Trafiki pigeni marufuku hizi taa na angalieni honi

Alwaz

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,055
10,723
Kaitka miaka hii michache nyuma maendeleo ya teknolojia yamepelekea kutengenezwa taa za vimuli vimuli kwenye magari ambazo nionavyo mimi ni hatari kwa maisha yetu.

Nazungumzia zile taa za kuashiria kupinda au kusimama kwa vyombo vya moto. Taa hizi sasa zimekuwa zikitumika ovyo kiasi kwamba ishara zote zilizoziklitumika mwanzo hazina maana. Watumiaji wake huwa wanaona ni mapambo lakini zinaingiliana sana na ishara halisi za matumizi ya vyombo hivyo.

Unaweza ukawa nyuma ya chombo cha mwenzako na usijue kipi amekusudia ni kupinda kulia au kushoto au ni kusimama..
Nimewahi kushuhudia ajali iliyotokana na vimulimuli hivyo. Nionavyo mimi bila utaalamu wa usalama barabarani
Taa za kuashiria kupinda kulia na kushoto ziwe ni njano. Taa za kusimama ziwake maeneo hayo hayo lakini nyekundu.

Honi nzito sana iwe ni za malori makubwa, ukisikia bila kugeuka unajua semi linakuja hilo upishe mbali.
Honi za dala dala ziwe nyepesi kidogo
Honi za mabasi ya abiria ziwe nzito lakini nyembamba. Ukisikia hata gari haijajitokeza unajua basi la mikoani hilo linakuja na kadhalika.
 
Kaitka miaka hii michache nyuma maendeleo ya teknolojia yamepelekea kutengenezwa taa za vimuli vimuli kwenye magari ambazo nionavyo mimi ni hatari kwa maisha yetu.
Nazungumzia zile taa za kuashiria kupinda au kusimama kwa vyombo vya moto.Taa hizi sasa zimekuwa zikitumika ovyo kiasi kwamba ishara zote zilizoziklitumika mwanzo hazina maana.Watumiaji wake huwa wanaona ni mapambo lakini zinaingiliana sana na ishara halisi za matumizi ya vyombo hivyo.Unaweza ukawa nyuma ya chombo cha mwenzako na usijue kipi amekusudia ni kupinda kulia au kushoto au ni kusimama..
Nimewahi kushuhudia ajali iliyotokana na vimulimuli hivyo.Nionavyo mimi bila utaalamu wa usalama barabarani
Taa za kuashiria kupinda kulia na kushoto ziwe ni njano
Taa za kusimama ziwake maeneo hayo hayo lakini nyekundu.
Honi nzito sana iwe ni za malori makubwa,ukisikia bila kugeuka unajua semi linakuja hilo upishe mbali.
Honi za dala dala ziwe nyepesi kidogo
Honi za mabasi ya abiria ziwe nzito lakini nyembamba.Ukisikia hata gari haijajitokeza unajua basi la mikoani hilo linakuja. na kadhalika.
Vinginevyo waturudishe wote darasani kujifunza tafsiri mpya ya vimulimuli
 
Tatizo ni ujinga miongoni mwa madereva wengine.

Unakuta mtu mzima kaweka vimulimuli kwenye gari lake. Kama anapenda vimulimuli aende kufunga nyumbani kwake kuanzia nje ya nyumba, sebuleni, chumbani mpaka chooni, kuliko kuchanganya watu barabarani!

Kuna mzee alikuwa anaendesha Prado TX kaweka taa za vimupimuli mbele, hivyo ukipishana nae zinakuchanganya machoni.
 
Washakataza sana

Washapiga marufuku sana

Tatizo wabongo wabishi,kila mtu anataka aonekane mtu wa kitengo

Nchi ngumu sana hii

Ova
 
Kaitka miaka hii michache nyuma maendeleo ya teknolojia yamepelekea kutengenezwa taa za vimuli vimuli kwenye magari ambazo nionavyo mimi ni hatari kwa maisha yetu.

Nazungumzia zile taa za kuashiria kupinda au kusimama kwa vyombo vya moto. Taa hizi sasa zimekuwa zikitumika ovyo kiasi kwamba ishara zote zilizoziklitumika mwanzo hazina maana. Watumiaji wake huwa wanaona ni mapambo lakini zinaingiliana sana na ishara halisi za matumizi ya vyombo hivyo.

Unaweza ukawa nyuma ya chombo cha mwenzako na usijue kipi amekusudia ni kupinda kulia au kushoto au ni kusimama..
Nimewahi kushuhudia ajali iliyotokana na vimulimuli hivyo. Nionavyo mimi bila utaalamu wa usalama barabarani
Taa za kuashiria kupinda kulia na kushoto ziwe ni njano. Taa za kusimama ziwake maeneo hayo hayo lakini nyekundu.

Honi nzito sana iwe ni za malori makubwa, ukisikia bila kugeuka unajua semi linakuja hilo upishe mbali.
Honi za dala dala ziwe nyepesi kidogo
Honi za mabasi ya abiria ziwe nzito lakini nyembamba. Ukisikia hata gari haijajitokeza unajua basi la mikoani hilo linakuja na kadhalika.
... siku hizi bodaboda na bajaji wanafunga honi za semi! Hatari sana.
 
Tatizo Polisi HAWAWEZI kusikilizwa mana hawana maamuzi nje ya SHERIA nyingine hata kama SHERIA inawapa mamlaka hayo. Kuna TBS wanatakiwa waoige marufuku uingizwaji wa hizo taa.

Makontena ya hiyzo taa kila kukicha yanaingizwa Toka China. Na wanaoinguza utakuta ni wafanyabiashara waoshirikiana na hao wakubwa. Sasa huku chini watu wanakamatwa lakini aliyeingiza hizo zana hatari hakamatwi Wala makontena yake kuziwa na kuharibiwa.

Tuache tuu inyeshe tutajua panapovuja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom