TRC na Ajali ya Dodoma: Kuna tatizo la kiutendaji

Hii ajali ya majuzi, treni kuacha njia baada ya mvua kubwa, limeniacha na maswali ambayo lazima yajibiwe.

Baada ya ajali mbaya ya train na MV Bukoba zilizotokea miaka ya My Mkapa, Awamu ya pili, nilitegemea tutakuwa kumetengenezwa Stand at Operating Procedures kwa kuendesha hivi vifaa vyetu cha mass transport.

Haingii akilini kuwa reli haikaguliwi KILA KABLA YA SAFARI.

Na haingii akilini kuwa ma Station Master kati ya vituo vikubwa viwili vya karibu hawakuwasiliana.

Na haingii akilini kuwa dereva wa train hakuwa na weather reports, na hali ya mito mbele ya safari yake.

Haingii akilini vile vile kwamba kusafiri kwa reli za TRC is a question of chance, kufika safari yako ni majaliwa.

Hata yote, TRC inapaswa kuyajibu.
Narudia kusema Tanzania ya leo ukilala njaa nisiri yako,usishangae mambo unayosema sii ya lazima kwakuwa tunayo makubwa na ya muhimu zaidi ya hayo yanayo hitaji gharama.
 
Miaka ya nyuma kulikua na gangs kati ya station moja na nyingine, kazi yao kubwa ilikua kukagua njia kati ya reli na reli na kisha kutoa taarifa kwa station masters. Sasa hivi hakuna hivyo vitu...
 
Narudia kusema Tanzania ya leo ukilala njaa nisiri yako,usishangae mambo unayosema sii ya lazima kwakuwa tunayo makubwa na ya muhimu zaidi ya hayo yanayo hitaji gharama.
Wakulima toka Mwanza wakifia Bahi, poa tu.
Au siyo?
 
Mkuu, uko sahihi keyman na SPWI wako responsible kuhusu hilo la ukaguzi. Kwa muda wa treni uliopita ni majira ya jioni kitu kinachomaanisha wahusika walikuwa wamekagua kuwa njia iko salama. Tatizo inawezekana shirika halijaweka utaratibu wa kufanya ukaguzi kwenye vipindi kama mvua au usiku hii pia huenda ikawa ni sababu ya ajali.
Hakika mkuu...
 
Reli ya kati imechakaa mvua kubwa ya dakika 30 inaweza ikabomoa tuta la rail wakat train imetoka kituo fulan kwend kituo fulani....

Rail ya tazara huwez kusikia ovyo mvua imesomba rail japokuw inapita ukanda wenye mvua kubwa na nyingi kwa mwaka..fikiria rail ya kati ingekuwa inapita sehemu Kama bonde la kilombero
Ni kweli reli ya TRC ujenzi wake ni wa kizamani sana.
Hata hii mpya inayojengwa kuna makosa yanaonekana hata kwa mtu asiye mtaalamu wa reli. Kuna maeneo ujenzi wa matuta hauna ubora na hauzingatii njia za maji. Tuta kubwa lakini halina karavati la kuruhusu maji kwenda upande mwingine.
Mifereji ya maji pembeni ya reli ni midogo sana.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
CHANZO CHA AJALI

Kwa mujibu wa mkuu wa kitengo cha uhusiano cha Shirika la Reli Tanzania (TRC), Jamila Mbarouk treni iliyopata ajali juzi ilikuwa na abiria 720, mabehewa ya abiria 10 na ya mizigo mawili, jumla 12.

Alisema treni hiyo iliwasili Dodoma saa 9:15 alasiri na iliondoka saa 11:40 jioni. “Treni iliwasili katika kituo cha Kigwe saa 12:25 na kuondoka saa 12:27,” alisema.



Jamila lieleza kuwa baada ya kuondoka kituo cha Kigwe ndipo treni hiyo ilikwenda kupata ajali baada ya injini yake na mabehewa sita ya abiria kuacha njia.

Chanzo cha ajali hiyo kimeelezwa ni mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia juzi na maji yalifurika hata kusomba kokoto juu ya tuta la reli na kuiacha inaning’inia, hivyo injini ya treni iliyumba na kupinduka ikifuatiwa na mabehewa sita.

“Kwa sasa hicho ndio tunachoweza kuwaambia lakini baada ya uchunguzi kamili wa tukio hili tutatoa taarifa kwa wananchi,” alieleza Jamila.

Mwananchi Newspaper
 
Back
Top Bottom