mandella
JF-Expert Member
- Oct 29, 2011
- 3,048
- 3,227
Aisee inakera bana. Hii ni too much, nasema tena hii ni TOO MUCH. Ni experience mbaya sana ndani ya mkoa huu.
Juzi nimeombwa Elfu tano na Traffic zaidi ya Mara tatu kwa Siku moja,na hapo ni ndani ya mji, nikawa nawagomea wote, sasa mmoja akang'ang'ania leseni yangu katika mabishano akabadili kesi kuwa eti nimevuka Zebra.
Nikamuuliza mbona ulivyonikamata hukuniambia kuwa nina kosa, kwanza nikamcheka kwa dharau, na mimi nikamuuliza pale nilisimama au sikusimama embu kuwa mkweli?
Akajibu ulisimama Ila kuna watu walikuwepo hapo, nikamuuliza kama nilisimama na hawajaruka je lilikuwa ni jukumu langu kushuka na kwenda kuwavusha. Akasema kwa hilo Utajua wewe ngoja uichangie serikali, akanipiga fine.
Kumbuka hapo kulikuwa na watu wamesimama wanapiga zao story hata hawana habari ya kuruka. Nilimlaani tu na kumwambia mafanikio yako ni machache mno kwenye maisha ya baadae.
Nikaondoka, ila sababu ya yote ni kumnyima anachookiita hela ya lunch.
Wakikusimamisha wanakutupia Kijitabu au Note Book, wanakuambia Weka Chochote huko.
Najiuliza Hivi vitabu na Note books wanazishika za kazi gani? Hivyo ndio vikapu vyao vya Kuwekea Rushwa.
Halafu wapo wengi mno ndani ya mji! Wasambazeni embu ikiwezekana wasambazeni huko Kigoma Mtwara na miji mipya mingine.
Juzi nimeombwa Elfu tano na Traffic zaidi ya Mara tatu kwa Siku moja,na hapo ni ndani ya mji, nikawa nawagomea wote, sasa mmoja akang'ang'ania leseni yangu katika mabishano akabadili kesi kuwa eti nimevuka Zebra.
Nikamuuliza mbona ulivyonikamata hukuniambia kuwa nina kosa, kwanza nikamcheka kwa dharau, na mimi nikamuuliza pale nilisimama au sikusimama embu kuwa mkweli?
Akajibu ulisimama Ila kuna watu walikuwepo hapo, nikamuuliza kama nilisimama na hawajaruka je lilikuwa ni jukumu langu kushuka na kwenda kuwavusha. Akasema kwa hilo Utajua wewe ngoja uichangie serikali, akanipiga fine.
Kumbuka hapo kulikuwa na watu wamesimama wanapiga zao story hata hawana habari ya kuruka. Nilimlaani tu na kumwambia mafanikio yako ni machache mno kwenye maisha ya baadae.
Nikaondoka, ila sababu ya yote ni kumnyima anachookiita hela ya lunch.
Wakikusimamisha wanakutupia Kijitabu au Note Book, wanakuambia Weka Chochote huko.
Najiuliza Hivi vitabu na Note books wanazishika za kazi gani? Hivyo ndio vikapu vyao vya Kuwekea Rushwa.
Halafu wapo wengi mno ndani ya mji! Wasambazeni embu ikiwezekana wasambazeni huko Kigoma Mtwara na miji mipya mingine.