Transition period......

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,003
112,650
Baada ya Kikwete kutangazwa mshindi na tume ya uchaguzi (Ijumaa) kesho yake (Jumamosi) akaapishwa. Mwenzeni nilibaki na maswali kadhaa.

Hivi katiba yetu inasemaje kuhusu kuapishwa kwa raisi mpya? Maana nilijiuliza kama ingekuwa ndiyo Dkt. Slaa kashinda na kutangazwa mshindi Ijumaa hiyo na kesho yake kuapishwa, kungekuwa na smooth transition of power kweli?

Je, hili nalo ni moja ya mapungufu ya katiba yetu? Manake ni kama wanaharakisha tu kumwapisha huyo raisi mpya......
 
Huu ndio udikteta na ubinafsi wa wengi viongozi wetu wa kiafrika, kwangu ushindi wa Kikwete,Kibaki,Mugabe n.k makes no difference
 
Huu ndio udikteta na ubinafsi wa wengi viongozi wetu wa kiafrika, kwangu ushindi wa Kikwete,Kibaki,Mugabe n.k makes no difference

Yaani inashangaza kweli. Mtu anatangazwa mshindi leo halafu kesho anaapishwa. Na wageni waalikwa wanakuja kutoka za nje kama vile walikuwa wameshatonywa kuwa kaeni mkao wa kula Jumamosi tunamwapisha Mkwere.....huo mwaliko ulitumwa lini kama mshindi alitangazwa jana yake tu? Gademu!!!
 
Yaani inashangaza kweli. Mtu anatangazwa mshindi leo halafu kesho anaapishwa. Na wageni waalikwa wanakuja kutoka za nje kama vile walikuwa wameshatonywa kuwa kaeni mkao wa kula Jumamosi tunamwapisha Mkwere.....huo mwaliko ulitumwa lini kama mshindi alitangazwa jana yake tu? Gademu!!!

Ratiba ya kuapishwa iko wazi, yaani inaeleweka ni lini rais mpya ataapishwa. Wageni waalikwa wanapewa taarifa kuwa ni lini rais wa tanzania ataapishwa iwe mkwere kikwete kama ilivyokuwa au kama angekuwa mchaga slaa au mnyamwezi lipumba, kwa hiyo wao wageni wanakaa mkao wa kula
 
Baada ya Kikwete kutangazwa mshindi na tume ya uchaguzi (Ijumaa) kesho yake (Jumamosi) akaapishwa. Mwenzeni nilibaki na maswali kadhaa.

Hivi katiba yetu inasemaje kuhusu kuapishwa kwa raisi mpya? Maana nilijiuliza kama ingekuwa ndiyo Dkt. Slaa kashinda na kutangazwa mshindi Ijumaa hiyo na kesho yake kuapishwa, kungekuwa na smooth transition of power kweli?

Je, hili nalo ni moja ya mapungufu ya katiba yetu? Manake ni kama wanaharakisha tu kumwapisha huyo raisi mpya......

Wasiwasi wako tu. Hapakuwa na kosa lolote. Kwanza kumbuka kwamba rais akishatangazwa hakuna mamlaka yoyote ya kutengua matokeo yake. Kuapishwa kesho yake au baada ya mwezi ni mipangilio tu na wala hapana dosari yoyote. Wewe ulitaka aapishwe lini na kwa sababu zipi ?? Hivi Dr. Slaa angeshinda kungekuwa na haya yote??? Ana wabunge wangapi na mwenzake ana wangapi??? Halafu (Slaa) anataka kudanganya umma kuwa alishinda!!!! Padri kusema uongo ni jambo baya zaidi kuliko asiye na dini.
 
Ratiba ya kuapishwa iko wazi, yaani inaeleweka ni lini rais mpya ataapishwa. Wageni waalikwa wanapewa taarifa kuwa ni lini rais wa tanzania ataapishwa iwe mkwere kikwete kama ilivyokuwa au kama angekuwa mchaga slaa au mnyamwezi lipumba, kwa hiyo wao wageni wanakaa mkao wa kula
We unayejiita baba mtu, slaa sio mchaga ni mbulu.
 
Ratiba ya kuapishwa iko wazi, yaani inaeleweka ni lini rais mpya ataapishwa. Wageni waalikwa wanapewa taarifa kuwa ni lini rais wa tanzania ataapishwa iwe mkwere kikwete kama ilivyokuwa au kama angekuwa mchaga slaa au mnyamwezi lipumba, kwa hiyo wao wageni wanakaa mkao wa kula

Wewe baba fisi, kwa jinsi ulivyomkabila unawataja kwa ukabila wao na kumbe Slaa ni Mbulu ndugu, wewe ulijua mchaga maana mnasema Chadema ni ya Wachaga.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom