo yake ya chuma huko chumbani ana subiri miaka kumi iishe hajui kua anaweza kuitumia hiyo hiyo kupata mkopo hadi 75% invested money(50m). hamna kitu kinalipa kama investiment kwenye Money market, capital market na stock market.

Hata mm kunakitu nimepamga kufanya juu ya hii sector, sema haitabiriki
Hiyo interest rate ya 12% ni kwa mwezi au kwa mwaka au kwa iyo miaka kumi? jibu
 
Mtamba wa Panya,
Kuweka mtaji kwenye hati fungani ile faida ina ongezeka kwenye mtaji je nayenyewe ina pigiwa hesabu ya faida yake au utaruhusiwa kuwa unaichukua faida kila mwaka mtaji unabaki pale pale
 
Wataalam wa uchumi wanasema "Compound interest is eighth wonder of the world" wengi wanaoenda kuwezeza kwenye hizi bond hawana elimu ya kutosha unakuta mtu anachukua 50m ana nunua gov-bond kwa 10yrs for 12%cp-interest. akipewa ile certificate anaenda kuficha kwenye droo yake ya chuma huko chumbani ana subiri miaka kumi iishe hajui kua anaweza kuitumia hiyo hiyo kupata mkopo hadi 75% invested money(50m). hamna kitu kinalipa kama investiment kwenye Money market, capital market na stock market.

Hata mm kunakitu nimepamga kufanya juu ya hii sector, sema haitabiriki
unaichukulia mkopo halafu unalipa ndani ya miaka 10 au
 
Kaazi Kweli.., Kweli....

Hivi unadhani dunia hii wote ni financial gurus na risk takers au wafanyabiashara ? Lolote likiwa na risk kuna uwezekano wa kupata sifuri.., sasa mtu kafanya kazi miaka yake yote alafu savings zake akiweka kwenye kitu chenye risk kikienda belly up what next... ?

Kwa kukuacha nakuachia extract ya Advantages ya Treasury Bonds..

Advantages of Treasury Bonds
Putting your money into Treasury bonds comes with pros and cons. Understand the advantages and decide if T-bonds are right for your financial strategy.

In addition to having no maintenance fees, Treasury bonds feature:

  • Guaranteed rate of return: You’re guaranteed a certain rate of return on your investment.
  • No value loss: Treasury bonds are considered extremely safe investments — because the government backs your principal investment, your money will not lose value.
  • Tax exemptions: You don’t have to pay state or local income tax on the interest you receive every six months.
  • Good for retirement: Because T-bonds are typically safer than stocks, you might find them useful if you’re looking toward retirement. In addition, they can help generate a steady stream of income through interest payments.
 
Back
Top Bottom