Faana
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 31,677
- 32,983
Jana majira ya saa 5 asubuhi tulipanda daladala moja inayokwenda UDOM, ilitoka na abiria kadhaa waliosimama, kufika eneo la posta na kuendelea likajaza abiria kupita kiasi, na yapata kilomita moja toka hapo kuna askari wa usalama barabarani waliokagua basi lile na kuliruhusu kuendelea na safari, baada ya kufika kwenye ule mlima karibu na ukumbi wa Chimwaga, gari likazidiwa na kuzima, dereva akawa analalizisha kuliwasha huku likitaka kuporomoka kurudi nyuma, baada ya abiria kupiga kelele za kumlazimisha kondakta afungue mlango naye akiwa hataki ndipo wakatoa vitisho akafungua na abiria kushuka huku wengine wakibaki ndani na dereva akijaribu kuliondoa kwa lazima lakini likawa linarudi nyuma huku kondakta akiweka mawe na mengine yakikatika.
Binafsi niliona ile ni hatari kwasababu eneo lile lina kona kali na mteremko mkali pia, ipo haja kwa vyombo hivyo viwili kushirikiana kukagua usalama wa daladala za UDOM, hasa msongamano/ujazaji wa abiria na pia kama magari yale yapo salama.
Hata hivyo nilishangaa baada ya muda dereva aligeuza gari kwa namna anayojua yeye na kuondoka kurudi mjini huku abiria wakitelekezwa eneo la tukio.
Binafsi niliona ile ni hatari kwasababu eneo lile lina kona kali na mteremko mkali pia, ipo haja kwa vyombo hivyo viwili kushirikiana kukagua usalama wa daladala za UDOM, hasa msongamano/ujazaji wa abiria na pia kama magari yale yapo salama.
Hata hivyo nilishangaa baada ya muda dereva aligeuza gari kwa namna anayojua yeye na kuondoka kurudi mjini huku abiria wakitelekezwa eneo la tukio.